Maahad Imam shafii Tanga

Maahad Imam shafii Tanga Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Maahad Imam shafii Tanga, Education, Tanga.

فِي قَلْبِ تَنْغَا مَنَارُ العِلْمِ قَدْ سَطَعَا . . . وَمَعْهَدُ الشَّافِعِيِّ بِالفَخْرِ قَدْ رَفَعَا​رِيَاضُهُ الخَضْ...
09/05/2026

فِي قَلْبِ تَنْغَا مَنَارُ العِلْمِ قَدْ سَطَعَا . . . وَمَعْهَدُ الشَّافِعِيِّ بِالفَخْرِ قَدْ رَفَعَا
​رِيَاضُهُ الخَضْرَاءُ تَزْهُو فِي نَضَارَتِهَا . . . كَأَنَّهَا الجَنَّةُ الفَيْحَاءُ مُتَّسَعَا
​بِيئَةٌ تَسْكُنُ الأَرْوَاحُ فِي كَنَفٍ . . . وَيَنْشَرِحُ الفُؤَادُ لِمَنْ بِهَا طَلَعَا
​عُلُومُ دِينِ الهُدَى فِيهَا مُؤَصَّلَةٌ . . . تَسْقِي العُقُولَ بَيَانًا صَافِيًا نَصَعَا
​فِيهِ التُّقَى وَنُورُ الحَقِّ مُجْتَمِعٌ . . . يَا حَبَّذَا صَرْحُ عِزٍّ لِلْوَرَى نَفَعَا
​فَاسْلَمْ مَنَارًا يُضِيءُ الدَّرْبَ فِي شَمَمٍ . . . وَدُمْتَ لِلْأُمَّةِ الغَرَّاءِ مُرْتَبَعَا

MADHARA YA MIPIRA...NA SHEKH: SAALIM BARAHIYAAN
07/05/2026

MADHARA YA MIPIRA...NA SHEKH: SAALIM BARAHIYAAN

Nyd de videoer og den musik, du holder af, upload originalt indhold, og del det hele med venner, familie og verden på YouTube.

07/05/2026

Nyd de videoer og den musik, du holder af, upload originalt indhold, og del det hele med venner, familie og verden på YouTube.

18/02/2026

RAMADHANI DAY 01 | 2026 M 1447 H | SHEIKH MIRAJI ZUBER

UDUGU WA KIELIMU WAZIDI KUIMARIKA: KULIYYA AL-BARAKAH YAFANYA ZIARA MAAHAD IMAM SHAFII – TANGATanga:Katika kuendeleza ma...
14/01/2026

UDUGU WA KIELIMU WAZIDI KUIMARIKA: KULIYYA AL-BARAKAH YAFANYA ZIARA MAAHAD IMAM SHAFII – TANGA
Tanga:
Katika kuendeleza mashirikiano ya kielimu na kidini, Chuo cha Kuliyya ya Qur’an na Duruus Islamiyya Al-Barakah kutoka Tandale, Dar es Salaam, kimefanya ziara rasmi katika Maahad Imam Shafii, Tanga.
Ziara hiyo imelenga kuimarisha udugu wa kielimu na kuendeleza uhusiano wa kihistoria uliopo kati ya taasisi hizi mbili za Kiislamu, sambamba na kubadilishana uzoefu katika nyanja za elimu ya Qur’an na Duruus za Kiislamu.
Katika ziara hiyo, wanafunzi wa Maahad Imam Shafii wamepata fursa adhimu ya kuhamasishwa kujiunga na Chuo cha Al-Barakah kwa ajili ya kujiendeleza kimasomo, hususan katika fani ya Qur’an kwa mfumo wa Qira’at na Riwayaat, ambao ni msingi muhimu katika taaluma ya Qur’an Tukufu.
Akizungumza na wanafunzi, ujumbe wa hamasa umetolewa ukisisitiza kuwa changamoto za kielimu ni daraja la mafanikio, huku wanafunzi wakihimizwa kuwa na subira, uvumilivu na kumtegemea ALLAH katika safari yao ya elimu.
Aidha, wanafunzi wamekumbushwa kuwa fursa za kielimu hazijirudii mara nyingi, hivyo wametakiwa kuzitumia ipasavyo kwa bidii na juhudi kubwa ili kujijengea mustakabali bora wa kielimu na kidini.
Ziara hii ni sehemu ya juhudi endelevu za taasisi hizi katika kuhakikisha vijana wa Kiislamu wanapata elimu bora, madhubuti na inayojengwa juu ya misingi sahihi ya Qur’an na Sunnah.







