11/10/2021
MELKIZEDEKI NI NANI?
Kuhani Mkuu, Mfalme na kiongozi katika Agano la Kale aliyeishi baada ya gharika na katika wakati wa Ibrahimu. Aliitwa mfalme wa Salemu, mfalme wa amani, mfalme wa haki (ambayo kwa Kiebrania ndiyo maana ya neno Melkizedeki), na kuhani wa Mungu Aliye Juu Sana. Yeye ndiye kuhani wa kwanza anayetajwa katika Maandiko; alikuwa na cheo hicho muda fulani kabla ya mwaka wa 1933 K.K
Melkizedeki na Ibrahimu walikutana kwanza baada ya Ibrahimu kushindwa kwa Kedorlaoma na washirika wake watatu. Melkizedeki iliwasilisha mkate na mvinyo kwa Ibrahimu na watu wake walokuwa wamechoka, kwa kuonyesha urafiki. Yeye alitawaza baraka kwa Ibrahimu kwa jina la El Elyon ("Mungu aliye juu zaidi") na kumsifu Mungu kwa kumpa Abraham ushindi katika vita (Mwanzo 14: 18-20).
Kulingana na utafiti nilioufanya neno Melkizedeki limeonekana katika Biblia mara kumi (Mwanzo 14:18, Zaburi 110:4, Kitabu cha Waebrania - 5:6, 5:10, 6:20, 7:1, 7:10, 7:11, 7:15, 7:17).
Mfalme huyu wa Salem anaibuka k**a mvuke na kuyeyuka k**a barafu, hivyo kuna mengi ambayo inakuwa vigumu kuyafahamu kwa hakika. Ili kuchanganua vema nimeligawa jibu katika sehemu kuu tatu: tunachokijua, kilicho na utata na mtazamo wangu.
Waebrania 7: 3 inasema kuwa ”hana baba, hana mama, hana wazazi, hana mwanzo wa siku zake, wala mwisho wa uhai wake, bali amefananishwa na Mwana wa Mungu; huyo adumu kuhani milele.”Swali ni iwapo mwandishi wa waebrania anamaanisha hii halisi au kitamathali.
(a) Tunachokijua kuhusu Melkizedeki
Mwanzo 14:18, bila taarifa ya kabla inamleta katika picha Melkizedeki. Hebu tuone tunapata nini katika andiko hili:
(Mwanzo 14:14 - 18) Abramu aliposikia ya kwamba nduguye ametekwa mateka, akawapa silaha vijana wake, waliozaliwa katika nyumba yake, watu mia tatu na kumi na wanane, akawafuata mpaka Dani. Akajipanga apigane nao usiku, yeye na watumwa wake, akawapiga, akawafukuza mpaka Hoba, ulioko upande wa kushoto wa Dameski. Naye akarudisha mali zote, akamrudisha na Lutu nduguye na mali zake, na wanawake pia, na watu. Abramu aliporudi kutoka kumpiga Kedorlaoma na wale wafalme waliokuwa pamoja naye, mfalme wa Sodoma akatoka amlaki katika bonde la Shawe, nalo ni Bonde la Mfalme. Na Melkizedeki mfalme wa Salemu akaleta mkate na divai, naye alikuwa kuhani wa Mungu Aliye juu sana.
Tunaona sifa mbili za Melkizedeki, kwanza mfalme na pili ni kuhani wa Mungu aliye juu. Salem ndiyo eneo ambalo mfalme huyu alitawala kulingana na mstari huu. Salem ina maana ya amani. Kwa hiyo Melkizedeki alikuwa mtawala wa sehemu yenye jina lenye tafsiri ya amani. Akiwa k**a kuhani, anambariki Ibrahimu na anapokea zaka za Ibrahimu (mst 19-20). Je sehemu hii yenye jina la Salem ni wapi?
