04/02/2026
MAANDAMANO YA AMANI BAADA YA USHINDI WA F4 NAMBA 3 KITAIFA 2025
Ndugu wazazi na walezi, viongozi wa serikali na wa chama, walimu wenzangu, wanafunzi wapendwa, wageni waalikwa, na wananchi wote wa wilaya ya kibondo na maeneo jirani BWANA YESU ASIFIWE :
Kwanza kabisa, napenda kumshukuru Mungu kwa kutuwezesha kufika siku hii ya furaha na fahari kubwa. siku ya jumamosi tutakuwa na maandamano ya kuuzunguuka mji wa KIBONDO Leo kusherehekea ushindi mkubwa wa Shule ya Sekondari Ahava, ambayo imefanikiwa kupata nafasi ya TATU KITAIFA. Huu ni ushindi wa kihistoria, si kwa shule yetu tu, bali kwa wilaya ya Kibondo, Mkoa wa Kigoma, na Taifa kwa ujumla.
Ushindi huu haukuja kwa bahati mbaya. Umetokana na juhudi, nidhamu, kujituma, na mshikamano wa wadau wote wa elimu.
Nawapongeza sana wanafunzi wetu kwa bidii yenu, uvumilivu, na kuamini kuwa inawezekana kufika mbali hata ukiwa Kibondo.
Hakika Mmeonyesha kuwa ndoto haina mipaka.
Nawashukuru kwa dhati walimu wetu kwa kazi kubwa ya kufundisha kwa moyo, kufuatilia maendeleo ya wanafunzi, na kujitoa mchana na usiku. Nyinyi ni nguzo ya mafanikio haya.
Pia nawapongeza wazazi na walezi kwa ushirikiano wenu, malezi bora, na kuunga mkono jitihada za shule.
Shukrani za pekee ziende kwa mkurugenzi wa shule yetu MCH MAILIDI JUMA , kwa kuweka mazingira mazuri ya elimu. Msaada wa kiroho , miundombinu, vitabu, sera na miongozo umechangia kwa kiasi kikubwa mafanikio haya.
Zaidi shukurani zangu ziende kwa serikali kuanzia ngazi ya wilaya ,mkoa hadi taifa kwa ushirikiano wenu na shule yetu ulio chanya ambao ndio sababuya mafanikio haya :
Ndugu zangu, ushindi huu ni mwanzo, si mwisho. Unatupa changamoto ya kufanya vizuri zaidi. Tunajipanga kuhakikisha tunadumisha viwango vya juu vya taaluma, maadili, na nidhamu ili Ahava Secondary School iendelee kung’ara zaidi kitaifa na kimataifa.
Kwa pamoja, tuendelee kushirikiana, tuilinde shule yetu, na tuijenge Kibondo yenye elimu bora.
Nawakaribisha wananchi wote kushiriki maandamano ya ushindi kwa amani, furaha, na nidhamu siku ya jumamosi ya tarehe 07/02/2026
MWISHO
Siku ya jumapili 08/02/2026 tutakuwa na ibada ya kumshukuru MUNGU WETU ALIYE TUWEZESHA KUFANYA HAYA YOTE ITAKAYOFANYIKA UKUMBI WA AHAVA SECONDARY.
Wafilipi 4:13
Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu.
MKUU WA SHULE AHAVA SEC