20/04/2025
Mkaguzi Mkuu wa Elimu Zanzibar Bi Maimuna Fadhil Abass akiwa katika picha ya pamoja katika ghafla ya kuwaaga wastaafu wawili ndugu Ali Nassor Hamad na Bi. Shuweikha Massoud Omar iliofanyika katika ukumbi wa Chuo Cha Ualimu WIARC Wete Pemba
14/04/2025
Mkaguzi Mkuu wa Elimu Zanzibar Bi. Maimuna Fadhil Abas amewataka Walimu Wakuu kuandaa mikakati ya kuwawezesha Walimu kuanzisha mpango wa utakaowawezesha Wanafunzi kusoma vizuri, kuandika na kuhesabu.
Wito hua ameutoa kwa nyakati tofauti wakati akizungumza na Walimu Wakuu katika Mafunzo ya SBI yaliyofanyika katika Ukumbi wa Kituo Cha Walimu Michakaini na Wingwi Kisiwani Pemba.
Amesema Mafunzo ya SBI yatawawasaidia Walimu kusaidiana wenyewe na kuepusha dharau baina yao.
Aidha amesema Mafunzo hayo ya SBI yatasaidia kuwaandaa Wanafunzi wa Msingi kuingia Sekondari wakiwa na uwezo na kupunguza mzigo kwa Walimu wa Sekondari.
Akielezea zaidi kuhusu umuhimu wa mafunzo hayo Bi. Maimuna amesema yatawapa Walimu fursa ya kuangalia changamoto zao zinazowakabili nakuzitafutia suluhisho.
Nae Mkuu wa Kitengo Cha Mafunzo kazini. Ndg. Rashid Masheko Ali amesema lengo la Mafunzo hayo ni kuwasaidia Walimu waweze kujiendeleza wenyewe wanapokua maeneo yao ya kazi.
Amesema ili kuwapa hamasa walimu, Kitengo kitatoa zawadi kwa Walimu ambao watayafanyia kazi kwa vitendo mafunzo hayo.
Kwa upande wake Mratibu Idara ya Mafunzo ya Ualimu Mwalimu. Khamis Yahya amesema Mafunzo ya SBI yatawasaidia Walimu kuweza kushirikiana na kufanya mambo yao kwa pamoja.
Imetolewa na Kitengo cha Habari na Mawasiliano (OCIE )
07/11/2024
Mkuu wa Ukaguzi Mkoa wa Kaskazini Unguja Nd. Bakili Haji Iddi akiwasilisha Ripoti ya Ukaguzi ya Mkoa wa Kaskazini Unguja mwaka 2023/2024 kwa wadau wa Elimu wa Mkoa huo kwa lengo la kuelewa na kuimarisha utendaji juu ya kuzitatua changamoto ambazo zimejitokeza katika mwaka huo Hafla hiyo ilifanyika katika ukumbi wa Skuli ya Sekondari Mkwajuni
07/11/2024
Wakaguzi wa Elimu katika Mikoa mitatu ya Unguja wakishiriki katika mafunzo ya Mtaala wa CBC ikiwa na dhumuni la kuelewa na kutekeleza katika kazi zao ili mafunzo hayo yaliendeshwa kwa kushirikiana na shirika la KOICA la Tanzania
07/11/2024
Watendaji kutoka Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Elimu Zanzibar wakishiriki katika mafunzo ya Sheria yalioendesha na Mwanasheria wa Ofisi Ndug. Subira M***a Kheir kwa lengo la kuwawezesha kujua sheria na wajibu katika kutekeleza majukumu ya Ofisi pamoja na Utendaji kazi wao mafunzo hayo yalikuwa ya siku katika ukumbi wa Kiembe Samaki Teacher Training Center
08/05/2024
Mkaguzi Mkuu wa Elimu Zanzibar Bi. Maimuna Fadhil Abass pamoja na Mratibu wa Ukaguzi Pemba Dr. Amour Rashid Ali wakiwa katika Ufunguzi wa mafunzo ya upimaji kwa walimu wa skuli za maandalizi na msingi.
yenye lengo kuu la kuwasaidia wanafunzi wa levels za chini (Lower primary) hususan wale wenye uwezo mdogo wa kusoma, kuandika na kuhesabu.
19/04/2024
Wakaguzi wa Elimu Mkoa wa Mjini magharibi wakiwa kwenye mafunzo endelevu yakujadili vipengele na muongozo wa ukaguzi kwenye ngazi za elimu Msingi , Maandalizi na Sekondari kwa dhumuni la kuimarisha utendaji kazi ili kuiwezesha dira na dhamira kuwa kituo bora cha ukaguzi wa Elimu
18/04/2024
Wakaguzi kutoka Mkoa wa Mjini Magharibi wakiwa katika mafunzo ya utekelezaji wa Mtaala mpya wa umahiri wa ngazi ya maandalizi na msingi ili kuweza kuimarisha utendaji kazi katika majukumu yao mafunzo hayo yamefanyika leo katika Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Elimu Zanzibar
21/03/2024
Watendaji kutoka Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Elimu Zanzibar wakishiriki katika hafla ya ugawaji wa vyeti vya wahitimu wa mafunzo ya muda mafupi yaliyoendeshwa na Shirika la Goodneighbour Tanzania chini ya usimamizi wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar....
18/03/2024
Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri kutoka Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Elimu Zanzibar Mh. Hussein Ali Suleiman pamoja na Mkaguzi Mkuu wa Elimu Zanzibar wakiwa kwenye picha ya pamoja na Wakaguzi wapya katika kikao cha Ufunguzi wa Mafunzo .
Mafunzo hayo yameanza leo Jumatatu tarehe 18-March 2024 hadi siku Ijumaa ambayo ni sawa na tarehe 22 March kwa madhumuni ya kuwajengea uwezo na umahiri wakati wa Utendaji kazi zao
18/03/2024
Wakaguzi kutoka Mkoa wa Mjini Magharibi wakisoma Ripoti ya Ukaguzi kwenye Mkoa huo kwenye kikao cha pamoja na Walimu Wakuu kikao hicho kiliendeshwa na Shirika la GoodNeighbour kwa madhumuni ya kuboresha ustawi wa Elimu Zanzibar
19/02/2024
Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri kutoka Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Elimu Zanzibar Mh. Hussein Ali Suleiman akiwa kwenye mkutano wa pamoja na Wakaguzi kutoka Mikoa yote ya Unguja wakijadili namana ya kuimarisha misingi ya utendaji kazi na uwajibikaji ili kuweza kuleta maendeleo kwenye sekta ya Elimu
Mkutano huo pia ulishirikisha wajumbe mbali mabli kutoka kwenye Bodi ya Ushauri kutoka Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Elimu Zanzibar na wakiwataka Wakaguzi kuengeza bidi ya utendaji kazi kwa kuimarisha mashirikiano baina ya Walimu .