Jina la Melkizedeki tunalikuta katika Zaburi 110:4. Lakini, kabla hatujaiangalia Zaburi hii ni vyema machache yakasemwa juu yake. Mwandishi wa zaburi hii ni Daudi na anaiandika k**a "Neno la Bwana kwa Bwana wangu". Bwana wa kwanza wa Daudi anamwambia Bwana wa pili, katika mistari saba ya zaburi hii. Na sehemu ya maneno ya Bwana kwenda kwa Bwana ni yale ya mstari wa nne ambayo ndiyo tutayaangalia kwa sasa:
Bwana ameapa, Wala hataghairi, Ndiwe kuhani hata milele, Kwa mfano wa Melkizedeki (Zaburi 110:4)
Kwa hiyo Bwana anaambiwa na Bwana kuwa yeye ni kuhani (sio atakuwa kuhani), mfano wa Melkizedeki. Neno mfano wa ni dibrâh ambalo lina maana ya "utaratibu wa kufuata" au "namna ya". Kwa hiyo Bwana ni kuhani kwa mpangilio au utaratibu uleule wa Melkizedeki, mfalme wa Salem. Ingawa hakuna mengi sana tuyapatayo hapa kuhusu Melkizedeki, ila machache tunayapata.
Moja ni kuwa Melkizedeki sio mfano au roho, ila ni mtu halisi. Hii inatufanya tujue kuwa Mwanzo 14:18 inaongelea historia na si mfano kutoka hewani. Lakini pia ukuhani wake ni halisi na sio aina fulani ya mfano usio halisi (abstract title).
Hizi ndizo sehemu mbili pekee ambazo tunaziona katika Agano la kale. Sasa na tuangalie kitabu pekee cha agano jipya kinachotuambia habari za Melkizedeki. Sehemu ya kwanza jina Melkizedeki liaonekana katika agano jipya ni Ebr 5:6 amabapo ni nukuu ya Zab 110:4 ikitupa majibu ya Bwana anayeambiwa na Bwana kuwa ni Yesu Kristo. Hicho ndicho tunachokipata katika mstari huu. Mstari wa 10 sura hii hii unatupa picha ya Melkizedeki kuwa hakuwa kuhani wa kawaida, bali kuhani mkuu. Sura 6:20 inarudia kusisitiza kile sura ya 5:6 kinasema, kuwa, Yesu ni kuhani mkuu mfano wa Melkizedeki.
Sura ya saba inatupa historia ya Melkizedeki kwa kina kidogo kuliko Zaburi 110 na Waebrania 5 na 6. Haya ni mambo tunayoyapata sura ya 7:1-17:
Melkizedeki ni halisi k**a alivyokuwa Ibrahimu
Maana ya Jina Melkizedeki ni mfalme wa haki na Salem maana yake ni amani Alikuwa kuhani aliyepokea zaka, ukuhani wake ni tofauti na ule wa Walawi
Kwa hiyo tunajua bila shaka kuwa Melkizedeki alikuwa ni mtu halisi na sio kisasili, na alikuwa kuhani mkuu. Melkizedeki ni jina lenye maana ya Mfalme wa haki, tena Mfalme wa salem ina maana ya Mfalme wa amani.
Ibrahimu alilipa fungu la kumi kwa Melkizedeki, Mwanzo 14:18–20.
Watu wa Melkizedeki walitenda haki, na wakaipata mbingu, Mwanzo 14:25–40.
Kristo alikuwa kuhani mkuu kwa mfano wa Melkizedeki, Waebrania 5:6.
Melkizedeki alikuwa Mfalme wa Salemu, kuhani wa Mungu Aliye Juu Sana, Waebrania 7:1–3.
Baada ya kuyaona yale yaliyo bayana na tuhamie sehemu ngumu yenye mawazo mgawanyiko juu ya utambulisho na asili ya Melkizedeki.
(a) Utata wa Utambulisho wa Melkizedeki na Mtazamo wangu
Kwa sababu Katika kitabu cha Mwanzo hatuna maelezo ya kutosha kumhusu huyu mtu, tutategemea sana Waraka wa Waebrania kujua juu ya utambulisho wake. Kumbuka kuwa mwandishi wa kitabu hiki ni Myahudi mzuri ambaye alikuwa na nafasi ya kusoma maandiko ya kihistoria ya Wayahudi ambayo leo hatuna baada ya hekalu kuchomwa moto. Hivyo basi lazima katika kusoma kwetu tusijifanye kujua kuliko mwandishi bali tujaribu kwa kadri ya uwezo wetu kuelewa alichomaanisha mwandishi.
