Injili MOTO- Mwl. Amani C. Maswaga

Injili MOTO- Mwl. Amani C. Maswaga This page aims at providing BIBLICAL TEACHINGS and GOSPEL that will help unsaved ones to become saved, and hence making the prevailing Generation healthy!!

12/11/2025

Shout out to my newest followers! Excited to have you onboard! Neema Isaya, Ashura Jackson, Carolyn Mwangi, Paster Yohana Mollel, Asbela Miguti. May God bless you indeed!!

!!!

04/09/2024

Keep mentioning "YOUTHS TO JESUS MINISTRY" in your daily prayers.

Jesus will surely reward you.
© Mwl. Maswaga, A.C - Founder!

04/11/2022

Tiwa moyo na hii tena katika Jina la Yesu ...

*NGUVU YA KIBALI KUTOKA KWA BWANA*
--------------------------
Sikia,

Kibali ni kitu cha ajabu sana,,, tena zaidi sana kiwe ni kibali Kutoka kwa BWANA mwenyewe!---aisee utaishi wa raha sana!!!

Somo hili ni pana mno ila LEO Nataka nikutazamishe jambo moja juu ya kibali hiki kinachotoka kwa Bwana.

Iko hivi ,,,,

""" _*ILE KWAMBA UNACHO KIBALI KUTOKA KWA BWANA,, HAIMAANISHI KILA MTU ATAKUKUBALI*_ """".

Umenielewa ninachosema????

---usije ukasema mbona natukanwa , nanenwa vibaya ,,,
Mbona watu hawa hawanikubali, wananichukia tu ,,,Mbona kazi yangu haipendwi na marafiki zangu hawa,,,Mbona ! Mbona! Mbona! Mbona hivi na vile ,,, basi mimi Sina Kibali!!!

LA HASHA!!!
Mimi nakwambia kibali unacho,,,ila hujajua sifa za kibali cha Mungu!

Moja ya sifa hizo ndio ambayo naieleza hapa,,,,,

Kuwa
""" *SI KILA MTU ATAKUKUBALI ,PALE MUNGU AKIKUKUBALI* !!!""""

Unapaswa uelewe hilo,,,

Haya mazingira yalimkuta Mwokozi wetu YESU Kristo

Ona...

"" _Naye Yesu akazidi kuendelea katika hekima na kimo, AKIMPENDEZA MUNGU NA WANADAMU_ """
[ Luka 2: 52 ]

Ona hapo,,,↑↑↑

Swali !

Je, k**a Yesu aliwapendeza wanadamu *WOTE* (maana alipata kibali kwa Mungu),,, *NI WANADAMU GANI TENA AMBAO* walimpiga, walimtukana, walimsengenya na hata kumuua ❓❓❓❓❓
..basi tambua kuwa pamoja na kuwa alipewa kibali kwa Bwana,,,lakini *SI_WOTE WALIOMKUBALI*!!!!--------wapo walioendelea kumpinga katika mambo yake yote---hata nduguze walithubutu kumpinga!

Jambo jema ni hili,

Kibali cha Bwana kinapokuwa juu yako *UTAFANIKIWA KATIKA MAMBO YAKO YOTE*!(siyo mambo baadhi , ni YOTE)---umenisikia???????

haijalishi watu 100 watakupinga juu ya hatua yako moja unayotaka kuipiga ,,,,lakini BWANA ATAKUPA KIBALI kwa mtu mmoja TU atakayekuwezesha KUIFANIKISHA HATUA YAKO HIYO!!!!

Watakupinga wakitarajia kukuona umekwama ,,,chaajabu wanakuona UMEVUKA ng'ambo!!!
--- *wanajiuliza UMEVUKAVUKAJE hapo,,??????,,,*.ukiwasikia unawajibu """" NINAYE MTOA KIBALI---- ndiye Mungu Mkuu !

Oooooooh JESUS! JESUS! JESUS!

*IMO NGUVU KUBWA NDANI YA KIBALI CHA BWANA*,,,,----asikwambie Mtu aisee .

©Mwl. Maswaga, A.C
Njombe, Tanzania~ Now!
🙏🏼🙏🏼🙏🏼

KEEP PRAYING FOR THIS MINISTRY PLEASE.
23/07/2021

KEEP PRAYING FOR THIS MINISTRY PLEASE.

