Vifrem Entrepreneurship Training Agent

Vifrem Entrepreneurship Training Agent

Share

Non Government Organization conerning with providing education about health, enterpreneurship, psych

11/10/2021

MELKIZEDEKI NI NANI?

Kuhani Mkuu, Mfalme na kiongozi katika Agano la Kale aliyeishi baada ya gharika na katika wakati wa Ibrahimu. Aliitwa mfalme wa Salemu, mfalme wa amani, mfalme wa haki (ambayo kwa Kiebrania ndiyo maana ya neno Melkizedeki), na kuhani wa Mungu Aliye Juu Sana. Yeye ndiye kuhani wa kwanza anayetajwa katika Maandiko; alikuwa na cheo hicho muda fulani kabla ya mwaka wa 1933 K.K

Melkizedeki na Ibrahimu walikutana kwanza baada ya Ibrahimu kushindwa kwa Kedorlaoma na washirika wake watatu. Melkizedeki iliwasilisha mkate na mvinyo kwa Ibrahimu na watu wake walokuwa wamechoka, kwa kuonyesha urafiki. Yeye alitawaza baraka kwa Ibrahimu kwa jina la El Elyon ("Mungu aliye juu zaidi") na kumsifu Mungu kwa kumpa Abraham ushindi katika vita (Mwanzo 14: 18-20).

Kulingana na utafiti nilioufanya neno Melkizedeki limeonekana katika Biblia mara kumi (Mwanzo 14:18, Zaburi 110:4, Kitabu cha Waebrania - 5:6, 5:10, 6:20, 7:1, 7:10, 7:11, 7:15, 7:17).

Mfalme huyu wa Salem anaibuka k**a mvuke na kuyeyuka k**a barafu, hivyo kuna mengi ambayo inakuwa vigumu kuyafahamu kwa hakika. Ili kuchanganua vema nimeligawa jibu katika sehemu kuu tatu: tunachokijua, kilicho na utata na mtazamo wangu.

Waebrania 7: 3 inasema kuwa ”hana baba, hana mama, hana wazazi, hana mwanzo wa siku zake, wala mwisho wa uhai wake, bali amefananishwa na Mwana wa Mungu; huyo adumu kuhani milele.”Swali ni iwapo mwandishi wa waebrania anamaanisha hii halisi au kitamathali.

(a) Tunachokijua kuhusu Melkizedeki

Mwanzo 14:18, bila taarifa ya kabla inamleta katika picha Melkizedeki. Hebu tuone tunapata nini katika andiko hili:

(Mwanzo 14:14 - 18) Abramu aliposikia ya kwamba nduguye ametekwa mateka, akawapa silaha vijana wake, waliozaliwa katika nyumba yake, watu mia tatu na kumi na wanane, akawafuata mpaka Dani. Akajipanga apigane nao usiku, yeye na watumwa wake, akawapiga, akawafukuza mpaka Hoba, ulioko upande wa kushoto wa Dameski. Naye akarudisha mali zote, akamrudisha na Lutu nduguye na mali zake, na wanawake pia, na watu. Abramu aliporudi kutoka kumpiga Kedorlaoma na wale wafalme waliokuwa pamoja naye, mfalme wa Sodoma akatoka amlaki katika bonde la Shawe, nalo ni Bonde la Mfalme. Na Melkizedeki mfalme wa Salemu akaleta mkate na divai, naye alikuwa kuhani wa Mungu Aliye juu sana.

Tunaona sifa mbili za Melkizedeki, kwanza mfalme na pili ni kuhani wa Mungu aliye juu. Salem ndiyo eneo ambalo mfalme huyu alitawala kulingana na mstari huu. Salem ina maana ya amani. Kwa hiyo Melkizedeki alikuwa mtawala wa sehemu yenye jina lenye tafsiri ya amani. Akiwa k**a kuhani, anambariki Ibrahimu na anapokea zaka za Ibrahimu (mst 19-20). Je sehemu hii yenye jina la Salem ni wapi?

Jina la Melkizedeki tunalikuta katika Zaburi 110:4. Lakini, kabla hatujaiangalia Zaburi hii ni vyema machache yakasemwa juu yake. Mwandishi wa zaburi hii ni Daudi na anaiandika k**a "Neno la Bwana kwa Bwana wangu". Bwana wa kwanza wa Daudi anamwambia Bwana wa pili, katika mistari saba ya zaburi hii. Na sehemu ya maneno ya Bwana kwenda kwa Bwana ni yale ya mstari wa nne ambayo ndiyo tutayaangalia kwa sasa:

Bwana ameapa, Wala hataghairi, Ndiwe kuhani hata milele, Kwa mfano wa Melkizedeki (Zaburi 110:4)

Kwa hiyo Bwana anaambiwa na Bwana kuwa yeye ni kuhani (sio atakuwa kuhani), mfano wa Melkizedeki. Neno mfano wa ni dibrâh ambalo lina maana ya "utaratibu wa kufuata" au "namna ya". Kwa hiyo Bwana ni kuhani kwa mpangilio au utaratibu uleule wa Melkizedeki, mfalme wa Salem. Ingawa hakuna mengi sana tuyapatayo hapa kuhusu Melkizedeki, ila machache tunayapata.

