08/03/2025
Maziko ya mwanafunzi Mhoja Maduhu aliyekuwa akisoma kwenye shule ya sekondari Mwasamba ambaye anadaiwa kufariki kutokana na kupigwa viboko na mwalimu wake yanatarajiwa kufanyika leo Machi 8, 2025.
Tayari mwili wa mwanafunzi huyo umewasili nyumbani kwao kwenye kijiji cha Lutubiga wilayani Busega mkoani Simiyu kwa ajili ya shughuli za maziko.
Wakiwa kwenye msafara wa kuusindikiza mwili huo nyumbani hapo waombolezaji wameonekana wakiwa na ujumbe ulioandikwa kwenye mabango ‘Kupiga Sio Kufundisha’.
Imeandaliwa na Rehema Evance
Mhariri