24/10/2019

OKOKA SASA,,, ACHA DHAMBI !!!

31/10/2018

INJILI BADO INASONGA MBELE WAPENDWA...

mafundisho yataendelea muda mchache ujao!

Barikiweni Sana !!!

24/09/2017

SOMO: MAADUI ZAKO WOTE WATAYEYUKA KATIKA JINA LA YESU

""Na mara tuliposikia hayo MIOYO YETU ILIYEYUKA, wala HAUKUSALIA UJASIRI wo wote katika mtu awaye yote, kwa sababu yenu; kwa kuwa Bwana , Mungu wenu, yeye ndiye Mungu, katika mbingu juu, na katika nchi chini""
[Yoshua 2:11]
..
shalom Mtu wa Mungu!
>>hakuna mtu aliyeokoka amabaye hana maadui,,,k**a huna basi jichunguze vizuri.

Unajua kwa nini ni LAZIMA uwe na maadui????
>>>Ni kwa sababu MUNGU AMEWEKA KUSUDI NDANI YAKO LA KULITIMIZA DUNIANI,,, hivyo shetani kupitia watu anapambana na wewe kuliua hilo kusudi ndani yajko.

tunaenda pamoja?

lakini, leo hii nakutangazia USHINDI kuwa KILA ADUI YAKO anaepambana na kusidi la Bwana lililokondani yako, Atakaposikia habari zako ATAYEYUKA MARA.

nasema,,, NI LAZIMA AYEYUKE MBELE ZAKO!

HATAKUWA NA UJASIRI tena mbele zako maana Mungu wa nchi na mbingu yu upande wako!

nsema hiyo Roho inayoinuka kinyume na huduma yako, afya yako, uchumi wako, familia yako, masomo yako, kazi yako, mahusiano yako, na mafanikio yako yote IYEYUKE MARA MOJA KATIKA JINA LA YESU KRISTO WA NAZARETHI!!!

nakutakia baraka za Bwana Daima!

ameeni!

14/08/2017

*CHAKULA CHA BWANA NDICHO KITUFANYACHO TUISHI*
----------------------------------

→kazi ya chakula ni kukifanya kile kilichohai kiendelee KUWA HAI,,,---

→kwa lugha rahisi ningeweza kusema *CHAKULA NI UHAI*

>>k**a wana wa Mungu ili tuweze kuishi na kustawi milele,,, ni lazima *tukipate chakula cha Mungu*

sikia,,,

Chakula cha Mungu ni hiki hapa:-

""" *KUYAFANYA MAPENZI YA MUNGU SIKU ZOTE* """
---
Ona hapa Yesu anachosema....

"" Chakula Changu ndicho hiki, *niyatende Mapenzi yake aliyenipeleka*,nikaimalize kazi yake"""
[Yoh 8: 34]

Unasikia anachosema hapo??????....
→tukijua tupo duniani *kwa sababu gani*, tutayatafuta na kuyafanya Mapenzi yake aliyetupeleka hapa,, na si kitu kingine...
..hatujaja kujenga majumba hapa duniani,,, hatujaja kula nankunywa ,,hatujaja kujiremba hapa duniani,,,.sikia,...

" *Tumekuja kwa kusudi maalumu*....

lipi hilo..????

*KUYAFANYA MAPENZI YA MUNGU KWANZA*

unanisikia ninachosema???
....

→Ni lazima Mapenzi yetu *yafe kwanza* ,,ndipo tutaweza KUYAFANYA Mapenzi ya BABA....

Sikia maneno ya wimbo huu wa Tenzi...
👇🏻
👇🏻
👇🏻

4. "" Mapenzi yako yafanyike,
Natoa kwako *vitu vyote*
*MAISHA,MALI, MOYO,MWILI*
Vyote ni vyako, *kweli kweli*""

5. ""Mapenzi yako yafanyike,
*Mapenzi yangu "yavunjike*,
Ninakubali uwe Bwana,
Ni mali yako, *twaa kabisa*""

[ TENZI 91 ]
.barikiwa sana,,,na asubuhi njemA...

©Mwl. Maswaga,A.C,
( _The Visionary_ )

31/07/2017

Shalom!