Moja ni kuwa Melkizedeki sio mfano au roho, ila ni mtu halisi. Hii inatufanya tujue kuwa Mwanzo 14:18 inaongelea historia na si mfano kutoka hewani. Lakini pia ukuhani wake ni halisi na sio aina fulani ya mfano usio halisi (abstract title).

Hizi ndizo sehemu mbili pekee ambazo tunaziona katika Agano la kale. Sasa na tuangalie kitabu pekee cha agano jipya kinachotuambia habari za Melkizedeki. Sehemu ya kwanza jina Melkizedeki liaonekana katika agano jipya ni Ebr 5:6 amabapo ni nukuu ya Zab 110:4 ikitupa majibu ya Bwana anayeambiwa na Bwana kuwa ni Yesu Kristo. Hicho ndicho tunachokipata katika mstari huu. Mstari wa 10 sura hii hii unatupa picha ya Melkizedeki kuwa hakuwa kuhani wa kawaida, bali kuhani mkuu. Sura 6:20 inarudia kusisitiza kile sura ya 5:6 kinasema, kuwa, Yesu ni kuhani mkuu mfano wa Melkizedeki.

Sura ya saba inatupa historia ya Melkizedeki kwa kina kidogo kuliko Zaburi 110 na Waebrania 5 na 6. Haya ni mambo tunayoyapata sura ya 7:1-17:

Melkizedeki ni halisi k**a alivyokuwa Ibrahimu
Maana ya Jina Melkizedeki ni mfalme wa haki na Salem maana yake ni amani Alikuwa kuhani aliyepokea zaka, ukuhani wake ni tofauti na ule wa Walawi

Kwa hiyo tunajua bila shaka kuwa Melkizedeki alikuwa ni mtu halisi na sio kisasili, na alikuwa kuhani mkuu. Melkizedeki ni jina lenye maana ya Mfalme wa haki, tena Mfalme wa salem ina maana ya Mfalme wa amani.

Ibrahimu alilipa fungu la kumi kwa Melkizedeki, Mwanzo 14:18–20.

Watu wa Melkizedeki walitenda haki, na wakaipata mbingu, Mwanzo 14:25–40.

Kristo alikuwa kuhani mkuu kwa mfano wa Melkizedeki, Waebrania 5:6.

Melkizedeki alikuwa Mfalme wa Salemu, kuhani wa Mungu Aliye Juu Sana, Waebrania 7:1–3.

Baada ya kuyaona yale yaliyo bayana na tuhamie sehemu ngumu yenye mawazo mgawanyiko juu ya utambulisho na asili ya Melkizedeki.

(a) Utata wa Utambulisho wa Melkizedeki na Mtazamo wangu

Kwa sababu Katika kitabu cha Mwanzo hatuna maelezo ya kutosha kumhusu huyu mtu, tutategemea sana Waraka wa Waebrania kujua juu ya utambulisho wake. Kumbuka kuwa mwandishi wa kitabu hiki ni Myahudi mzuri ambaye alikuwa na nafasi ya kusoma maandiko ya kihistoria ya Wayahudi ambayo leo hatuna baada ya hekalu kuchomwa moto. Hivyo basi lazima katika kusoma kwetu tusijifanye kujua kuliko mwandishi bali tujaribu kwa kadri ya uwezo wetu kuelewa alichomaanisha mwandishi.

(i) Nini Mwanzo wa Melkizedeki?

Kuna mawazo ya aina mbili hapa. La kwanza ni kuwa Melkizedeki alikuwa mwanadamu na mfalme wa Salem. Wengine (nikiwemo mimi) huamini kuwa maelezo ya Biblia kuhusu Melkizedeki yanabeba vitu ambavyo mwanadamu hawezi kuwa navyo. Mathalani Ebr 7:3 inatuambia kuwa yeye hana baba wala mama naye ni kuhani milele. Wandugu wanaotafsiri kuwa ni mwanadamu hudai kuwa andiko hili lina maana ya kuwa kumbukumbu zake kuhusu uzao na wazazi wake hazipo na kwamba umilele wa ukuhani wake ni kuweka mkazo na si vinginevyo.

Binafsi naona msimamo huu una mapungufu mengi sana. Kwanza Biblia iko wazi kuwa hana wazazi (na sio hana kumbukumbu ya wazazi) na kuonesha hilo imeweka wazi kuwa hana baba wala mama. Lakini kuonesha sio mwanadamu maandiko yameweka wazi kuwa " hana mwanzo wa siku zake, wala mwisho wa uhai wake" Kwa maana nyingine ni kuwa amekuwapo siku zote na uhai wake upo ndani yake Mwenyewe.

(ii) Melkizedeki ni Nani?

Baada ya kuona maandiko yanasema nini juu ya Melkizedeki ni wakati wa kuvumbua utambulisho wake. Kwa kuwa Mtu huyu hana mwazo wa siku wala mwisho wake (wa milele), k**a ulivyo ukuhani wake, basi yeye ni Mungu. Ni Mungu peke yake ndio hana mwanzo wala mwisho. Pia ni Mungu pekee uhai wake uko ndani yake, na hivyo kwa kuwa hana mwanzo wala mwisho vivyo hivyo na uhai wake!

