23/11/2021
Kufaulu si kupita mtihani unaofanywa siku moja au mbili shuleni, si kusomea taaluma kisha urudi kitini ukakae, si kuwa na pesa nyingi wala si kumiliki mali nyingi hapa duniani bali ni kuutafuta ulipo ubora wako kisha kuifanyia kazi mpaka ukapata unachohitaji katika maisha yako kabla hujaiaga dunia. Kwa hiyo wewe dada yangu, wewe ndugu yangu, jaribu sana kujiweka katika mkutano kila wakati kisha ujisikize na bila shaka utapata uliyezaliwa kuwa. Huenda;
Haukuumbwa kuwa mwalimu, dereva, daktari, mkulima, Imam, mwadhini, mzegazegaa,tarishi, kiongozi wa shule au kampuni, kandawala, mwanahabari, mhariri au hata rubani lakini ukajipata katika taaluma moja au nyingine.
Moyo wako hauna amani hata chembe; unajidanganya tu kwa kujikaza. Tafuta taaluma yako kisha ifanyie kazi utayaona matokeo yake.
Wassalam!