Jerry100 - Kiswahili

Jerry100 - Kiswahili Kiswahili Nguzo Maendelea kwa Jumuiya Itumiayo Lugha ya Kiswahili Natumai itawezekana.

Ukurasa huu ni muafaka kwa masuala yanayoandamana na Lugha ya Kiswahili (Swahili Language) kwa dhumuni la kuelezea changamozo zinazokabili lugha hii. Aidha, elimu kuhusu Kiswahili itajadiliwa, mijadala kuhusu utoshezi, ukubalifu, mukumo wa Kiswahili, na mengineyo kemkemu yatakuwa kichokoo katika ukurasa huu. Maono ni kuona Kiswahili kikiwa miongoni kwa lugha kadha zitakazobahatika kuwa lugha ya ku

tolea elimu katika mfumo wa elimu ya juu duniani. Ili kulifanikisha hili, hamasa juu ya matumizi ya Kiswahili, elimu ya kubadili fikra za watu kusudi wawe na fikra chanya juu ya lugha ya Kiswahili, uimarishaji ushirikishwaji wa wadau, nguvu ya serikali kurasimisha sheria zitakazoipa hadhi zaidi Kiswahili, ni kati ya njia tunazoamizi zikitekelezwa kwa ufasaha, dira au maono yatafikiwa ifikapo miaka ya karibuni ijayo (2030).

27/01/2026

Mbuzi wenye nyama safi, wanakula majani safi.

0693 987271

01/10/2024

Salamu wafuasi wangu wapya! Nina furaha kuwa nanyi! Ally Suleiman Msuya, Letisia Jakobo

Hapa ndugu Afande lazima alone umuhimu wa wazururaji 🤭🤭🤭
06/11/2023

Hapa ndugu Afande lazima alone umuhimu wa wazururaji 🤭🤭🤭

27/01/2023

Anaandika Alloyce Nyanda MTOZI

Nimemsikiliza Jana Lissu akiwa Temeke.

1.Lissu anafundisha Elimu ya kujitambua

2.Lissu anaingiza falsafa zake mioyoni

3.Anaingiza falsafa zake akilini

4.Anakulazimisha ujue Nini sababu ya wewe kushinda njaa,kukosa kazi,kutokuwa na pesa.

5.Lisu anafundisha ni nani chanzo cha umasikini

6.Lissu anafundisha na kuelekeza dhana halisi ya Haki na wajibu

7.Lissu anafundisha namna ya kusaliti Mifumo ya kinyonyaji

8.Lissu Anafundisha namna ya kufanya Mapinduzi dhidi ya walioko madarakani wanaosimamia mifumo Haramu

Lisu ananikumbusha hotuba ya Mwalimu Nyerere aliyoitoa 1969 akiwaeleza walimu wawafundishe vijana kuwa jeuri na wadadisi hasa kwa viongozi wanyonyaji.

Hotuba inaitwa the job of the teach is revolution. Tukaisome

K**a CCM watachagua njia ya kuchafua Kwa propaganda za Ushoga,watashangaa 2025 wanapenda mlima mrefu wa kuukabili upinzani.

Huku nje kwenye field
1.Kuna kundi kubwa la vijana haliijui kesho Wala Leo Yao,likihoji linajibiwa kihuni eti lihamie Burundi.

2.Kuna kundi Lina mtaji kiduchu,limejiajiri halafu linakumbana na makali ya Mazingira ya biashara na hayupo wa kulisemea.

3.Kuna kundi lipo kwenye ajira ambazo zinawaganya waishie kule chakula kilichopo na siyo wanachokitamani.

CCM wakiendelea kupokea taarifa za kudanganyana,2025 watahangaika sana na bahati mbaya sana wao wenyewe baadhi wanampinga Mama ambaye 2025 watake wasitake watagombea.

Alloyce Nyanda
Mtozi

14/12/2022

Morocco wameshaanza kupigwa k**a ngoma. K**a unashabikia waafrika weusi wa Ufaransa gonga like 😂😂😂😂

11/03/2021

Je, neno 'boresha' ni Kiswahili Sanifu au Fasaha?

Pamekuwa na matumizi makubwa ya neno 'boresha' katika mazungumzo ya kila siku kuanzia kwa watu wa kawaida, maafisa wa serikali, viongozi na vyombo vya habari. Ni jambo la kawaida kumsikia kiongozi fulani akisema: "Serikali imekusudia 'kuboresha' huduma za kijamii k**a vile maji, afya, umeme na kadhalika." Je, ni sahihi?

