Daniel Masubo

Daniel Masubo Iwe Unataka Mafanikio ya Kifedha, Afya Njema, au Kuwa na Mahusiano Bora. Tutakusaidia Uwe Bora Zaidi!

Ujinga ni kukosa maarifa, ujuzi, ufahamu, na uelewa. Katika maisha haya, unachokijua ndiyo ulinzi wako. Mafanikio yako k...
10/01/2024

Ujinga ni kukosa maarifa, ujuzi, ufahamu, na uelewa. Katika maisha haya, unachokijua ndiyo ulinzi wako. Mafanikio yako katika kufanya jambo lolote yanategemea ufahamu wako katika jambo hilo. Pasipo maarifa sahihi mtu anakosa nguvu za kufanikisha mambo. Ujinga ni sawa na uhanithi.
!

Mwandishi Napoleon Hill anasema neno elimu, chimbuko lake ni kutoka katika neno la kilatani "educo" lenye maana ya kuend...
09/01/2024

Mwandishi Napoleon Hill anasema neno elimu, chimbuko lake ni kutoka katika neno la kilatani "educo" lenye maana ya kuendeleza kitu kutoka ndani. Kwa mantiki hii, elimu kwa mtu ni zaidi ya kwenda shule kujifunza kuandika, kuchora, kusoma, au kuhesabu herufi na namba. Kuendeleza kilicho ndani ya mtu ni elimu bora zaidi kuliko ya kumfundisha kuhesabu, kuandika na kusoma herufi na namba.
!

Nelson Mandela, baba wa taifa wa Afrika Kusini aliwahi kusema "Elimu ndiyo silaha pekee ambayo mtu anaweza kuitumia kuba...
07/01/2024

Nelson Mandela, baba wa taifa wa Afrika Kusini aliwahi kusema "Elimu ndiyo silaha pekee ambayo mtu anaweza kuitumia kubadilisha ulimwengu." Nao wahenga walisema "Elimu ni ufunguo wa maisha." Umechoka kuwa mtu maskini? Pambana kutafuta hekima, ufahamu na maarifa sahihi.
!

Watu wengi wanaishi katika umaskini kwa sababu tu hawajatambua vyanzo vya umaskini wao. Kwavile hawajui sababu zinazopel...
05/01/2024

Watu wengi wanaishi katika umaskini kwa sababu tu hawajatambua vyanzo vya umaskini wao. Kwavile hawajui sababu zinazopelekea umaskini wao, wanaendelea kuishi katika ujinga huo miaka nenda rudi pasipo mabadiliko. Wanaishi kwa mazoea na wanafanya mambo yao kwa namna ileile ya miaka yote. Wasichokijua ni kuwa kufanya mambo kwa namna ileile, mara kwa mara huku ukitegemea matokeo tofauti ndiyo uchizi wenyewe huo.
!

Kuna watu wa kuepukana nao ili kujiunga na makundi ya watu sahihi watakaokujenga na kukuongezea hamasa ya kupambana vita...
04/01/2024

Kuna watu wa kuepukana nao ili kujiunga na makundi ya watu sahihi watakaokujenga na kukuongezea hamasa ya kupambana vita dhidhi ya umaskini. Kuna fıkra, akili, mitazamo na mawazo ya kimaskini ambavyo kila mtu anatakiwa kuepukana navyo ili kupambana vita ya umaskini. Kuna maneno na mazingira ya kuepukana nayo k**a kweli mtu unataka kushinda vita dhidhi ya umaskini.
!

Hizi ni nyakati ambazo watu wengi siyo waaminifu.Tunaishi katika kipindi ambacho watu waaminifuwanapatikana kwa nadra sa...
04/01/2024

Hizi ni nyakati ambazo watu wengi siyo waaminifu.

Tunaishi katika kipindi ambacho watu waaminifu

wanapatikana kwa nadra sana. Hizi ni zama ambazo

binadamu amegeuka kuwa ni adui mkubwa wa wanadamu wenzake. Binadamu amegeuka kuwa tishio kubwa kwa wanadamu wenzake kuliko hata simba na nyati.
!

03/01/2024
Wavivu wa akili hawathamini maarifa. Wanadharau kujifunza vitu vipya. Hawaoni thamani ya kusoma vitabu, kuhudhuria semin...
02/01/2024

Wavivu wa akili hawathamini maarifa. Wanadharau kujifunza vitu vipya. Hawaoni thamani ya kusoma vitabu, kuhudhuria semina, kusikiliza videos na audios za kuelimisha na hamasa.
!

Mwanafalsafa wa kiyunani kwa jila la Socrate alisema kitu cha muhimu katika maisha ya mtu ni "Kujitambua au Kijijua mwen...
02/01/2024

Mwanafalsafa wa kiyunani kwa jila la Socrate alisema kitu cha muhimu katika maisha ya mtu ni "Kujitambua au Kijijua mwenyewe." Daima alisema ugunduzi mkubwa zaidi katika maisha haya ni ule wa kujijua. Alisisitiza "Know thyself."
!

Address

Migombani
Morogoro

Opening Hours

Monday 08:00 - 01:30
Tuesday 08:00 - 01:30
Wednesday 08:00 - 01:30
Thursday 08:00 - 01:30
Friday 08:00 - 01:30
Saturday 08:00 - 01:30

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Daniel Masubo posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The School

Send a message to Daniel Masubo:

Shortcuts

Share

Category