Yohana 1 inatuelezea habari za Neno nayo inasema "Ndani yake ndimo ulimokuwa uzima" (mst 4) na Yoh 1:1 inaweka wazi kuwa kabla ya Mwanzo neno alikuwepo. Kwa hiyo kwa kwa uelewa wangu wa Biblia Takatifu ni kuwa Melkizedeki ni Mwana wa Mungu kabla hajauvaa mwili na kuitwa Yesu. Hii sio mara ya kwanza kwa Kristo, Masihi (Bwana wa pili katika Zab 110), kuwatokea wanadamu katika mwili. Alimtokea Ibrahimu akiwa na malaika wawili (Mwanzo 18)

(iii) Vipi wanaoamini Melkizedeki ni mwanadamu?

K**a ni swali la kuhusu tafsiri yao, ninaamini wanakosea kutafsiri maandiko. Lakini k**a ni swali la k**a wanakwenda mbinguni au motoni jibu ni kuwa haihusiani na safari hii. Kuna watu hawajui hata habari za Melkizedeki a tutakutana nao mbinguni na wengine wanajua kwa usahihi lakini, kwa huzuni, watakwenda Jehanamu. Hii ni kwa sababu njia ya kwenda mbinguni si kujua juu ya Melkizedeki au mtu mwingine yeyote bali ni kutubu dhambi zako mbele za Mungu na kumwamini Yesu Kristo na kazi aliyofanya pale msalabani kulipa deni ya dhambi yako. Hii ndio tofauti ya waendao mbinguni na Jehanamu: Yesu Kristo!

Kwa hiyo, k**a una elimu sahihi juu ya tafsiri ya biblia, jua haitakusaidia k**a dhambi zako hazijasamehewa bado. Utubu sasa na kumwamini Yesu k**a Bwana na Mwokozi wa maisha yako. Nani ajua kuwa maneno haya yanaweza kuwa ya mwisho kuyasoma kabla hujapita mlango wa mauti kukutana na Mungu wako?

"Kwa sababu, ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua katika wafu, utaokoka." (Warumi 10:9)

References:
i. Alfa and omega Org
ii. Christ for All Nations
iii. NKJV Bible
iv. Got Questions Ministries
v. Church of God Inc.

Shalom

17/06/2019

MADA:NJIA NZURI ZA KUONDOA MAGADI (SALTS) SHAMBANI

Utangulizi
Katika mashamba mengi tatizo la udongo na ardhi kwa ujumla kujaa chumvi au magadi limekuwa tatizo kubwa kwa wakulima wengi kwani magadi au chumvi huleta madhara makubwa sana kwa mazao na hata mazao mengine hufa kabisa pale
yanapooteshwa kwenye udongo wenye magadi mfano wa mashamba yalioadhirika ni Ndungu irrigation scheme, kitivo irrigation scheme, Dakawa, Kiroka na Mkindo irrigation scheme (Morogoro), Kinyasugwe scheme (Dodoma) pia baadhi ya maeneo ya Lower Moshi, Mawala, Kikavu chini, na hivyo kufanya mashamba yalio na tatizo hilo yasitumike katika uzalishaji, makala hii itakusaidia kumuelekeza mkulima kujua namna ya kurudisha ardhi ya shamba lako katika hali nzuri na kuzuia uwezekano wa magadi kuongezeka katika shamba lako na hii itaongeza uzalishaji kwani utaweza kuotesha mazao mengi na ya aina mbalimbali k**a udongo wako utakuwa na hali nzuri ya kuupatia mmea wako maji na madini au (nutrients) za kuuwezesha kukua vizuri na kuzaa sana

AINA ZA MAGADI ZILIZOPO KWENYE UDONGO

Kuna aina nyingi za chumvichumvi zilizopo ardhini na huwa katika viwango tofauti kulingana eneo moja na lingine na tofauti hii husababishwa na asili ya udongo wa mahali husika chumvi hizi ni k**a Sodium ambayo hupatikana kwenye chumvi ya kawaida(NaCl), Potasium, Boron, Magnesium, Calcium, Phosphorous. Madini mengine ni muhimu katika ukuaji wa mmea lakini kwa kiwango kinachotakiwa na huwa ni sumu endapo yatazidi kiwango chake

NAMNA AMBAVYO MAGADI HUDHOOFISHA MIMEA

Madhara yatokanayo na magadi ni makubwa sana na huleta hasara kwa wakulima wengi sana, kitaalamu magadi huzuia mizizi ya mimea kufyonza maji kwenye udongo na kuufanya mmea kushindwa kukua kwani maji ni muhimu katika mfumo wa mimea kujitengenezea chakula chake hata k**a utamwagilia maji ya kutosha katika shamba lenye magadi bado mimea haitaweza kupata maji hayo (salts induce water stress to crops through matrix forces build up between the soil particles and the salts ion and hinder plant water uptake via capillarity and osmosis).

Pia magadi huharibu mfumo wa udongo(soil structure) na kuufanya udongo kuwa mgumu na kuzuia mizizi ya mmea kupenya vizuri kwenye ardhi na hivyo kupunguza udhabiti wa mimea iwapo shambani na kusababisha kuanguka angauka kwa mazao yanapofikia wakati wa kubeba matunda au maua kwani hukosa nguvu za kujishikilia kwenye ardhi na hali hii husababishwa sana uwepo na sodium nyingi shambani na mkulima hupata hasara kubwa sana.

