Moshi Co-operative University

Moshi Co-operative University Moshi Co-operative University (MoCU)

29/08/2026
WATUMISHI WA MOCU WAJENGEWA UWEZO KUHUSU ELIMU JUMUISHI NA MASUALA YA JINSIAChuo Kikuu cha Ushirika Moshi (MoCU) kimeend...
29/08/2026

WATUMISHI WA MOCU WAJENGEWA UWEZO KUHUSU ELIMU JUMUISHI NA MASUALA YA JINSIA

Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi (MoCU) kimeendesha mafunzo kuhusu Elimu Jumuishi na Masuala ya Jinsia, yaliyofanyika tarehe 28 Agosti 2026 katika ukumbi wa Weruweru Lodge, mkoani Kilimanjaro.

Mafunzo hayo yaliyowahusisha Watumishi wa Chuo yamefadhiliwa na Mradi wa Elimu ya Juu kwa Mageuzi ya Kiuchumi (HEET) unaotekelezwa na Serikali kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia.

Akifungua mafunzo hayo, Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo Prof. George E. Matto, alimpongeza Mratibu wa Masuala ya Jinsia(kupitia timu ya inayoratibu mradi huo - Chuoni), Dkt. Asteria Ngaiza, pamoja na wawezeshaji kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, ambao ni Dkt. Lulu Mahay na Prof. Sarah Kisanga, kwa kufanikisha mafunzo hayo.

Prof. Matto amesema kuwa mafunzo hayo yanalenga kuwawezesha washiriki kupata uelewa wa kuzuia na kukemea vitendo visivyofaa, pamoja na kuchukua hatua pale changamoto zinapotokea.

Amesisitiza kuwa ni wajibu wa kila mwanajumuiya ya MoCU kutumia maarifa anayopata katika kujenga mazingira yenye usawa, utu, heshima na ujumuishi.

Mafunzo hayo ni sehemu ya utekelezaji wa miongozo mbalimbali ya Serikali kuhusu elimu na masuala ya jinsia, na yamehitimisha awamu ya mafunzo yaliyokuwa yakitekelezwa kwa hatua tangu mwaka 2021, lengo likiwa ni kuendeleza uelewa na uwajibikaji wa Watumishi katika kukuza mazingira jumuishi ndani ya Chuo.

MoCU YAENDELEA NA SAFARI YA KUONDOA HATI MBAYA KATIKA VYAMA VYA USHIRIKA KUPITIA MAFUNZOChuo Kikuu cha Ushirika Moshi (M...
24/08/2026

MoCU YAENDELEA NA SAFARI YA KUONDOA HATI MBAYA KATIKA VYAMA VYA USHIRIKA KUPITIA MAFUNZO

Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi (MoCU), Ofisi ya Mkoa wa Ruvuma kwa kushirikiana na Kamati ya Elimu ya Maendeleo ya Ushirika Mkoa wa Ruvuma (KAMEURU) na Chama Kikuu cha Ushirika Tunduru (TAMCU LTD), imeanza hatua muhimu ya kuimarisha uandishi na usimamizi wa vitabu vya hesabu katika Vyama vya Ushirika vya Msingi Wilayani Tunduru.

Katika hatua hiyo, MoCU, KAMEURU na TAMCU LTD wamefanya Kikao Kazi cha Maandalizi ya Kambi Maalumu ya Mafunzo ya Programu ya Uandishi wa Vitabu vya Hesabu za Vyama vya Ushirika (PUVU) na kukubaliana kuendesha Kambi hiyo katikati ya Mwezi Septemba 2026, Tunduru Mjini.

Kambi hiyo inalenga kuwawezesha Watendaji wa AMCOS kupata maarifa na ujuzi wa vitendo katika uandishi sahihi wa vitabu vya hesabu, utunzaji wa kumbukumbu za fedha, uwazi, uwajibikaji na usimamizi bora wa rasilimali za vyama.

Programu inatarajiwa kuwanufaisha zaidi ya Watendaji 80 wa AMCOS zinazosimamiwa na TAMCU LTD, ikiwa ni sehemu ya jitihada

Timu ya Wataalamu na wabunifu wa Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi (MoCU) iko tayari kwaMaadhimisho ya wiki ya  Elimu, Ujuzi...
24/08/2026

Timu ya Wataalamu na wabunifu wa Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi (MoCU) iko tayari kwa
Maadhimisho ya wiki ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu yanafungwa leo 24 Agosti, 2026 na Waziri Mkuu wa Jamhuri Ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba

Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi (MoCU), Prof. Alfred Sife, ameongoza Kikao cha 44 cha Seneti ya Chuo kilich...
21/08/2026

Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi (MoCU), Prof. Alfred Sife, ameongoza Kikao cha 44 cha Seneti ya Chuo kilichofanyika leo, tarehe 21 Agosti 2026, katika kampasi kuu, Moshi.

Kikao hicho ni sehemu muhimu ambapo wajumbe wa Seneti hukutana, kujadili na kuridhia kuhusu masuala mbalimbali ya taaluma, utafiti, ushauri wa kitaalamu pamoja na shughuli nyingine muhimu zinazoangazia ustawi wa taasisi.

MoCU yachochea ubunifu na fursa katika usindikaji wa zao la ndizi Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi (MoCU) kimeonyesha ubuni...
21/08/2026

MoCU yachochea ubunifu na fursa katika usindikaji wa zao la ndizi

Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi (MoCU) kimeonyesha ubunifu na fura ya usindikaji wa zao la ndizi katika Maadhimisho ya Wiki ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu yanayoendelea katika viwanja vya Shule ya Sekondari Usagara iliyopo mkoani Tanga.

Katika maonesho hayo, MoCU imewasilisha bidhaa na mbinu mbalimbali zinazolenga kuongeza thamani ya ndizi, kupunguza upotevu wa mazao na kuwawezesha wakulima na wajasiriamali kupata fursa zaidi za kiuchumi.

Ubunifu huo umeelezwa kuwa ni sehemu ya juhudi za kuunganisha elimu, ujuzi na teknolojia na mahitaji halisi ya jamii, hususan katika kuongeza tija na thamani ya mazao ya kilimo.

MoCU yawaalika Wananchi kujifunza na kugundua fursa mbalimbaliChuo Kikuu cha Ushirika Moshi (MoCU) kinaendelea kuvutia w...
21/08/2026

MoCU yawaalika Wananchi kujifunza na kugundua fursa mbalimbali

Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi (MoCU) kinaendelea kuvutia wadau mbalimbali katika Maadhimisho ya Wiki ya Kitaifa ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu, yanayoendelea katika viwanja vya Shule ya Sekondari Usagara, Tanga.

Wananchi wanapata fursa ya:
📚 Kufahamu programu mbalimbali za mafunzo zinazotolewa na MoCU
💡 Kujifunza na kugundua fursa za elimu, ujuzi na ubunifu
👩‍🏫 Kunufaika na ushauri kutoka kwa wataalamu wa Chuo
🤝 Kufahamu huduma mbalimbali zinazotolewa

Bado hujachelewa! 🔥
📌 Fika banda la MoCU leo—jifunze, gundua fursa na chukua hatua kuelekea mafanikio yako!

📍 Shule ya Sekondari Usagara, Tanga

Address

Moshi Co-operative University (MoCU)
Moshi
027

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Moshi Co-operative University posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The School

Send a message to Moshi Co-operative University:

Shortcuts

Share