12/05/2026
Anaitwa Rehema Ng'watu Mwanafunzi Wa Kidato cha nne kutoka Shule ya Sekondari ya Wasichana Korogwe iliyopo Mkoani Tanga Wilaya ya Korogwe Aliyeshinda Tuzo ya Mwanamichezo Bora Wa K**e Kitaifa kutoka Tuzo za (BMT) Baraza la Michezo Tanzania Kwa Mwaka 2025
Hongera kwake, Hongera Uongozi Wa Shule Ukiongozwa na Mama Mauka na Mwalimu wake Wa Michezo Madam Mokiwa Kwa Usimamizi mzuri mpaka kufikia Hatua kubwa ya Kupata Tuzo ya BMT Kitaifa Kwa Mwaka 2025
11/12/2025
TAMASHA LA KOROGWE JOGGING FITNESS CLUB LAFANA KWA KISHINDO KIKUBWA KATIKA KUADHIMISHA MIAKA MITATU TANGU KUZINDULIWA KWAKE
Disemba 07 2025
CPA CHARLES MHANDO NJAMA Mbunge wa Jimbo la Korogwe mjini Alipata wasaa Wa kuwa Mgeni Rasmi katika Tamasha kubwa la Korogwe jogging fitness club ambapo Aliwapongeza KOROGWE JOGGING FITNESS CLUB Kwanza kwa Uongozi imara Wa kuweza kuandaa na kuratibu Tukio kubwa la aina yake ambapo takribani watu 600 Kutoka club mbalimbali mkoani Tanga walipata kuhudhuria
Mbali na kuwapongeza pia alitoa ushauri na kumuomba Afisa Michezo wa Halmashauri ya Mji Korogwe ya kwamba Korogwe na sisi tuwe na KOROGWE MARATHON itakayoratibiwa na Afisa Michezo pamoja na umoja Wa club za mazoezi hapa Korogwe ili mwisho wa siku tuzalishe fursa nyingine za kuweza kujiajiri kupitia mchezo huu Wa Marathon
Pia aliweza Kutoa zawadi Kwa washindi mbalimbali katika mchezo wa kukimbiza kuku pamoja Vyeti vya Ushiriki Kwa Jogging Mbalimbali zilizohudhuria Tamasha hilo
02/12/2025
Picha za matukio mbalimbali katika Uzinduzi wa Mashindano ya mpira Wa Miguu yanayojulikana k**a NJAMA AMANI NA UZALENDO CUP yalifanyika mjini KOROGWE TANGA
02/12/2025
Disemba 01 2025 katika kata ya Kwamndolwa MH WILLIAM MWAKILEMA ambaye ni mkuu wa Wilaya ya Korogwe mkoani Tannga amezindua Rasmi Mashindano ya mpira Wa Miguu football yanayohusiaha Timu 32 ambapo Timu 16 zinatoka Halmashauri ya Korogwe mjini na Timu 16 zinatoka Halmashauri ya Korogwe vijijini
Mashindano haya yanajulikana k**a
NJAMA AMANI NA UZALENDO CUP Malengo ya Mashindano hayo ni kuwaunganisha vijana katika jukwaa moja ili kuleta burudani, upendo na Amani pili Kutoa fursa ya Ajira Kwa vijana kuonyeaha vipaji vyao ili mwisho wa siku wafike katika club kubwa hapa Tanzzania
Pamoja na kuwaleta vijana katika jukwaa moja vilevile Mashindano haya ni moja ya ahadi za Mbunge alizoahidi kipindi cha Kampeni ya kuwa Atafanya Michezo kuwa Ajira , Burudani na ni njia ya ushik**ani katika jamii