VYANZO VYA MAGADI KWENYE UDONGO

1.Asili ya udongo wenyewe

Baadhi ya maeneo yana udongo wenye asili ya chumvi kwa Tanzania maeneo hayo yanapatikana kwa wingi Dodoma na Singida na hasa wakati wa kiangazi baada ya mvua kukatika unaweza ukaona kabsa mabonge ya chumvi ardhini

2. Maji yanatumika kwa umwagiliaji

Kuna baadhi ya maeneo maji yake huwa na chumvi kiasi kwenye mito na hapa chemichemi na wakulima hutumia maji kutoka kwenye vyanzo hivyo vyenye maji ya chumvi katika kumwagilia mashammba yao, hii huongeza chumvi kidogo kidogo kwenye ardhi na k**a mwendelezo wa kutumia maji hayo utafanyika kwa miaka mitano basi shamba hilo litakuwa limejaa chumvi na halitafaa tena kwa kilimo endapo njia na mbinu stahiki hazitachukuliwa. Mfano skimu ya Mazinde pamoja na Mombo.

3. Utumiaji wa mbolea za viwandani bila maelekezo ya kitaalamu

Tujue ya kuwa sio kila mbolea ya kiwandani inafaa kwenye kila aina ya udongo, pili tunapokuwa tunaweka mbolea shambani lazima tuwatumie wataalamu ili watupe vipimo sahihi vya uwekaji wa mbolea hizi ili ziwe kwa kiwango kinachotakiwa pasipo kuzidisha wala kupunguza , kila shamba lina rutuba tofauti na lingine kwa hiyo ata uwekaji wa mbolea utatofautiana.
Pia kila zao lila vipimo vyake vya kiasi cha mbolea kinachotakiwa, kumbuka ni muhimu kufuata ushauri wa wataalamu kabla ya kuweka mbolea shambani ili kuondokana na matatizo na uweze kuzalisha mazao yenye tija ndio maana mfano, wataalamu kutoka TARI Mlingano wanashauri upime udongo kwanza kabla hujaanza kulima

4. Mfumo mbaya wa utoaji maji shambani(poor drainage system)

Tatizo hili ni kubwa sana hasa pale wakulima wengi wanapoamini kuwa katika kumwagilia shamba lazima aone maji yametuama ndio aridhike kuwa amemwagilia, hili ni kosa kubwa kwani tunatakiwa tujue kuwa mimea hufyonza maji yaliyo ardhini tuu(plants absorb water, and they don't drink water ......... Myth), maji yaliyotuama shambani hupandisha chumvi iliyopo chini kuja juu na baada ya ardhi kukauka chumvi ile hubakia juu ya ardhi na kuathiri mimea

NJIA ZA KUONDOA MAGADI SHAMBANI

Hili ndilo lengo kuu la makala hii ili kumsaidia mkulima kuondokana na tatizo hili, nitaeleza njia za kitaalumu na za gharama nafuu za kuondoa na kupunguza magadi shambani.

1. Kuzamisha chumvi (Leaching of salts)

Wakati wa kumwagilia shamba unashauriwa umwagilie maji mengi kiasi kuliko yale yanayotosheleza mmea wako ili maji hayo ya ziada yasaidia katika kuzamisha chumvi iliyoko juu wa udongo iende chini zaidi ambako mizizi ya mimea haifiki, njia hii lazima utumie wataalamu wa umwagiliaji (irrigation engineers) ambao watasaidia kitaalamu kuendena na udongo wako na kujulisha ni kiasi gani cha maji inatakiwa umwagilie katika shamba lako ili kuondoa chumvi na kusaidia mimea yako kukua (irrigation and leaching requirements)

2. Uwekaji wa Gypsum (Calcium Sulfate)

Gypsum hufanya kitu kinachoitwa neutralization ambapo hubadilisha chumvi iliyopo ardhini isilete madhara kwa mimea na katika maduka mengi ya pembejeo zinauzwa hizi gypsum kwa ajili ya mashamba ili kudhibiti chumvi na magadi lakini njia hii ni ya gharama kidogo

3. Utumiaji wa Samadi

Mbolea za wanyama na mimea husaidia sana kwenye kuongeza rutuba kwenye ardhi pia katika kuhakikisha na kupungiuza magadi kwenye udongo na njia hii matokeo yake ni polepole lakini ina uhakika na pia samadi ina faida nyingine nyingi katika kuimarisha udongo na kuongeza upatikanaji wa madini kwa mimea

4. Njia ya mafuriko (flooding)

Njia hii hufanywa katika maeneo yenye maji mengi na hasa kipindi cha mvua , shamba lenye magadi hutifuliwa na kufurishwa au kumwagiliwa mpka maji yanatuama (wakati hamna mazao shambani) na baada ya hapo maji hutolewa kwa mifereji maalumu na maji hayo huchukua magadi katika shamba husika

NB. njia hii usiifanye kwenye mashamba yaliosongamana ili maji yaliyo na magadi yasiende kwenye shamba la jirani yako na kumpa hasara

5. Utumiaji wa njia za kisasa za kufanya umwagiliaji k**a drip irrigation, sprinkler system hupunguza uwepo wa magadi kwenye udongo.
Lakini kwa maeneo ambayo yana magadi sana unashauriwa kupanda mazao yanayoshahimili ardhi yenye chumvi

mazao yanayoshahimili chumvi zabibu, mbaazi, Nanasi, Miembe hasa mazao ya miti ndio hushauriwa sana katika ardhi yenye magadi

mazao yasiostahimili udongo wenye magadi

Mahindi, Tikiti maji, Nyanya, Mbogamboga, na mengne mengi.