(i) Nini Mwanzo wa Melkizedeki?
Kuna mawazo ya aina mbili hapa. La kwanza ni kuwa Melkizedeki alikuwa mwanadamu na mfalme wa Salem. Wengine (nikiwemo mimi) huamini kuwa maelezo ya Biblia kuhusu Melkizedeki yanabeba vitu ambavyo mwanadamu hawezi kuwa navyo. Mathalani Ebr 7:3 inatuambia kuwa yeye hana baba wala mama naye ni kuhani milele. Wandugu wanaotafsiri kuwa ni mwanadamu hudai kuwa andiko hili lina maana ya kuwa kumbukumbu zake kuhusu uzao na wazazi wake hazipo na kwamba umilele wa ukuhani wake ni kuweka mkazo na si vinginevyo.
Binafsi naona msimamo huu una mapungufu mengi sana. Kwanza Biblia iko wazi kuwa hana wazazi (na sio hana kumbukumbu ya wazazi) na kuonesha hilo imeweka wazi kuwa hana baba wala mama. Lakini kuonesha sio mwanadamu maandiko yameweka wazi kuwa " hana mwanzo wa siku zake, wala mwisho wa uhai wake" Kwa maana nyingine ni kuwa amekuwapo siku zote na uhai wake upo ndani yake Mwenyewe.
(ii) Melkizedeki ni Nani?
Baada ya kuona maandiko yanasema nini juu ya Melkizedeki ni wakati wa kuvumbua utambulisho wake. Kwa kuwa Mtu huyu hana mwazo wa siku wala mwisho wake (wa milele), k**a ulivyo ukuhani wake, basi yeye ni Mungu. Ni Mungu peke yake ndio hana mwanzo wala mwisho. Pia ni Mungu pekee uhai wake uko ndani yake, na hivyo kwa kuwa hana mwanzo wala mwisho vivyo hivyo na uhai wake!
Yohana 1 inatuelezea habari za Neno nayo inasema "Ndani yake ndimo ulimokuwa uzima" (mst 4) na Yoh 1:1 inaweka wazi kuwa kabla ya Mwanzo neno alikuwepo. Kwa hiyo kwa kwa uelewa wangu wa Biblia Takatifu ni kuwa Melkizedeki ni Mwana wa Mungu kabla hajauvaa mwili na kuitwa Yesu. Hii sio mara ya kwanza kwa Kristo, Masihi (Bwana wa pili katika Zab 110), kuwatokea wanadamu katika mwili. Alimtokea Ibrahimu akiwa na malaika wawili (Mwanzo 18)
(iii) Vipi wanaoamini Melkizedeki ni mwanadamu?
K**a ni swali la kuhusu tafsiri yao, ninaamini wanakosea kutafsiri maandiko. Lakini k**a ni swali la k**a wanakwenda mbinguni au motoni jibu ni kuwa haihusiani na safari hii. Kuna watu hawajui hata habari za Melkizedeki a tutakutana nao mbinguni na wengine wanajua kwa usahihi lakini, kwa huzuni, watakwenda Jehanamu. Hii ni kwa sababu njia ya kwenda mbinguni si kujua juu ya Melkizedeki au mtu mwingine yeyote bali ni kutubu dhambi zako mbele za Mungu na kumwamini Yesu Kristo na kazi aliyofanya pale msalabani kulipa deni ya dhambi yako. Hii ndio tofauti ya waendao mbinguni na Jehanamu: Yesu Kristo!
Kwa hiyo, k**a una elimu sahihi juu ya tafsiri ya biblia, jua haitakusaidia k**a dhambi zako hazijasamehewa bado. Utubu sasa na kumwamini Yesu k**a Bwana na Mwokozi wa maisha yako. Nani ajua kuwa maneno haya yanaweza kuwa ya mwisho kuyasoma kabla hujapita mlango wa mauti kukutana na Mungu wako?
"Kwa sababu, ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua katika wafu, utaokoka." (Warumi 10:9)
References:
i. Alfa and omega Org
ii. Christ for All Nations
iii. NKJV Bible
iv. Got Questions Ministries
v. Church of God Inc.
Shalom
04/04/2019
25/02/2019