Tosamaganga High School Alumni

Tosamaganga High School Alumni Ukurasa huu ni maalumu kwa ajili ya wadau kupata taarifa kuhusu shule ya Tosamaganga na mikakati ya "alumni" wake kuboresha Taaluma na miundo mbinu

02/06/2024

YANGA BINGWA TENA

20/06/2023
25/11/2019

To manage and secure projects.
To make sure projects are being completed in specified specifications and standards

SHEREHE YA KUKUTANA PAMOJA WANAFUNZI WALIOSOMA TOSAMAGANGA.Wanafunzi waliosoma Tosamaganga wanapanga kukutana kwa pamoja...
10/04/2019

SHEREHE YA KUKUTANA PAMOJA WANAFUNZI WALIOSOMA TOSAMAGANGA.

Wanafunzi waliosoma Tosamaganga wanapanga kukutana kwa pamoja mnamo tarehe 29/06/2109.

Pamoja na mambo mengi ni kutaka kuwafikia Alumni wengi zaidi. Kwa uchache wao hadi sasa wameweza kuchangisha takribani milioni 100 kwenye shughuli mbalimbali ikiwemo: Ujenzi wa vyoo vya kisasa, Kutoa Msaada Hospitali ya Ipamba, Kushiriki na kutoa michango kwenye misiba (Alumni, wazazi wao, wake na watoto) na kusaidia Alumni wagonjwa wenye uhutaji maalumu.

Kwa sasa wamejikita kwenye kutengeneza ICT lab na kuangazia kutatua changamoto nyingine.
HIVYO kwa pamoja wameamua kufanya sherehe itakayowakutanisha wanafunzi waliosoma Tosamaganga (TOSA BOYS REUNION 2019).

MCHANGO kwa ajili ya sherehe hiyo kima cha chini ni TZS 50,000/= itumwe kwenye namba ya Halopesa (0622 602 440 - Jina JAFARI SIMIKA).

Kwa maelezo zaidi na wale wanafunzi waliosoma Tosamaganga wanaotaka kujiunga na kundi la jumla (kubwa) la WhatsApp wasiliana na Dr. Stephen Biginagwa (0713 180 265) ili aweze kukuunga.
Mwerangi Iddy , Zitto Kabwe

18/03/2019

TOSAMAGANGA ALUMNI DIRECTORY 2019

Napenda nichukue fursa hii kuwajulisha kuwa tunaanza kuandaa saraka kwa ajili ya wana Alumni ili iwe rahisi kuwasiliana.
Kwa hiyo naomba mnitumie taarifa katika muundo huu hapa chini:

*Jina kamili*
*Tosamaganga O au A level?*
* Mchepuo “Combinations”*
*Taaluma yako*
*Mahala unapofanyia kazi*
*Mkoa unaoishi*
*Mawasiliano ya Simu*
*Barua pepe*

*MFANO*
👇🏾👇🏾👇🏾👇🏾

Prof. Baltazar Mlagara Lyamongo Namwata
Advanced Level, CBG (1994-1996)
Trainer, Researcher and Consultant at the Institute of Rural Development Planning, Dodoma Municipality, Dodoma Region
0784/0767/0622 588258
Email ni [email protected]

MUHIMU: Tuma taarifa hizo kwenda kwa Iddy MWERANGI (0620 111 000).

TANZIA TANZIA TANZIANdugu yetu Mwana TOSA Alumni Mhandisi Erick NYINGE (1996-1998) amefiwa na Baba yake Mzazi. Mazishi y...
06/04/2018

TANZIA TANZIA TANZIA

Ndugu yetu Mwana TOSA Alumni Mhandisi Erick NYINGE (1996-1998) amefiwa na Baba yake Mzazi.
Mazishi yatafanyika huko NJOMBE siku ya Jumamosi (07/04/2018).

K**a ilivyo ada yetu tunaombwa KUSHIRIKIANA kwa kutoa MICHANGO yetu ya RAMBIRAMBI Kwa Dr. Stephene BIGINAGWA 0713180265 (TIGOPESA).

Mwisho wa kukusanya rambi rambi k**a kundi ni kesho Jumamosi saa 5 asubuhi.
Ukipata taarifa hii mjulishe na Mwana Alumni mwengine.

11/03/2017
20/01/2017

WANA ALUMNI Habari?

NAPENDA KUWAKUMBUSHA tuna mambo makubwa matatu mbele yetu.

1. MSIBA wa mama yetu mpendwa.
Ndugu yetu Dr. Melkiory NGIDO amefiwa na Mama yake Mzazi. Kila mjumbe anatakiwa achangie walau kuanzia Tsh 20,000/=. Mnaweza kutoa zaidi. Leo Ijumaa wataaga mwili wa marehemu huko mitaa ya UKONGA Magereza.

TUMA mchango kwenda kwa (Gabriel MWAIKASU 0767 894515)

2. Suala la RASIMU YA KATIBA ya TOSAMAGANGA.

21st January 2017 ni mwisho wa kupokea maombi ya wadau mbali mbali kuhusu rasimu hiyo. Baada ya hapo k**ati itakutana kujadili na baadae kutoa "Final Draft version" itakayoenda kupitishwa 04th February 2017. Na baadae kusajiliwa rasmi.
Maelezo zaidi wasiliana na MWENYEKITI ( Isaack MBOMA - 0717 455 492)

3. HARUSI YA JOVIN MOSES

Kiijana wetu anatarajia kufunga ndoa 11 February 2017. Michango yote ya wana Alumni iwe imemfikia Lutengano WILLIAM (0756 094 309) kabla ya 31st January 2017.