Avoid Using the Word "Very" 04/04/2019

Great Lesson For All Learner !!!

07/03/2019

JONAS SAVIMBI ALIKUWA MUASI AU MPIGANIA UKOMBOZI?
__________________________
Francis Daudi

Tulipokuwa tunakuwa, mtoto mtundu na mkorofi basi aliitwa SAVIMBI, kwa wakati huo sikujua Savimbi maana yake nini. Mara nyingine nilihisi ni jina maalumu kwa watu wakorofi. Historia ilifungua macho yangu!

Baada ya nchi nyingi za Afrika kupata uhuru bado zilitumbukia katika mapinduzi na kila aina ya ghasia. Hii ilitokana na sera za mataifa makubwa kutaka kuendelea kuyatawala mataifa hayo huru, Ukabila, Vita baridi na uchu mkubwa wa madaraka waliokuwa nao wapigania ukombozi. Historia ya Afrika na hasa kusini mwa jangwa la Sahara kamwe haitamsahau Jonas Savimbi.

Jonas Savimbi ni nani?
Huyu alikuwa kiongozi mkuu wa chama ambacho kilikuwa kikundi cha wapiganaji wa msituni wa United Front for the Total Independence of Angola (UNITA). Aliongoza vita vya Msituni vya muda mrefu kuliko vyote kusini mwa Afrika. Jonas Savimbi akiongoza vuguvugu la UNITA lilipelekea vifo vya Zaidi ya watu milioni moja na maelfu ya wakimbizi nchini Angola. Kipindi chote cha takribani miaka 27 alikuwa akisaidiwa na Serikali ya Marekani na Serikali ya kidhalimu ya mabeberu wa Afrika kusini. Hivyo kwa mataifa ya Magharibi aliitwa Mpigania ukombozi wa Angola Mpya!

Savimbi alizaliwa Agosti 3, 1934 na, kufariki tarehe 22 Februari 2002 kutoka na shambulio la kushtukiza lililofanywa na jeshi la Angola! Alikuwa ni wa kabila kubwa Zaidi Angola la Ovimbundu na alikulia Jimbo la kusini lililoitwa Moxico. Savimbi alikuwa ana uwezo wa kuongea lugha sita kwa ufasaha kabisa zikiwemo Kiingereza, Kifaransa na Kireno. Baada ya Masomo yake huko Ulaya kati ya miaka ya sitini alirudi na kujiunga na MPLA Youth kupigana vita vya msituni dhidi ya Wareno!

Kutokana na Mgogoro alijiunga na kundi la National Liberation Front of Angola (FNLA) mwaka 1964. Savimbi alikuwa mwenye uelewa mkubwa wa mbinu za kupigana vita. Mara kadhaa alikwaruzana na viongozi wa FNLA na hatimaye akaamua kuanzisha kundi lake lililoitwa UNITA mara baada ya kupata mafunzo maalumu nchini China.

Kulingana na taarifa za Siri, Savimbi aliamua kufungua mazungumzo na wakoloni wa Kireno ili waweze kumwachia nchi. Alikubali kupigana dhidi ya MPLA na FNLA katika operesheni maalumu ya kijeshi “Operation Timber”(Maelezo yake yapo ndani ya kitabu cha Prof. Gerald Bender ). Kufikia mwaka 1974 Wareno walishindwa kuhimili vita vikali vilivyoongozwa na MPLA hivyo waliiacha nchi ya Angola bila utaratibu wa kueleweka.

Vikundi vyote vilikubaliana kuingia katika uchaguzi mkuu wa Novemba, 1975 ili Angola iongozwe kidemokrasia. Savimbi hakukubali hilo, alitaka waongoze nchi kwa zamu! Haikuwezekana, akarudi msituni na kuongoza vita vikali kwa Zaidi ya miongo miwili. Savimbi alipata usaidizi wa karibu wa Holden Roberto wa shirika la CIA la Marekani. Serikali ya Ubaguzi wa rangi iliingiza vifaa vya kivita na fedha kwa ajili ya kumsaidia Savimbi na UNITA.

