01/05/2026
Karibu tena Mhe. Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi (NACTVET) (), Bi. Bernadetta Ndunguru.
Sisi JEMA Institute of Technology tunaahidi kuendelea kutekeleza kikamilifu matakwa ya mfumo wa CBET (Competence Based Education and Training), na kuendelea kuzalisha wataalamu wenye ujuzi wa vitendo watakaoweza kutatua changamoto mbalimbali katika sekta ya Madini na Teknolojia.
Aidha, tumepokea kwa shukrani pongezi zako kwa kutambua namna chuo chetu kinavyozingatia kwa umakini taratibu, miongozo na viwango vinavyowekwa na Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi (NACTVET) ().