05/06/2026
engeneers
vocational
kist
karume
tanzania
zanzibar
all
Karume Institute of Science and Technology (KIST) is a parastatal organisation under the Ministry of
05/06/2026
engeneers
vocational
kist
karume
tanzania
zanzibar
all
03/06/2026
vocational
kist
karume
tanzania
zanzibar
al
30/05/2026
NOW IN PEMBA !!!!
JOIN US !!!!
29/05/2026
JOIN US NOW !!!
27/05/2026
27/05/2026
vocational
kist
karume
tanzania
zanzibar
14/05/2026
Leo, tarehe 14 Mei 2026, Uongozi wa Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Karume (KIST) umefanya mazungumzo na Bodi ya Wahandisi kutoka Tanzania Bara pamoja na Bodi ya Wahandisi ya Zanzibar kwa lengo la kuimarisha ushirikiano wa kitaaluma na maendeleo ya Sekta ya uhandisi nchini.
Katika mazungumzo hayo, pande zote zilijadili njia mbalimbali za kuwajengea uwezo Wanafunzi kuhusu umuhimu wa kujiunga na Bodi za Wahandisi mara baada ya kuhitimu masomo yao, hatua ambayo itawawezesha kukuza taaluma zao, kuendeleza vipaji vya ubunifu na uhandisi, pamoja na kuzitambua fursa mbalimbali zinazopatikana kupitia bodi hizo za kitaaluma.
Pia Wanafunzi walipata elimu kuhusu majukumu ya Bodi za Wahandisi, taratibu za usajili wa kitaaluma, maadili ya kazi, pamoja na umuhimu wa kuwa sehemu ya Jumuiya za kitaaluma katika kujenga Taifa lenye wataalamu wenye uwezo na viwango vya kimataifa.
Mazungumzo hayo yameonesha dhamira ya pamoja ya kuendelea kuwawezesha vijana kitaaluma, kuwajengea ushindani wa kimataifa, na kuandaa kizazi chenye mchango mkubwa katika maendeleo ya Sekta ya Sayansi, Teknolojia na Uhandisi.
13/05/2026
Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Karume (KIST), kupitia Idara ya Mawasiliano ya Anga, Elektroniki na Kompyuta, leo tarehe 13 Mei 2026, imefanya kikao maalum cha kupitia na kuboresha Mtaala wa Fani ya Data Science and Artificial Intelligence (AI).
Kikao hicho kilikuwa na lengo la kujadili, kupokea maoni pamoja na mapendekezo mbalimbali yatakayosaidia kuimarisha mtaala huo ili uendane na maendeleo ya Teknolojia, mahitaji ya Soko la ajira, pamoja na mabadiliko ya dunia ya kidijitali.
Wadau mbalimbali kutoka Taasisi za Serikali na Sekta Binafsi walishiriki katika kikao hicho kilichofanyika katika Taasisi ya Karume Mbweni, Zanzibar, ambapo walitoa michango yenye lengo la kuhakikisha programu hiyo inazalisha wahitimu wenye ujuzi, ubunifu na uwezo wa kushindana kimataifa katika nyanja za Sayansi ya Takwimu na Akili Unde.
Hatua hiyo inaonesha dhamira ya Taasisi ya Karume katika kuendelea kuimarisha ubora wa elimu ya juu ya Teknolojia na kuendana na kasi ya maendeleo ya Sayansi na Teknolojia duniani.
07/05/2026
Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Karume (KIST) imesaini hati ya ushirikiano na Kampuni ya Growth Energy Solution inayojihusisha na matumizi ya nishati ya Umeme katika vyombo vya moto.
Kwa upande wa Taasisi ya Karume hati hiyo imesainiwa na Mkuu wa Taasisi ya Sayansi na Teknolojia Dkt.Mahmoud Abdulwahab Alawi, na kwa upande wa kampuni ya Growth Energy imesainiwa na Meneja mwendeshaji wa kampuni hiyo Bwana John Okoro.
Lengo kuu la kuanzisha ushirikiano huo ni kuhakikisha kuwa Zanzibar inapata wataalamu, vifaa pamoja na ujuzi wa kutumia ,kutengeneza na kukarabati vyombo vya usafiri vinavyotumia nishati ya umeme.
Mbali na nushirikiano huo , kampuni ya Growth Energy kwa kushirikiana na Taasisi ya Karume imewapatia mafunzo baadhi ya wakufunzi na wahandisi wa Umeme na magari , ikiwa ni hatua ya awali ya kuhakikisha lengo la ushirikiano huo linafikiwa kwa wakati.
01/05/2026
KIST YASHIRIKI MAADHIMISHO YA MEI MOSI ZANZIBAR.
Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Karume (KIST), leo tarehe 01 Aprili 2026, imeshiriki katika kilele cha maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Mosi) kilichojumuisha maonesho ya Mabanda, Magari, Boda Boda pamoja na Bajaji yaliyofanyika Dole, Kizimbani Zanzibar.
Hafla hiyo imehudhuriwa na Mgeni rasmi , ambaye ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi.
Maadhimisho hayo yamekusanya Wafanyakazi kutoka Sekta mbalimbali za Serikali na Binafsi kwa lengo la kutambua mchango wao katika maendeleo ya jamii na Taifa kwa ujumla.
Kauli mbiu ya mwaka huu ni “Upatikanaji wa haki na mazingira bora kazini ni msingi wa uwajibikaji, nidhamu na maadili ya Wafanyakazi.” Kauli hiyo inalenga kuhimiza umuhimu wa kulinda haki za Wafanyakazi pamoja na kuboresha mazingira ya kazi ili kuongeza ufanisi, uwajibikaji na maadili mema kazini.
Ushiriki wa KIST katika maadhimisho hayo unaonesha dhamira yake ya kuunga mkono juhudi za kitaifa za kuimarisha ustawi wa Wafanyakazi na kukuza maendeleo endelevu kupitia elimu, Sayansi na Teknolojia.
vocational
kist
karume
tanzania
zanzibar
all
| Monday | 07:30 - 16:00 |
| Tuesday | 07:30 - 16:00 |
| Wednesday | 07:30 - 16:00 |
| Thursday | 07:30 - 16:00 |
| Friday | 07:30 - 16:00 |