Angola iligeuka uwanja wa vita baridi kati ya Marekani na Umoja wa Nchi ya Kisovieti chini ya Urusi. MPLA ambacho ni Movimento Popular de Libertação de Angola kiliomba usaidizi wa Urusi ili kupambana na Savimbi. Haikusaidia kitu, Savimbi alitumia fedha na vifaa vya mabepari upande mmoja na kwingine akitumia mbinu za kisoshalisti alizopata Uchina!
UNITA ilishambulia maeneo ya migodi, vituo vya afya na vyakula vya misaada. Kati ya mwaka 1980 mpaka 1988 Serikali ya Angola ilitumia dola bilioni 30 za kimarekani katika vita dhidi ya UNITA( Hii ni mara sita zaidi ya Pato la Taifa la Angola kwa wakati huo)

Pamoja na vita hivyo, Angola ilifanya uchaguzi wa vyama vingi mwaka 1992. Kabla ya uchaguzi huo, mmoja kati ya waanzilishi wa UNITA Antonio da Costa Fernandes alijitoa! Alilaumu kuwa Savimbi amekuwa akiendesha vitendo vya udhalilishaji wa kijinsia na mauaji mabaya! Wakati malengo ya UNITA yalikuwa ni kuleta ukombozi wa pili kwa nchi ya Angola. Athari za vita zilikuwa kubwa mno, kwa miaka 10 ya mwanzo, watoto 330,000 walifariki. Savimbi aliongoza ukatwaji wa viungo k**a mikono na miguu kwa watu waliosaliti au kuunga mkono serikali ya Angola.

Serikali mpya ya Marekani (Chini ya Bill Clinton) iliitambua MPLA k**a chama tawala cha Angola hivyo waliita UNITA katika meza ya makubaliano. Savimbi hakukubaliana na masharti ya kugawana madaraka! Akarudi tena msituni.

Baraza la usalama la umoja wa Mataifa likamtambua raisi Jose Eduardo dos Santos mwaka 1993 na Marekani ikafunga misaada kwa UNITA. Savimbi alikuwa ameshikilia migodi ya Almasi hivyo aliendelea na mapambano! Mwaka 1998 Umoja wa Mataifa ulipiga marufuku biashara ya Almasi kati ya mataifa wanachama na UNITA.

UNITA ilikosa nguvu zaidi, Hivyo wapiganaji wake wakawa wanavamia vijiji na miji kupora vitu! Walipelekea njaa kwani walishambulia maghala ya chakula. Angola ambayo ilikuwa mzalishaji wa pili wa mafuta ghafi katika bara ya Afika ikawa nchi isiyo na usalama k**a Syria na Iraq ya sasa!

Kulifanyika majaribio karibu 15 kumuua na yalishindikana, Lakini tarehe 22 Februari 2002 alishambuliwa na Jeshi la Angola na Kufariki dunia. Nafasi yake ilichukuliwa na Antonio Dembo! Jonas Savimbi aliacha wake angalau 25 na mpaka sasa idadi ya watoto wake haifahamiki.

Hakuna aliyeamini Savimbi amefariki mpaka mwili wake ulipooneshwa kwenye televisheni ya Taifa la Angola. UNITA ilikubali kuwa chama na kuangushwa vibaya na MPLA katika uchaguzi wa mwak 2008. Wakati Fulani vijana wa MPLA ambacho ni chama Tawala walibomoa kaburi la Jonas Savimbi. Wote waliohusika walishtakiwa!

Bado swali linabaki, Je Savimbi anapaswa kuitwa Muasi au mpigania ukombozi?

Francis Daudi

25/02/2019

Shilingi Kushuka Thamani na Hali Mbaya ya Uchumi Wetu: Sababu ni Nini na Nini Kifanyike?

Thamani ya sarafu ya Tanzania imezidi kuporomoka kwa kasi dhidi ya Dola ya Marekani katika wiki za hivi karibuni. Mwishoni mwa wiki iliyopita dola moja imeuzwa mpaka TZS 2415, mporomoko wa karibia 15% kulinganisha na thamani ya Dola katika mwezi wa Januari Mwaka 2018. Kwa maoni yangu, Watanzania wanapaswa kujua kuwa Haya ni matokeo ya Mambo Matatu Makubwa:

Mosi: Ni maamuzi ya hovyo juu ya Zao la Korosho, ambalo ndio zao kiongozi katika kuleta fedha za Kigeni nchini. Kutokana na maamuzi mabaya ya Serikali ya kutaka sifa za muda mfupi za kisiasa, mwaka 2018 Tanzania haikuuza Korosho nje ya nchi kutoka msimu wa 2018/19. Pia kitendo cha Serikali kuingia mkataba na kampuni ya kitapeli kutoka Kenya ili kununua Korosho kumesababisha Tanzania kuchelewa kuwahi soko la korosho kabla ya msimu wa mavuno wa nchi za Nigeria, Guinea Bissau, Benin, Ivory Coast na Indonesia kuingiza Korosho zao kwenye soko la dunia. Hasara ya Korosho itafikia TZS 1 trilioni na zaidi.

Pili: Ni ubinywaji wa Demokrasia nchini, msingi wake Mkuu ukiwa ni kuporwa kwa ushindi wa Chama cha CUF katika ngazi ya Uwakilishi na Urais kwenye Uchaguzi Mkuu wa Zanzibar wa mwaka 2015. Kisha vitendo vya kuzuia Bunge Live, kuzuia mikutano ya hadhara ya vyama vya siasa vya Upinzani (ya CCM ikiruhusiwa), na kuwabambikia kesi mbalimbali wanasiasa wa upinzani, kupigwa risasi kwa Mbunge Tundu Lissu akiwa kwenye eneo la Bunge, na Kutungwa kwa sheria mpya ya vyama vya siasa inayoua kabisa siasa za vyama vingi nchi.

