05/02/2026
TANGAZO LA NAFASI ZA MASOMO MUHULA WA MACHI 2026/2027
CHUO CHA IMPERIAL COLLEGE OF HEALTH AND ALLIED SCIENCES (ICHAS), KINATANGAZA NAFASI ZA MASOMO KWA MWAKA 2026/2027
1. STASHAHADA YA UUGUZI NA UKUNGA (NURSING AND MIDWIFERY)
Cheti cha D 4 za Physics, Biology, Chemistry na D moja ya somo jengine
2. STASHAHADA YA UFAMASIA (PHARMACEUTICAL SCIENCES)
Cheti cha D 4 za Chemistry, Biology na D 2 za masomo mengine
3. STASHAHADA YA UTABIBU WA MENO (CLINICAL DENTISTRY)
Cheti cha D 4 za Physics, Biology, Chemistry na D ya somo jengine
KOZI ZINA MKOPO WA SERIKALI, ADA ZETU NI NAFUU NA ZINALIPWA KWA AWAMU
FANYA MAOMBI KUPITIA: www.maombi.ichas.ac.tz AU FIKA CHUONI KISAUNI NJIA YA PANGANI
MAWASILIANO:
+255(0)778454565, +255(0)621120720
Email: [email protected],
Website: www.ichas.ac.tz
MWISHO WA MAOMBA NI MACHI 31, 2026
KARIBUNI SANA!!
03/12/2025
BODI YA USHAURI ICHAS YAKUTANA
Bodi ya Ushauri ya Chuo Cha Afya cha Imperial College of Health and Allied Sciences (ICHAS) imefanya kikao cha kawaida cha kalenda ya muhula wa mwisho wa mwaka 2025 kuhusu tathmini ya utekelezaji wa mambo mbalimbali ya kiutendaji, kitaaluma na kisera.
Kikao hicho chenye kuleta tija kwa Chuo kiliongozwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri Dr. Omar Dadi Shajak kilifanyika siku ya Jumamosi Disemba 29, 2025 katika Jengo la Chuo lililopo Kisauni, Wilaya ya Magharib 'B' Mjini Zanzibar.
Aidha, wajumbe wa bodi walijadili maendeleo ya kitaaluma ya wanafunzi hususani matokeo ya mwisho wa muhula wa mwisho wa mwaka wa masomo 2023/2024 na matokeo ya muhula wa kwanza wa 2024/2025 ambapo walitoa pongezi kwa maeneo ambayo yamefanya vizuri na kuwasihi walimu kuongeza jitihada maeneo yenye mapungufu.
Pia, kikao kiliridhishwa na namna Chuo hicho kinavyoendesha mafunzo kwa uweledi na kilisisitiza kuongeza umahiri kwa wanafunzi na kuhakikisha Chuo kinatoa wahitimu walio bora kitaaluma na watakaoweza kushindana kwenye soko la ajira.
Kwa upande wa wajumbe kikao cha bodi ya ushauri kinachofanyika mara moja kwa kila muhula, hivyo kukamilisha vikao viwili kwa mwaka kilihudhuriwa na; Mwenyekiti wa bodi, Katibu, wajumbe, sekretarieti, mwakilishi wa serikali ya wanafunzi na wageni wengine waalikwa.
Sambamba na hayo, Uongozi wa Chuo hicho uliwatunuku vyeti Wajumbe wote ikiwa ni zawadi kwa utendaji wao nzuri wa kazi kwa muda wa miaka mitatu katika uendeshaji wa Bodi hiyo.
20/10/2025
TANGAZO LA NAFASI YA AJIRA KWA CHUO CHA ICHAS!!!
23/09/2025
Kwa Wahitimu wa Kidato cha nne na cha sita, udahili unaendelea...
Fanya Maombi sasa ujiunge na Diploma ya Fundi Usanifu Madawa/Ufamasia (Pharmaceutical Sciences) kwa ufaulu wa alama D4 (Kemia, Biolojia na D2 nyengine ukitoa Dini na Kiarabu)
Na Diploma ya Uuguzi na Ukunga (Nursing and Midwifery) kwa ufaulu wa alama D4 tu (Fizikia, Kemia, Bailojia na D1 nyengine ukitoa Dini na Kiarabu)
Pia utapata Mkopo wa masomo kutoka Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu.
Jiunge na:
Imperial College of Health and Allied Sciences (ICHAS)
"Enlightening The Future"
.ichas.ac.tz
.ichas.ac.tz
22/09/2025
Kwa Wahitimu wa Kidato cha nne na cha sita, udahili unaendelea...
Fanya Maombi sasa ujiunge na Diploma ya Fundi Usanifu Madawa/Ufamasia (Pharmaceutical Sciences) kwa ufaulu wa alama D4 (Kemia, Baiolojia na D2 nyengine ukitoa Dini na Kiarabu)
Diploma ya Uuguzi na Ukunga (Nursing and Midwifery) kwa ufaulu wa alama D4 tu (Fizikia, Kemia, Bailojia na D1 nyengine (ukitoa Dini na Kiarabu)
Pia utapata Mkopo wa masomo kutoka Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu.