WAJUMBE mnaombwa ushirikiano wenu wa hali na mali kwenye maswala hayo muhimu.

NB kuna wajumbe hawapo kwenye mitandao ya kijamii tusaidiane kuwafikishia TAARIFA

20th January 2017

HISTORIA ZA WANA ALUMNI: Zuberi Zitto KABWEJe wajua?Ni Godfrey HILUKA ndiye aliyemshawishi Mheshimiwa Zuberi Zitto Kabwe...
08/11/2016

HISTORIA ZA WANA ALUMNI: Zuberi Zitto KABWE

Je wajua?

Ni Godfrey HILUKA ndiye aliyemshawishi Mheshimiwa Zuberi Zitto Kabwe kuja kusoma Tosamaganga? Sababu kubwa shule ya Mazengo aliyokuwa anataka kuhamia ina tatizo la walimu wa Uchumi na miundombinu ya vyoo ni mibovu.

Moja ya sababu ya kuja Tosamaganga kipindi hicho miundo mbinu ya choo ilikuwa mizuri na kulikuwa na walimu wa kutosha.
Leo hii Alumni wa Tosamaganga wameungana kuhakikisha wanatudisha hadhi ya shule yao, wameanza na ujenzi wa vyoo, maarufu k**a "half mile"

Karibuni wana Tosamaganga tukamilishe mradi huu.

WANAFUNZI WALIOSOMA TOSAMAGANGA WAANZA MCHAKATO WA KUBORESHA SHULE YAO.Wanafunzi waliosoma Tosamaganga High School, wame...
02/11/2016

WANAFUNZI WALIOSOMA TOSAMAGANGA WAANZA MCHAKATO WA KUBORESHA SHULE YAO.

Wanafunzi waliosoma Tosamaganga High School, wameanza mchakato wa kuboresha shule yao.

Pichani chini: Ni ujenzi wa vyoo (maarufu k**a "halfmile"). Mradi utakaogharimu zaidi ya fedha za kitanzania milioni ishirini (20,000,000+). Huu ni mchango mkubwa sana. Michoro na ujenzi unasimamiwa na Alumni wenyewe.

Huu ni mwanzo wa safari ndefu ya kuifanya Tosamaganga kuwa shule ya mfano, kuna changamoto kadhaa zipo shuleni ikiwemo.
i) Matumizi ya nishati ya kuni kupikia
ii) Kuzuiwa kutumika kwa bweni la Mandela ambalo limeachwa lianguke.
iii) Ukosefu wa walimu hasa wa masomo ya Sayansi
iv) Kukosekana kwa vyoo, kufuatia uchakavu na kuanguka kwa vyoo vya zamani.
v) Mgogoro wa Ardhi, kati ya Wizara na Kanisa katoliki juu ya umiliki wa eneo hilo.
vi) kushuka kwa kiwango cha ufaulu wa watahiniwa
vii) Uchakavu wa miundo mbinu kwa ujumla.

Kwa kuwa tumedhamiria tutalienda moja baada ya jingine kuhakikisha shule hii inakuwa ya mfano.

Mweka Hazina wetu Dr. Erasto Mbugi ( +255 759 352504 MPesa: Jima Erasto Vedastus MBUGI ) anaendelea kukusanya michango. Pongezi za dhati kabisa kwa kazi nzuri anayofanya.

Kwa maelezo zaidi juu ya harakati hizi na kupata maelezo zaidi wasiliana na Danford Mbilinyi, tumemteua kuwa Mwenyekiti wetu na msemaji wa Alumni kwa sasa.

Shukran za pekee kwa Mnyitafu, Shack Noel, Maulilo KIPANYULA, Arch Yusuf, Kwame Lutangilo, Isaack Mboma Greyson Nyamoga na Eng Nickie M kwa kujitoa na kuhamasisha.

Tafadhali wa"tag" wanafunzi waliosoma Tosamaganga ili tushirikiane nao kwenye kuboresha shule yetu ili iweze kupanda kitaaluma.

Mungu Ibariki Tanzania, Mungu Ibariki Tosamaganga!!

| MWERANGI, Iddy |
| Tosamaganga PCB1 1996/1998 |

24/09/2016

MKUTANO WA ALUMNI UMEAHIRISHWA:

Mkutano uliokuwa ufanyike leo 24th September 2016, umeahirishwa kufuatia maombi ya wadau wa makundi mbali mbali walioomba tufanye jambo moja baada ya jingine.

Kwa sasa tumekubaliana tuendelee na kukusanya hela kwa ajili ya halfmile. Ambayo tunapambana ili kufikia lengo.

Ujenzi wa vyoo hivyo maarufu k**a Halfmile utaanza rasmi tarehe 05th October 2016

Kwa hiyo tunaombwa kuendelea kutuma michango kwa MWEKA HAZINA WETU (Erasto MBUGI +255 759 352 504)

Tukifanikiwa kuanza ujenzi wa halfmile tunahamia kwenye kujadili na kupitisha suala la KATIBA ili kuturahisishia mfumo wa uendeshaji wa Alumni yetu.

Kila mtu akitimiza wajibu wake inawezekana.

VIVA TOSAMAGANGA....

Address

Tosamaganga
Iringa
026

Telephone

0713727373

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Tosamaganga High School Alumni posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share

Category