Mfululizo wa matukio hayo yanayoua Demokrasia yetu nchini umepelekea Nchi Wahisani (wafadhili) kutoleta fedha za kigeni nchini. Pia uminywaji huu wa Demokrasia pamoja na matukio mengine ya ukandamizwaji wa haki za binadam vimesababisha mahusiano ya Tanzania na nchi zinazofadhili na kuchangia Bajeti na hata mashirika ya kimataifa kudorora. Baadhi ya mashirika na nchi zikifuta kabisa misaada na huku wengine wakizuia au kuchelewesha kutoa fedha za kusaidia bajeti yetu ya Maendeleo.

Tatu: Ni kushuka kwa Fedha za Kigeni zitokanazo na mitaji ya uwekezaji nchini. Tangu Serikali ya awamu ya tano iingie madarakani mitaji kutoka nje imeshuka kutoka 5% ya Pato la Taifa kwa mwaka 2015 mpaka kufikia 2% ya Pato la Taifa kwa mwaka 2018. Msingi wa kushuka huko kwa uwekezaji wa mitaji ni kutokuwepo kwa hali ya uhakika kwenye usimamizi na uendeshaji wa Sera za Uwekezaji nchini.

Athari Gani Zitarajiwe Kutokana na ya Hali Hii?

1. Uwezo wetu wa kulipa madeni ya Mikopo na ya Wakandarasi wa Miradi mikubwa utashuka mno. Inatarajiwa kuwa Serikali itashindwa kulipa wakandarasi wa miradi yake mikubwa au k**a ikiwalipa basi ita’default’ malipo ya madeni ya Taifa yaliyowiva au kuchelewesha mishahara ya watumishi wa umma. Athari za jambo hili zimeshaanza kuonekana, kwa nusu mwaka wa Fedha wa 2018/19 kiwango cha fedha za umma zinazotumika kuhudumia deni la Taifa kimeongezeka sana, hiyo ni kwa sababu madeni kadhaa yamewiva na pia Serikali ya Rais Magufuli inachukua mikopo mingi yenye riba ghali na ya muda mfupi kutoka kwenye Benki za Biashara. Kwa miaka miwili sasa mikopo ya kuendesha Bajeti inatoka Benki k**a HSBC, CreditSuisse na mabenki mengine ya Nje yenye riba kubwa na kutukopesha kwa fedha za kigeni.

2. Athari ya pili kubwa itakuwa ni kupanda kwa gharama za kuhudumia deni la Taifa. Nionavyo, Kwa kuwa Serikali hii ni kiburi na isiyo sikivu, itaamua kuendelea kukopa kutoka benki za nje kwa fedha za kigeni ili kuficha aibu kwa Wananchi na hivyo kuingiza nchi kwenye madhara makubwa zaidi. Gharama za kuhudumia deni (debt services) litakuwa kubwa kiasi cha Serikali kushindwa kutoa fedha kwa matumizi mengine k**a vile Elimu na Afya. Kwa sasa, katika Kila TZS 100 inayokusanywa nchini, zaidi ya shilingi 80 inakwenda kwenye kuhudumia deni la Taifa na mishahara ya watumishi wa umma. Kwa kushuka huku kwa thamani ya Shilingi pamoja na ukopaji wetu wa Kiholela kwenye Benki za Kibiashara, ni dhahiri kuwa fedha zote tunazozikusanya tutaishia kulipa madeni na mishahara tu.

3. Gharama za Uzalishaji Viwandani itakuwa kubwa zaidi, hasa kwa upande wa Sekta binafsi. Viwanda vyetu hutegemea sana ununuzi wa mitambo, vipuri, na malighafi za kuzalishia bidhaa za viwandani kutoka nje ya nchi, kwa kushuka thamani ya shilingi yetu dhidi ya Dola ya Marekani, ununuzi wa vyote hivyo utakuwa ghali zaidi kwa sababu malighafi nyingi zinatoka nje ya nchi na hunuliwa kwa dola ya Marekani. Matokeo ya jambo hilo itakuwa ni kuongezeka bei ya bidhaa za Viwandani na hata kushindwa kununulika na wananchi, na kushindwa kushindana kwenye soko na bidhaa za Nje ya nchi ambazo gharama zake zitakuwa ndogo zaidi. Wananchi watatumia shilingi nyingi zaidi kununua bidhaa ile ile waliyokuwa wakinunua kwa bei ndogo wakati sarafu yetu ilipokuwa na nguvu sokoni. Tayari Wafanyabiashara Katika sekta binafsi wameanza kuhangaika kupata fedha za kigeni maana hazipatikani sokoni. Sekta binafsi itajikuta inafunga Biashara na kusababisha watu wengi kukosa Ajira.

Nini Kifanyike Kuokoa Hali Mbaya Iliyoko?

1. Serikali Irudishe hali ya soko la Korosho ilivyokuwa kabla ya mwaka 2018/19, kwanza kwa kufanya marekebisho ya sheria na kurudisha Fedha zote za Export Levy kwa Wakulima wa Korosho ili zitumike kuwapa bure mbolea, salfa na madawa mengine ili kuwapa motisha na hali ya kukata tamaa iliyotokana na msimu huu wa manunuzi. Serikali iwalipe kwa haraka wakulima wote waliopeleka korosho kwenye vyama vya msingi, izichukue korosho inazozirudisha sasa kwa wakulima na iwalipe, na kisha itafute masoko ya korosho hizo hata kwa kuuza kwa Serikali kwa Serikali.