Kabla ya kuangalia usahihi wa neno hilo tutazame asili ya neno hilo. Ni wazi kuwa neno boresha linatokana na shina 'bora' ambalo kikategoria ni kivumishi. Vivumishi huweza kuunda vitenzi ikiwa itaonezewa kiambishi mwishoni. Kwa mfano:
fupi - fupi+sha
refu - refu+sha
Lakini itambulike kuwa si kila kivumishi kinaweza kuongezewa viambishi, mojawapo ni neno 'bora' ambalo huambikwa kiambishi -esh- ili kuunda neno 'boresha', yaani bor+esh+a. Si sahihi. Bora ni bora.

Lakini, ukitazama nia ya wazungumzaji wanalinyumbua neno 'bora' na kuwa 'boresha' kuwa mbadala wa neno la Kiingereza, 'improve'. Hapa matumizi sahihi ni kutumia neno 'imarisha' au 'kuimarisha. Kwa mfano: "serikali imekusudia kuimarisha huduma za kijamii."

kutoa maoni yako kuhusu mada hii.

21/01/2021

Msemo wa "Kwio hiyo kwio."

Msemo huo ni maarufu sana Jijini Dar es Salaam. Msemo huo ulianza kupata umaarufu baada ya kutumika katika wimbo wa mwanasingeli Meja Kunta aliyeshirikiana na mwanabongo fleva aitwaye Lava Lava.

Msemo wa "kwio" au "kwio hiyo kwio" umetokana na mlio wa kuku "kishingo" ukipewa maana ya "kudharau na kupuuza jambo unaloelezwa au kutokubaliana nalo". Kwa mfano:
MTU 1: Ndugu, yangu nimenunua gari.
MTU 2: gari hilo kwio!

Msemo huo unaenda sambamba na msemo mwingine uitwao "kudanga" ukiwa na maana ya kuchepuka kimapenzi kufanya ngono na wapenzi tofauti kwa maslahi au makusudio anayojua mhusika. Ni wazi kuwa misemo hii imepata umaarufu sana kipindi cha mwaka mmoja tu uliopita.

Hata hivyo msemo huo wa "kwio" umeonekana kumkera zaidi Mh. Makamu wa Rais wa JMT, mama Samia na kutaka mabaraza ya kiswahili kushughulikia hilo. Je, yupo sawa? Si sahihi, kwa nini?

Lugha ni zao la jamii, na lugha moja huwa na vilugha ndani mwake k**a vile: msimu, rejesta, lahaja, kitabaka, kibinafsi na lugha rasmi. Kila kilugha huwa na wazangumzaji wake kutokana na mazingira husika. Hivyo kusema kilugha fulani kisitumike maana yake umesema hiyo jamii itoweshwe duniani au jamii fulani isiwepo. Kwa hiyo hata msemo huo "kwio" ukipigwa marufuku hautaweza kuzuia jamii husika kutumia au kuibua misemo (misimu) mipya. Kazi ya mabaraza ni kuchunguza misemo (maneno) hiyo na kuona k**a itafaa kurasimishwa. Yapo maneno mengi yaliyotokana na misimu k**a ilivyo leo neno la "kwio" na baada ya kudumu kwa muda mrefu yakapata kuhalalishwa, nayo ni:
Kasheshe
Mchakato (neno la kubuni)
Kupe
Beberu au bepari
Ngangari
Mkereketwa, n.k.

Hivyo misimu haizuiliki, ukitaka kuizuia basi fisha jamii yote, pasiwepo mtu.

Kiswahili na Lugha za KiafrikaNi wazi kuwa Kiswahili kimeimarika na kimeenea vya kutosha. Si hivyo tu, hadhi yake pia in...
30/12/2020

Kiswahili na Lugha za Kiafrika

Ni wazi kuwa Kiswahili kimeimarika na kimeenea vya kutosha. Si hivyo tu, hadhi yake pia inaendelea kukubalika.

Kuimarika kwa Kiswahili inatokana na kujitosheleza kwake katika kutimiza kikamilifu mahitaji ya kijamii na kitaifa na katika nyanja mbalimbali. Swali kuu linalobaki ni kwamba: kwa nini na kuimarika kwake lakini serikali haioni haja ya kuipa Kiswahili dhima ya kutumika katika ufundishaji katika mfumo wa elimu ya juu (Sekondari na Vyuo ama vyuo vikuu)?

Yote ya yote Kiswahili kimeimarika, pamoja na mambo mengine, lugha za Kiafrika (lugha za kibantu na zosizo za kibantu) zimekifanya kiswahili kuimarika kimsamiati na kiistilahi. Hii inaonesha kwamba kuimarika kwa kila kilicho cha Mwafrika si lazima itegemee mambo ya nje (ughaibuni) bali kwa waafrika wenyewe. Hivyo tuzipe heshima lugha hizi za kiafrika pale tunapokisifu Kiswahili.