Jiunge na:
Imperial College of Health and Allied Sciences (ICHAS)
"Enlightening The Future"
.ichas.ac.tz
.ichas.ac.tz
09/01/2025
ICHAS washiriki uchangiaji damu salama
Chuo cha Imperial College ofa Health and Allied Sciences kwa kushirikiana na wadau mbali mbali pamoja na vyuo vyengine vya afya vilivyopo Zanzibar wameshiriki katika zoezi la mpango wa taifa wa uchangiaji damu salamaa
Zoezi hilo limeandaliwa na Kituo cha afya cha Urban Care Clinic kwa kushirikiana na Wizara ya Afya Zanzibar pamoja na Wadau wa Mpango uchagiaji wa damu salama wa Taifa limefanyika leo Alhamis Januari 9, 2025 katika Kituo cha 'Urban Care Clinic' kilichopo Nyamanzi Wilaya ya Magharib 'B' Mkoa wa Mjini Kisiwani Unguja
Mpango huo Uchangiaji damu salama wa taifa umefanyika ikiwa ni muendelezo wa shamra shamra za kuazimisha miaka 61 ya Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964 ambapo watu mbali mbali walijitokeza kuchangia damu kwa hiari
29/12/2024
ICHAS WAUNGANA NA SUZA, ZSH, GLORIOUS NA TAPSA KATIKA UZINDUZI WA 'UVIDA'
Wanafunzi vyuo vya Imperial College of Health and Allied Sciences (ICHAS), State University of Zanzibar (SUZA), Zanzibar School of Health (ZSH) na Glorious Polytechnic wa Kada ya Ufamasia kwa ngazi ya Stashahada (Diploma) wakiwa katika picha za pamoja kwenye shughuli ya Uzinduzi katika kampeni ya Usugu wa Vimelea katika Dawa (UVIDA)
Kampeni hiyo imeandaliwa na Chama cha Wanafunzi Wafamasia Tanzania (TAPSA) kwa kushirikiana na Wizara ya Afya Zanzibar imefanyika leo Disemba 29, 2024 katika Ukumbi wa (ICHAS) uliopo Kisauni, Unguja ambapo mgeni Rasmi alikuwa Waziri wa Afya Zanzibar Mh. Nassor Ahmed Mazrui.
Aidha Kampeni hiyo ilihudhuriwa na Rais wa Tanzania Pharmaceutical Students Association (TAPSA) Ndugu Sahad Senyuyuma pamoja na wataalamu mbali mbali wa afya kutoka Hospital kuu ya Mnazi mmoja
Uzinduzi huo pia ulihudhuriwa na Viongozi mbali mbali vya vyuo hivyo wakiongozwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri wa Chuo cha Imperial College of Health and Allied Sciences Dr. Omar Dadi Shajak pamoja na Mkuu wa chuo Dokta Jamila Hassan Kingwaba
Katika kampeni hiyo, Wafamasia walitakiwa kuisaidia jamii kutoka katika janga la usugu wa vimelea dhidi ya dawa, kuepuka kutoa dawa kiholela pomoja na madhara ya kutumia dawa kiholela bila ushauri wa daktari
13/12/2024
MATUKIO KATIKA PICHA WAKATI WA KUAPISHWA RAIS MTEULE ICHASSO, LEO IJUMAA DISEMBA 13, 2024
12/12/2024
MUZNE RAIS MPYA ICHASSO 2024-2025
Tume ya Uchaguzi ya Serikali ya Wanafunzi chuo cha Imperial College of Health and Allied Sciences imemteuwa Muzne Abdallah Yussuf kuwa Rais wa Serikali ya Wanafunzi wa chuo hicho kwa kipindi cha mwaka 2024-2025
Uteuzi huo umefanyika leo Alhamis Disemba 12, 2024 chuoni hapo baada ya kufanyika Uchaguzi uliowashirikisha Wagombea wawili Muzne Abdallah Yussuf na Is-haka Suleiman Said pamoja Makamo wao Yasir Massoud Shafii na Nassra Said Makame
Tume hiyo imemtangaza Muzne Abdallah Yussuf kwa ushindi wa 66.76% huku mpinzani wake Is-haka Suleiman Said akipata 28.26% na ambapo 5% ya kura zilizopigwa ziliharibika
Uchaguzi huo ulihudhuriwa na ndugu Shehe ambaye ni Afisa wa elimu kutoka Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar (WEMA) katika Kitengo cha Uratibu Elimu ya Juu Zanzibar pamoja Maafisa Waandamizi kutoka Shirikisho la Vyuo vikuu na Taasisi za Elimu ya Juu Zanzibar (ZAHILFE)
Rais mteule huyo pamoja na Makamo wake Yassir Mohammed Shafii wanatarajiwa kuapishwa kesho siku ya Ijumaa Disemba 13, 2024 saa 8 za mchana katika Ukumbi Mpya (New Hall) uliopo chuoni hapo
Muzne Abdallah Yussuf anakuwa Rais wa pili kutoka chuo cha Imperial College of Health and Allied Science tangu kuanzishwa kwake mwaka 2022 baada ya Ahmed Yassir Juma kumaliza muda wake.