Walter Moses Mrisha

Walter Moses Mrisha Mfuasi wa Yesu Kristo
Disciple of Jesus Christ

Mwalimu & Mwinjilisti
Teacher & Evangelist

KANUNI ZA MAISHA KATIKA KUWAJIBIKA MBELE ZA MUNGU (Lk. 11:9-10)1. Kupewa kwa kuomba2. Kupata kwa kutafuta3. Kufunguliwa ...
14/09/2024

KANUNI ZA MAISHA KATIKA KUWAJIBIKA MBELE ZA MUNGU (Lk. 11:9-10)
1. Kupewa kwa kuomba
2. Kupata kwa kutafuta
3. Kufunguliwa kwa kubisha

1. Usipoona matokeo ya maombi yako, chunguza wapi maombi yako
2. Maombi ni mawasiliano yanayotengeneza mahusiano ya mtu na Mungu.
3. Boresha mahusiano hayo kwa kuwasiliana na Mungu kwa njia ya maombi.
4. Maombi hujenga mahusiano baina ya mwanadamu na Mungu. Maombi ni kiungo, ni daraja la kumfikia Mungu.
5. Usichoke maombi kwakuwa ukiacha adui atapanda uharibifu ndani ya maisha yako (Mt. 13:25)
6. Huu ni wakati ambao Mungu amekupa ili uweze kumtafuta kwa bidii kwakuwa utamwona. (Yak. 4:8)
7. Unahitaji kuwa na nguvu ili kupata mambo yaliyoko katika Ufalme wa Mungu (Mt. 11:12) kwa Kusoma Neno, Kuomba, Utakatifu na kuishi katika haki.
8. Faida ya kutafuta Ufalme wa Mungu kwanza ni kupata FURAHA, AMANI NA MEMA (Rum. 14:17)

MAMBO YANAYOZUIA MAOMBI YASIJIBIWE
1. Kutokuomba kwa bidii
2. Kuomba kinyume na mapenzi ya Mungu (Yak. 4:3)
3. Dhambi/Uovu (Yh. 9:31)
4. Mazuio ya Ufalme wa Giza (Dan. 10:12)

MAMBO YA MUHIMU KUTAFUTA/VIPAUMBELE
1. Ufalme wa Mungu na haki yake (Mt. 6:33-34; Rum. 14:17-18)
2. Uso wa Bwana (Zab. 105:4)
3. Unyenyekevu (Sef. 2:3)
4. Kuwa na amani na watu wote (Ebr. 12:14)

Karibu Ibada leo kwanzia saa Tatu kamili asubuhi, Tegeta Dar es Salaam
08/09/2024

Karibu Ibada leo kwanzia saa Tatu kamili asubuhi, Tegeta Dar es Salaam

HUKUMU YA MILELE KWA KILA MTU.1. Usiangalie nyuma, usiangalie waovu wa dunia hii na kuwaiga. Usikumbuke uovu uliokuwa um...
04/09/2024

HUKUMU YA MILELE KWA KILA MTU.

1. Usiangalie nyuma, usiangalie waovu wa dunia hii na kuwaiga. Usikumbuke uovu uliokuwa umefanya nyuma na kuurudia. Songa mbele katika wokovu wako.
2. Weka bidii katika kusoma Neno la Mungu, Maombi, na Ibada ili siku ile isije ikakukuta hujajitayarisha.
3. Bado una nafasi ya kutubu na kutengeneza. Itumie nafasi hii vyema, usiichezee.
4. Tumia wakati huu kumtafuta Mungu kwa bidii kwamaana siku ya hukumu ikifika, hutakuwa na nafasi tena.
5. HAKIKISHA jina lako limeandikwa katika kitabu cha uzima mbinguni kabla ya siku ya hukumu.
6. Jichunguze maisha yako kila siku ili ujirekebishe mapema kabla ya kufika siku ile ya HUKUMU!
7. Tofauti na mahakimu wa dunia hii, wanaopendelea na kuhumu pasipo haki, siku ya hukumu Mungu atahukumu kwa HAKI.
8. Maisha yako sasa ndiyo yatakayoamua utakapoelekea katika siku ya hukumu.

https://www.youtube.com/live/O-07rrjqglM?si=M5O4nudHz2aOHRJx

Kwa wewe ambaye hujakwenda Kanisani, unaperuzi tuu huku mtandaoni, usiperuzi bure. Ungana nasi katika ibada LIVE. Karibu...
04/08/2024

Kwa wewe ambaye hujakwenda Kanisani, unaperuzi tuu huku mtandaoni, usiperuzi bure. Ungana nasi katika ibada LIVE. Karibu!

KARIBU KATIKA IBADA YA SIKU YA LEO KWA MAWASILIANO ZAIDI, 0673081038

MAMBO MUHIMU NILIYOJIFUNZA LEO1. Unapokutana na hofu ya kifo, OMBA AMANI YA BWANA ndani yako.2. TAMBUA: Mungu amekuacha ...
28/07/2024

MAMBO MUHIMU NILIYOJIFUNZA LEO
1. Unapokutana na hofu ya kifo, OMBA AMANI YA BWANA ndani yako.
2. TAMBUA: Mungu amekuacha ubaki hapa duniani hata sasa ili ufanye kusudi alilokupa katika Ufalme wa Mungu.
3. Tumia nafasi uliyopewa duniani kutengeneza na Mungu ili kifo kikija, usikihofu
4. Kristo akikaa ndani yako kikamilifu, utaondolewa hofu ya kifo
5. Usiweke tumaini katika mwili wa asili kwakuwa mwisho wake huharibika na kupotea
6. Unapaswa kuogopa DHAMBI kuliko kifo.

MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA SOMO: MUNGU ATAKUDAI WATOTOMzazi ni mfano wa kuigwa kwa watoto, angalia mtoto wako anajifunza ...
07/07/2024

MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA SOMO: MUNGU ATAKUDAI WATOTO

Mzazi ni mfano wa kuigwa kwa watoto, angalia mtoto wako anajifunza nini kwako.

Usimnyime mtoto wako fimbo ya adhabu, kwakuwa ndiyo itakayoondoa ujinga moyoni mwake.

Weka akiba kwa ajili ya watoto wako

Jifunze kuwasamehe watoto wako. Usiwalaani watoto wako kutokana na makosa yao

Wafundishe watoto wako ubatizo sahihi Kibiblia, ili wawe tayari wakati utakapofika.

Wafundishe watoto kuwa mafanikio yako yanatokana na Mungu.

Wafundishe watoto wako kwa bidii Neno la Mungu kila siku, asubuhi na jioni.

Mheshimu Mungu kuliko kuwaheshimu watoto wako, ili watoto wako wajifunze kumheshimu Mungu.

ONYA WATOTO WAKO.
KEMEA WATOTO wafanyapo makosa, ili wajilinde wasifanye makosa.

Waweke wakfu watoto wako wote kwa BWANA, ili Mungu awaongoze na kuwakinga dhidi ya tabia za kishetani.

Fundisha watoto wako njia za Mungu tangu wakiwa mdogo kwakuwa zitadumu katika maisha yake yote.

Maisha ya wazazi kabla, wakati na baada ya kuzaa watoto yanamadhara makubwa kwa watoto wao.

Hakikisha unafanya ibada kila siku nyumbani kwako asubuhi na jioni. OMBEA WATOTO WAKO KILA SIKU.

Kuwa makini kwakuwa shetani ametapanya roho chafu kupitia tv, shuleni na mtaani ili kuwadaka watoto wako kusudi wapotee.

Usipowekeza elimu ya Mungu kwa watoto wako, Shetani atawekeza elimu ya duniani/kuzimu kwake.

Wekeza kwa bidii elimu ya Mungu kwa watoto wako. Usiwe 'busy' na kazi zaidi ya hili.

Utapata faida katika vitu uvifanyavyo ikiwa Mungu pekee ndiye anayekuongoza.

Utapa faida katika watoto unaowalea si kwa kuwapa elimu ya duniani pekee bali kwa elimu ya Mungu.

05/06/2024


Usipokee Ushauri kutoka kwa mtu asiye mcha Mungu

Nimejifunza, niliposoma Mit. 11:9, kuwa utapotea ikiwa utapokea ushauri kutoka kwa mtu ambaye hana hofu ya Mungu.

Jizungushie watu wawili ama watatu wenye hofu ya Mungu ambao hao watakushauri.

‭Mit 11:9 SUV‬
[9] Asiyemcha Mungu humpoteza jirani yake kwa kinywa chake; Bali wenye haki watapona kwa maarifa.

6. UKIMDHARAU MZAZI WAKO KWASABABU YA UDHAIFU WAKE, UNAPATA LAANA MOJA KWA MOJA (Mwa. 9:22-27)Wazazi wanakosea k**a wana...
03/01/2023

6. UKIMDHARAU MZAZI WAKO KWASABABU YA UDHAIFU WAKE, UNAPATA LAANA MOJA KWA MOJA (Mwa. 9:22-27)

Wazazi wanakosea k**a wanadamu wengine, kwakuwa nao wana udhaifu wa kibinadamu, kwani wote tunafanya dhambi na kupungukiwa utukufu wa Mungu. Lakini kamwe usijechukua udhaifu na mapungufu ya mzazi wako k**a sehemu ya kumdharau au kumzalilisha au kumsema kwa watu wengine vibaya. Hii itakupa laana ya ‘automatic’ au moja kwa moja ya kufanyika kuwa mtumwa kwa watu wengine. Hii itasababisha ukwame hata kwenye maisha yako. Ndiyo maana Mungu anasema waheshimu baba yako na mama yako ili siku zako ziwe nyingi na za heri katika nchi upewayo na Bwana Mungu wako. Usipowaheshimu, basi hizo siku zako zitakuwa chache na zenye laana badala ya Baraka.

Wazazi wana nguvu waliyowekewa na Mungu ambayo wanaweza kuitumia kukubariki au kukulaana na Baraka au laana hiyo ikafika, hata k**a huyo mzazi hamwamini Mungu. hivyo mpendwa, chunga sana namna unavyoishi na wazazi wako. Waheshimu Zaidi ya ulivyokuwa unafanya mwanzo, wajali sana na kamwe usije ukawadharau.

Kumbuka Kristo aliwaheshimu wazazi wake na kuwatii (Lk. 2:51). Ikiwa Kristo aliye mwana wa Mungu alitii wazazi wake, ingawa pasipo yeye, hata Mariamu na Yosefu wasingekuwepo duniani, wewe je, si unapaswa kuwatii Zaidi. Yeye mwumbaji wa vyote alipovaa mwili na damu, alijitiisha na kujinyenyekesha kwa wazazi wake, wala hakujiona mkuu kuliko wao; basi imekupasa wewe nawe uwe na utiifu Zaidi ikiwa unamwita Kristo kuwa ni Bwana na mwokozi wako.

Address

Kilimanjaro

Telephone

+255714766148

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Walter Moses Mrisha posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The School

Send a message to Walter Moses Mrisha:

Shortcuts

Share

Category