Tazama mifano michache ya msamiati kutoka lugha za kiafrika kwenye lugha ya Kiswahili:*

Sinovial fluid: Ugiligili (Kinyakyusa)
Bone marrow: Uloto (Kizaramo)
Faculty: Kitivo (Kipare)
Landslide: Ngoko (Kichagga)
State house: Ikulu (Kinyamwezi)
Parliament: Bunge (Kiganda)
Soil texture: Unamu (Kigogo)
Duodenum: Mbuti (Kimasai)
Lung fish: Kamongo (Kijaluo)
Blank verse: Sukui (Kisusu-Guinea)
Griot: Yeli (Kimaninka-Guinea)
Ballad: Rala (Kiyoruba-Nigeria)
Kola nut: Kola (Lugha za Afrika Magharibi).

*Baraza la Kiswahili Tanzania (1994). "Mwongozo kwa Waandishi wa Kiswahili Sanifu." Dar es Salaam: Dar es Salaam University Press.

27/12/2020
24/12/2020

Lugha ya Kiswahili kuhusu Ulemavu

Lugha ni zao la jamii ikiwa na maana hubeba mitazamo anuwai ya jamii husika. Kwa kupitia lugha tunaweza kuona si tu muundo wa jamii ulivyo (kitabaka) bali pia namna jamiilugha inavyofikiri kuhusu ulimwengu.

Hivi basi, kwa kupitia lugha ya kiswahili tunaweza kujua mtazamo wa waswahili kuhusu ulemavu, hasa tukichunguza nahau na methali.

Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na Sudy (2013)* kwa kupitia ushahidi wa lugha ya kiswahili, ni wazi kuwa jamii ya watumia Kiswahili wana mtazamo hasi kuhusu watu wenye ulemavu. Kwa kuthibitisha hilo anatoa mifano ifuatayo watu wenye ulemavu wa macho (kipofu): "kipofu hamwelekezi kipofu mwingine kwa mwenge". Lakini pia kuna methali ambayo inahusu ulemavu wa kutosikia (kiziwi): "kumwimbia kiziwi ni kumaliza nyimbo." Pia kuna methali inayoonesha kunyanyapaa wakemavu wa viungo: "Agana na nyonga kabla ya kuruka."

Kwa kutumia mifano hiyo michache inaonesha kuwa jamiilugha (Waswahili na au watumia Kiswahili) wana mtazamo hasi kuhusu walemavu kwa kutumia kipengele cha lugha.

*Sudy, F. N. (2013). "Evaluation of Effectiveness of Primary Education Development Program on Enhancement of Inclusive Education for Children with Hearing and Visual Disabilities in Tanzania." Dar es Salaam: OUT.

21/12/2020

Dhanna ya Ubantu

Hakika, wanafunzi wengi wa sekondari na vyuo (kwa wanaosomea lugha ya Kiswahili) wamefahamikiwa kujua neno "ubantu" au "wabantu" hususan katika kudhannaisha uasilia wa lugha ya Kiswahili. Je, ni kweli kuna ubantu au kuna jamii inaitwa ubantu? Hakika, hakuna; ingawa wengi wanafahamu kuwa kuna wabantu. Si makosa yao bali ni makosa ya mitaala yetu au na silabasi zetu.

Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na Profesa James Mdee wa Chuo Kikuu Huria, hakuna watu wanaoitwa wabantu. Neno "bantu" lilibuniwa na mwanaisimu* Dakt. W. H. I. Bleek ambaye alifanya utafiti wa lugha za Afrika kusini mwa Sahara na kugundua kuwa lugha nyingi kusini mwa ikweta zinafanana kuwa zilikuwa za mbari au kikoa kimoja. Baada ya uchunguzi wa muda mrefu (case study) alibaini kuwa katika lugha nyingi neno 'ntu' au kibadala chake 'ndu' lilikuwa linajitokeza kwa maana ya 'mtu'. Katika lugha hizo neno 'ntu' kwa maana ya 'mtu na 'bantu' kwa maana ya 'watu' lina umbo linalokaribiana ila kwa tofauti ndogondogo za kifonolojia (kimatamshi). Kwa mfano:
Kiswahili: m-tu (u*), wa-tu (w*)
Kipare: m-ntu (u), bha-ntu (w)
Kichaga: m-ndu (u), wa-ndu (w)

Basi, kutokana na neno 'ntu' na wingi wake 'bhantu' ikiwa ina maana ya 'mtu' na 'watu' kwa mfuatano huo, Dakt. Bleek aliwaita wazungumzaji wote wa lugha hizi kuwa ni "wabantu'. Jina hili ni la jumla kwa jamii na si jamii yoyote mahususi. Ni kutokana na hali hiyo pia hakuna lugha inayoitwa kibantu.

*mwanaisimu - mtaalamu wa lugha
*u - umoja
*w - wingi.

Address

Kariakoo

Telephone

+255 712 113 939

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Jerry100 - Kiswahili posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The School

Send a message to Jerry100 - Kiswahili:

Shortcuts

Share

Category