16/05/2026
Kwa kifupi sana;
Wanasayansi kutoka nchini Marekani wamefanya utafiti na kugundua kuwa mwisho wa dunia ni Novemba 2026. Utafiti k**a huo pia uliwahi kufanywa na Mwanafizikia Heinz von Forster mwaka 1960 na kupata majibu ya utafiti wake kuwa dunia itaisha muda wake Novemba 13, 2026.
Story nzima;
Mwaka 1960, mwanafizikia Heinz von Foerster alichapisha utabiri wa kisayansi uliotikisa wengi katika jarida la Science. Kupitia hesabu za ukuaji wa idadi ya watu duniani, alidai kuwa ifikapo Novemba 13, 2026, dunia ingeweza kukumbwa na “mwisho” au kuporomoka kwa ustaarabu wa binadamu.
Tofauti na unabii wa kawaida, utabiri huu haukutegemea imani za kishirikina bali ulitokana na ongezeko kubwa la watu na matumizi ya rasilimali za dunia.
Von Foerster alionya kuwa ikiwa ongezeko hilo lingeendelea bila kudhibitiwa, dunia ingeweza kukabiliwa na njaa, vita vya rasilimali, uharibifu wa mazingira, na migogoro mikubwa ya kijamii.
Ingawa wataalamu wa sasa wanabishana kuhusu usahihi wa tarehe hiyo, ujumbe wake bado una uzito mkubwa leo, hasa katika mjadala wa mabadiliko ya tabianchi, usalama wa chakula, na matumizi endelevu ya rasilimali.
Chanzo: Heinz von Foerster, Patricia Mora & Lawrence Amiot (1960), “Doomsday: Friday, 13 November, A.D. 2026”, Science.