Cc AL Burhan
Ibrahim Kimaro
Swaadiq Bin Mwesa

08/12/2025

💫 MUHADHARA
‼ MADA QUDUWA KABLA YA DAWAH :
▪Mtu awe mfano wa kuigwa kabla ya kuwaita wenzie katika kheri.
🎤🎙
SHEIKH ALLY KOMBO FUNDI
(Allah Amhifadhi)
📍📍 Masjid Abiibakary swidiq {Maahad Imam Shafii} Tanga.
🗓 16 - Jumadal-Akhirah - 1446H
🗓 07 - December - 2025M
IDARA YA NASHATWI MAAHAD IMAAM SHAFII


*HABARI**Tarehe: 07/12/2025**Mahali: Chuo cha Maahad Imaam Shafii, Sahare – Tanga*~Na~YAZIDU ABDLKARIM Sheikh Kombo Ally...
08/12/2025

*HABARI*

*Tarehe: 07/12/2025*
*Mahali: Chuo cha Maahad Imaam Shafii, Sahare – Tanga*
~Na~
YAZIDU ABDLKARIM

Sheikh Kombo Ally Fundi, mmoja wa wahadhiri na wanazuoni wanaoheshimika nchini, ametembelea chuo cha Maahad Imaam Shafii kilichopo Sahare jijini Tanga kwa ajili ya kufanya muhadhara maalumu na wanafunzi wa chuo hicho.

Katika ziara hiyo, Sheikh Kombo Ally Fundi alipokelewa kwa furaha na uongozi wa chuo, walimu pamoja na wanafunzi. Muhadhara uliofanyika ulihusu maadili ya mwanafunzi wa dini na wajibu wao katika jamii. Akizungumza na wanafunzi, Sheikh aliwakumbusha umuhimu wa kujenga tabia njema kabla ya kujishughulisha na kazi ya kuulingania watu katika haki (Dawah).

Akinukuliwa katika Nahasa yake, Sheikh alisema:
“Quduwa kabla ya Dawah – Mtu uwe mfano wa kuigwa kabla ya kuanza kuwaita wengine kwenye kheri.”

Aliwaeleza wanafunzi kuwa mwalimu au Da’iyah mwenye tabia njema ana nguvu kubwa ya kuathiri jamii kuliko yule anayeunga mkono haki kwa maneno lakini matendo hayaendani na yale anayoyafundisha.

Sheikh Kombo aliwatia moyo wanafunzi kuongeza juhudi katika kusoma Qur’ani, kuifuata Sunna, kutengeneza nia njema (Ikhlasi), na kuonyesha unyenyekevu katika kila jambo. Pia aliwakumbusha umuhimu wa kusimamia ibada, kuheshimu walimu, kushikamana na umoja, na kuwa mfano wa kheri ndani na nje ya chuo.

Ziara ilihitimishwa kwa dua na nasaha, huku wanafunzi wakionesha kufarijika na ujumbe mzito walioupata.

AL Burhan

15/10/2025

Watendaji wa Taassisi ya Ansaar Muslim Youth Centre (AMYC) wametakiwa kutilia umuhimu vyombo vya habari katika kuvitumia kwa lengo la kutangaza dini na maadili.

Hayo yameelezwa na Mudir wa Markaz Kuu, Sheikh Barahiyan katika kikao kilichofanyika leo Oktoba 15, 2025 katika ukumbi wa maktaba ya chuo cha Dini cha Maahad Imam Shafii kilichopo jijini Tanga.

Sheikh Salim amewataka waalimu wa chuo hicho pamoja na watendaji wa radio Ihsaan kushirikiana kwa pamoja katika kuhakikisha wanaitumia Radio Ihsaan kufikisha mafundisho mbali mbali yanayokwenda sambamba na kitabu cha Allah na Sunna za Mtume Swallallahu 'Alayhi wa Sallam.

Naye Naibu Mudir wa AMYC ambaye pia ni Mkuu wa chuo hicho, Sheikh Ally Nassor ameshauri kuandaliwa kwa mpango endelevu na muongozo utakaowasaidi walimu kuweza kuzalisha vipindi bora na vyenye tija kwa jamii.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Dini Markaz Kuu, Sheikh Abubakar Kassim amewataka waalimu hao wa Maahad Imam Shafii na watendaji wa Radio Ihsaan kuanza maandalizi ya kuhakikisha wanazalisha vipindi mbali mbali kwa lengo la kufikisha ujumbe wa elimu na maadili kwa kupitia vyombo hivyo vya Ihsaan Media.


ZIARA YA KIDA’WAH JIMBO LA TANGA MJINI PANDE MAREMBWE. -- KIOMONI
03/10/2025

ZIARA YA KIDA’WAH JIMBO LA TANGA MJINI
PANDE MAREMBWE. -- KIOMONI

Address

Tanga

Telephone

+255713408748

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Maahad Imam shafii Tanga posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share

Category