DAWA YA DHAMBI ZOTE NA UOVU WOTE!
--------------------------------------------------------..
ili uweze kuishinda DHAMBI na UOVU wa kila namna yafuatayo yawe SEHEMU YA MAISHA YAKO:-

1. Omba sana na kwa bidii!

2. Funga sana pia,(fast)

3. Soma NENO LA MUNGU kwa bidii !!

4. Tafakari ukuu wa Mungu siku zote na kila wakati!

5. SHUHUDIA ukuu wa Mungu popote ,kwa mtu yeyote na kwa wakati wowote!!!

6. IWEKE WAZI NJOZI YAKO
→put your VISION clearly (openly),,, hakikisha haikupotei hata dakika moja!..PASIPO MAONO WATU HUACHA KUJIZUIA...!,,, yaani MAONO(VISION) itakupa adabu, nidhamu, uwezo wa kuweka vipaumbele!!!
...naishia hapo kwa leo..

Barikiwa sana!!!

ENDELEA KUIOMBEA HUDUMA HII NA MUNGU ATAKUBARIKI ZAIDI!!!

07/06/2017

*USIDANGANYIKE*

"" Hata kwenye *Movies* ulizowahi kuziangalia dada ambaye huwa anaigiza k**a *KAHABA*,,au *MZINZI*, au *MALAYA* ,ama *JINI* na maeneo mengine k**a hayo...
Dada huyo huwa ANAVAA aitha *SURUALI* au *VINGUO VIFUPI au VILIVYOBANA* na vyote vinavyofanana na hivyo.. Ili awe *VECTOR* mzuri wa hicho anachokiigiza hapo!!!"""
.........
Hata SHETANI anajua kuwa nguo k**a hizo si kwaajili ya wadada!!!..huo ni mpango wa shetani!!...hiyo ni *Fashion ya KUZIMU*,,,hamna kupindisha hapo!!!....hakuna kujifariji hata kidogo.....SHETANI ANAJUA ALIPEWA *MUDA MFUPI* SANA.., hivyo agenda zake anazipeleka *geometrically* na siyo
*arithmetically*!!!!
..uwe na tafakari njemA...

*©Mwl. Maswaga, A.C,*

05/06/2017

!
--------------------------------------------
sikia ...
Ukipenda na kutenda dhambi,,, UTAKUFA!!!...
Unapopenda dhambi na kuitenda pia itakuua kabisa katika maeneo haya:-....
1. Itaua IMANI yako kwa Mungu.
2. KARAMA au HUDUMA yako itakufa pia..
..ulikuwa unajua kuimba ,,utaona HUWEZI TENA,,,...ulikuwa mwombaji sana,,, lkn utajikuta hata HAMU YA KUOMBA HUNA....uliwapenda sana waliookoka,,lkn utaona UNAWACHUKIA TU..Kisa dhambi

3. UJASIRI WAKO utakufa pia,,,
4. MAFANIKIO YAKO hufa pia
5. Ulinzi wako unakufa pia....maana tunalindwa na NGUVU za Mungu kwa njia ya imani...hivyo imani ikifa, na ulinzi wako unakufa pia...
6. AKILI ZAKO pia zinakufa.....akili yako inatiwa GANZI,,yaani haiwi active tena......unakuwa UPO UPO tu...

7. AMANI YAKO INAKUFA PIA.......maandiko yanasema "" HAKUNA AMANI KWA WABAYA"""

8. FURAHA YAKO INAKUFA PIA........utajitahidi KUCHEKA lkn hutakuwa na FURAHA....utafungika ndani yako...utapata Ukengeufu....

9. UMUHIMU WA KUISHI HUTAUONA TENA....yaani nao pia unakufa....

10. MAONO au VISION YAKO INAKUFA PIA.........k**a hutajizuia katika kutenda dhambi,,, hata MAONO yako yanakufa...unapoteza kitu kinaitwa "FOCUS". ...utakuwa huna mbele wala nyuma....
...ndugu yangu sikia...
....Mtu akila zabibu mbichi,,,mwishowe GANZI ITAYASHIKA MENO YAKE...na ndipo itakapokuwa vigumu kufurahia ZABIBU MBIVU!!!!
.........
""" Hamjafanya vita bado kushindana na dhambi, hata kumwaga damu "'''

*DAHMBI NI HATARI SANA*

barikiwa sana,

Address

Njombe

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Injili MOTO- Mwl. Amani C. Maswaga posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The School

Send a message to Injili MOTO- Mwl. Amani C. Maswaga:

Shortcuts

Share

Category