College of Veterinary Medicine and Biomedical Sciences - SUA

College of Veterinary Medicine and Biomedical Sciences - SUA Welcome to the College of Veterinary & Medical Sciences.(CVMS) at Sokoine University of Agriculture for , , and ,services

The Veterinary education in East Africa started in 1942 in Makerere College which was affiliated to University of London in 1959, this Veterinary school shifted from Uganda (Makerere University) to Kenya and 1962 the School was incorporative into University Collage of Nairobi, Kabete Campus. Later the school was elevated to Nairobi Faculty of Veterinary Medicine in 1972 and started to award the Bachelor of Veterinary Medicine. In Tanzania the Veterinary Education started when the division of Veterinary Science was established under the Faculty of Agriculture and Forest of University of Dar es Salaam 1976. After establishment of Sokoine University of Agriculture, the Division of Veterinary Science was elevated to form the Faculty of Veterinary Medicine. Initially the Faculty was offering the Bachelor of Veterinary Science (BVSc) which was later changed to Bachelor of Veterinary Medicine (BVM). Currently, in addition to BVM the College also offers the Bachelor of Biotechnology and Laboratory Science (BLS) and postgraduate degrees at Masters and PhD Levels.

30/06/2024

Tumefika tena nusu ya mwaka 2024. Tunamshukuru Mungu na tunamuomba kudra zake ziendelee kuwa nasi tunapoingia katika nusu ya pili ya mwaka

Uchafuzi wa Sumukuvu (Aflatoxin) katika Mahindi: Visababishi, Athari, na Hatua za UdhibitiMahindi, hutumika k**a chakula...
10/05/2024

Uchafuzi wa Sumukuvu (Aflatoxin) katika Mahindi: Visababishi, Athari, na Hatua za Udhibiti

Mahindi, hutumika k**a chakula cha msingi kwa mamilioni duniani kote. Hata hivyo, uwezekano wake wa kuchafuka na aflatoxin husababisha hatari kubwa kwa afya na changamoto za kiuchumi. Aflatoxins ni kemikali inayosababisha kansa na madhara mengine inayozalishwa hasa na kuvu (fungus) aina ya Aspergillus, hususan Aspergillus flavus na Aspergillus parasiticus.
Uchafuzi wa aflatoxin katika mahindi hutokea hasa kwenye hali maalum za mazingira, ikiwa ni pamoja na joto kali, unyevu, na uhifadhi mbovu wa mahindi. Mazao ya mahindi huwa katika hatari kubwa hasa wakati wa awamu za kabla ya mavuno, wakati wa mavuno, na baada ya mavuno. Mahindi kutokaushwa sawa sawa na kuhifadhiwa isivyostahili huongeza hatari ya ukuaji wa kuvu na uzalishaji wa aflatoxin. Aidha, mimea ya mahindi inaweza kuwa katika hali ya msongo kutokana na ukame au uvamizi wa wadudu, kuongeza zaidi uwezekano wa maambukizi ya kuvu.
Athari za Uchafuzi wa Aflatoxin:
Uwepo wa aflatoxin katika mahindi una athari kubwa kwa afya ya binadamu na wanyama pamoja na kiuchumi. Kula mahindi yaliyo na aflatoxin kunaweza kusababisha matatizo ya afya ya ghafla na ya muda mrefu, ikiwa ni pamoja na uharibifu wa ini, upungufu wa kinga, na ongezeko la hatari ya saratani ya ini. Wanyama wanaolishwa na mahindi yaliyochafuliwa na aflatoxin wanaweza kudumaa, kupungukiwa na kinga, na hata kufa. Kwa upande wa kiuchumi, uchafuzi wa aflatoxin husababisha hasara kubwa kifedha kutokana na bidhaa zinazokataliwa kwa ajili ya kuuza nje, kupungua kwa thamani sokoni, na gharama zinazohusiana na usimamizi na kupunguza uchafuzi wa aflatoxin.
Hatua za Udhibiti:
Udhibiti wenye ufanisi wa uchafuzi wa aflatoxin katika mahindi unahitaji mkakati uliojikita katika hatua za kabla ya mavuno, wakati wa mavuno, na baada ya mavuno:
Hatua za Kabla ya Mavuno:
• Kudhibiti uvamizi wa wadudu kwenye mimea ya mahindi.
• Kuboresha rutuba ya udongo na ikiwezekana kufanya umwagiliaji pale inapobidi ili kukuza ukuaji wa mahindi wenye afya na kupunguza uwezekano wa maambukizi ya kuvu.
• Kutumia aina za mahindi yasiyoathirika kirahisi na aflatoxin.
Wakati wa kuvuna:
• Kuvuna mahindi kwa wakati ili kupunguza athari za hali mbaya ya hewa.
• Kuhakikisha mbinu sahihi za uvunaji ili kupunguza uharibifu wa mitambo na uchafuzi.
Usimamizi Baada ya Mavuno:
• Kukausha haraka mahindi yaliyovunwa hadi kiwango cha unyevu chini ya 14% ili kuzuia ukuaji wa kuvu.
• Kutumia vifaa sahihi vya kuhifadhi k**a mifuko ya kuhifadhi ya “kinga njaa” au vihenge vya bati (silos) zilizo na mifumo ya uingizaji hewa ili kuzuia kuzidi kwa unyevu na ukuaji wa kuvu.
• Kufanya vipimo vya mara kwa mara vya sampuli za mahindi kwa viwango vya aflatoxin kwa kutumia njia sahihi za uchambuzi.
Hivyo basi;
Uchafuzi wa aflatoxin katika mahindi unasababisha changamoto kubwa katika usalama wa chakula, afya ya umma, na uchumi wa kilimo. Kutatua suala hili kunahitaji juhudi za pamoja kutoka kwa wadau mbalimbali, ikiwa ni pamoja na wakulima, watafiti, watengeneza sera, na wasindikaji wa chakula. Kwa kuchukua njia zenye kujumuisha hatua za kabla ya mavuno, wakati wa mavuno, na baada ya mavuno, tunaweza kupunguza uchafuzi wa aflatoxin katika mahindi, kuhakikisha usalama na ubora wa zao hili muhimu la chakula kwa idadi ya watu duniani kote.

