16/06/2023
NACTVET kupitia Kurugenzi ya Udahili, Utahini na Utunuku imeendesha mafunzo ya siku mbili kwa maafisa mitihani wa kanda ya Kati na Kaskazini, kuanzia tarehe 15 na 16 Juni, 2023,Jijini Dodoma na Arusha.
Mafunzo hayo yamelenga kuwajengea uwezo Maafisa Mitihani wa Vyuo vya Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi ili kuwaongezea umahiri katika utendaji wa kazi zao. Mafunzo pia yalilenga kutatua changamoto mbalimbali zinazohusu uendeshaji wa mitihani.
Mkurugenzi wa Udahili, Utahini na Utunuku , Dkt. Marcelina Baitilwake, ameongoza mafunzo hayo akishirikiana na Meneja, Bw. Twaha Twaha na wakuu wa vitengo vya Kurugenzi hiyo.
Mafunzo hayo yameratibiwa kwa kuzingatia kanda na Bodi za Masomo.
Mafunzo k**a hayo yanatarajiwa kufanyika katika kanda ya Mashariki mwishoni mwa mwezi Juni, 2023 na baadae kwenye kanda zilizobaki.