2. Serikali ikae chini kufanya mazungumzo ya kutafuta muafaka juu ya Ushindi wa Chama cha CUF ulioporwa kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 wa Zanzibar. Muhimu zaidi Rais k**a Mkuu wa Nchi na mkuu wa chama kilichopora ushindi wa CUF, aombe kikao na Katibu Mkuu wa CUF na aliyekuwa Mshindi wa Urais kwenye Uchaguzi huo wa mwaka 2015 wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad ili kujenga msingi wa kupata suluhisho la haki ya Wazanzibari kupata Serikali waliyoichagua Oktoba 25, 2015.

3. Serikali ikubali kufanyika kwa uchunguzi huru wa shambulio na jaribio la kuuawa kwa mnadhimu mkuu wa Kambi ya Upinzani Bungeni, mbunge Tundu Lissu ili kupata ukweli juu ya nani hasa alihusika na shambulizi husika na hatua zichukuliwe juu ya wahusika hao. Jambo hili litaondoa hali ya shutuma juu ya Serikali kuhusika na shambulizi hilo. Uchunguzi huru wa namna hiyo ufanyike juu ya kupotea kwa Ben Rabiu Saanane, mwanasiasa na mwanaharakati kijana, Mwanahabari Azory Gwanda, na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kibondo, Simon Kanguye.

4. Kurudisha hali ya ufanyaji siasa huru kwa vyama vya Upinzani iliyokuwepo kabla ya Serikali ya Awamu ya Tano kuingia madarakani, jambo hilo lihusishe kufutwa au kurekebishwa kwa Sheria Kandamizi k**a Sheria ya Habari ya mwaka 2016, Marekebisho ya Sheria ya Takwimu, Sheria Mpya ya Vyama vya Siasa, Sheria ya Mtandao (Cyber Crime) nk, pamoja na kuondoa zuio haramu la mikutano ya Vyama vya Siasa vya Upinzani nchini, kuunda Tume Huru ya Uchaguzi pamoja na kuwaondoa Wakurugenzi wa Halamashauri (ambao ni Makada wa CCM) kuwa Wasimamizi wa Uchaguzi nchini.

5. Serikali iache siasa huru na wazi nchini kwa kurudisha Bunge Live na kuzifuta kesi zote ilizowafungulia wanasiasa, wafuasi na wanachama wa vyama vya Upinzani nchini. Kufutwa kwa kesi hizo ambazo nyingi ni za kubambikia kutapunguza chuki ya kisiasa inayojengeka kwa kasi nchini na kurudisha umoja wa kitaifa unaopotea kwa kasi.

6. Iundwe K**ati ya Kitaifa ya Vipngoni na Wanasiasa wa Vyama vyote nchini ya kusaidia mazungumzo na mashirika na nchi wahisani ili kurudisha mahusiano mabaya ya sasa kati yao na nchi yetu, mahusiano yanayowafanya wakatishe, kuzuia au kuchelewesha michango yao ya kifedha kwenye Bajati ya Taifa.

2. Mabadiliko makubwa yafanyike Wizara ya Fedha na Benki Kuu ili kuwezesha uendeshaji mzuri wa sera za kiuchumi (Fiscal Policy) pamoja na usimamizi imara wa Fedha za Umma. Ripoti Maalum ya CAG juu ya Kutoonekana kwa TZS 1.5 Trilioni imeonyesha Hazina imeoza, na Athari zinazoonekana sasa kwenye uchumi, hasa kuporomoka kwa mitaji ya uwekezaji, zinataka mabadiliko makubwa yafanyike BOT.

Rais anaweza kumuomba Gavana wa zamani, Profesa Beno Ndulu, au mtu yeyote mwenye Kaliba yake, kuwa Mshauri Mkuu wa Uchumi kwa angalau mwaka mmoja wa mpito wa kurekebisha Uchumi.

MUHIMU:

Najua Rais magufuli hatafanya hata moja kati ya haya niliyoyashauri licha ya yeye mwenyewe kujua hali ni mbaya sana kiuchumi nchini, Lakini k**a Kiongozi wa Taifa hili ninao wajibu wa kutoa mchango wangu wa mawazo wa kututoa kutoa kwenye hali mbaya tuliyonayo.

Kabwe Z. Ruyagwa Zitto
Mbunge, Kigoma Mjini
Kiongozi wa Chama, ACT Wazalendo
Februari 25, 2019

Want your school to be the top-listed School/college in Tanga?

Click here to claim your Sponsored Listing.

Location

Category

Telephone

Address


Vifrem2015@gmail. Com
Tanga
BOX483KOROGWE

Opening Hours

Monday 08:00 - 18:00
Tuesday 08:00 - 18:00
Wednesday 08:00 - 18:00
Thursday 08:00 - 18:00
Friday 08:00 - 18:00
Saturday 09:00 - 18:00
Sunday 09:00 - 18:00