Wanafunzi wa BVM SUA... Katika mafunzo kwa vitendo Serengeti NP.... Wamemlaza simba ili kumfanyia uchunguzi
19/03/2022

Wanafunzi wa BVM SUA... Katika mafunzo kwa vitendo Serengeti NP.... Wamemlaza simba ili kumfanyia uchunguzi

SUA STUDENTS.... Immobilizing and sampling from a Buffalo... Wanafunzi wa mwaka wa tano BVM na mhadhiri wao Dr Richard S...
18/03/2022

SUA STUDENTS.... Immobilizing and sampling from a Buffalo... Wanafunzi wa mwaka wa tano BVM na mhadhiri wao Dr Richard Samson (aliyevaa nguo ya blue) wakiwa Serengeti national park kwenye mafunzo

SUA student... Bachelor of science in Laboratory Science and Biotechnology akifanya "full blood picture" katika hospital...
17/03/2022

SUA student... Bachelor of science in Laboratory Science and Biotechnology akifanya "full blood picture" katika hospitali ya Nyamagana Mwanza... Wanafunzi wapo kwenye field practical training

28/01/2022

One of the few academic institutions with credibility remaining in Tanzania

Tunawapongeza wahitimu wetu leo
28/05/2021

Tunawapongeza wahitimu wetu leo

Kudhibiti aflatoxin
19/05/2021

Kudhibiti aflatoxin

KUSAGA MAHINDI NA KUDHIBITI HEWA YAWEZA KUPUNGUZA UCHAFUZI WA SUMUKUVU (AFLATOXIN B1) Sumukuvu ni aina ya sumu inayozalishwa na kuvu (fungi) aina ya Aspergillus. Sumu hii huchafua vyakula kwa sababu kuvu wa Aspergillus hupendelea kuota kwenye aina mbalimbali za vyakula k**a mahindi, karanga, mihogo....

Address

College Of Veterinary Medicine And Biomedical Sciences, Sokoine University Of Agriculture, P. O. Box 3015, Chuo Kikuu, Morogoro, Tanzania. Tel: +255 23 260 4647 +255 260 3511/4 Fax: +255 23 260 4647 E
Morogoro
67125

Opening Hours

Monday 07:30 - 15:30
Tuesday 07:30 - 15:30
Wednesday 07:30 - 15:30
Thursday 07:30 - 15:30
Friday 07:30 - 15:30

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when College of Veterinary Medicine and Biomedical Sciences - SUA posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The School

Send a message to College of Veterinary Medicine and Biomedical Sciences - SUA:

Shortcuts

Share