05/04/2023
Fahamu Kuhusu Sababu Ambazo Huathiri Fikra Za Binadamu...
Jambo la kwanza unalopaswa kujua ni kwamba hivyo ulivyo ni matokeo ya Fikra zako mwenyewe. Pia, unatakiwa kujua kwamba maisha ya kila binadamu ni matokeo ya fikra zake mwenyewe...
Ukiachilia mbali hilo unatakiwa kujua kwamba unaona dunia na vitu vilivyomo kutokana na wewe ulivyo, na siyo jinsi dunia na vitu vyote vilivyomo vilivyo!
Kadhalika, unaipa dunia na vitu vyote vilivyomo tafsiri fulani siyo kwamba vinastahili kupewa tafsiri hiyo, ila ni kutokana na wewe ulivyojipa tafsiri...
Hii inamaanisha kwamba unatizama vitu kwa angle ya Fikra zako na siyo kwa angle ya vitu hivyo k**a vilivyo!
Unachotakiwa kuchukua hapa ni kwamba, fikra zimewaweka watu wengi kwenye ukomo, uhaba na mateso pamoja na kuwafanya watu hao wawe wazito katika kuchukua maamuzi hali ambayo inawafanya wapige hatua ndogo kimaisha...
Hata hivyo unatakiwa kujua kwamba huwezi ukaenda Mbali ya zaidi ya pale ulipoishia kujiona!
Mbali na hilo unatakiwa kujua kwamba duniani hakuna vikwazo halisi zaidi ya vikwazo unavyojiwekea mwenyewe kupitia mtindo wako wa kufikiri!
Hivyo basi ukitaka kubadili maisha yako anza kubadili fikra zako kwanza! Yaani change your thinking change your life!
Katika makala hii fupi utajifunza sababu ambazo Huathiri Fikra Za Binadamu...
Hauhitaji kufanya mengi chukua kiti Kaa then relax, k**a una soda na popcorn zichukue then anza kula na kunywa huku ukishushia na content makini sana kuwahi kuandikwa....
Hata hivyo zifuatazo ni sababu hizo:
1. Historia ya Malezi...
Kuna watu wameathirika kifikra kutokana na athari za malezi...
Na hii ni kutokana na manyanyaso, kukemewa, kudharauliwa, kukosolewa sana, kauli za kukatishwa tamaa, kuitwa majina ya hovyo, kufananishwa na viumbe vya ajabu pamoja vipigo vya hapa na pale, watu wengi wamejikuta wakitengeneza fikra za kuona hawastahili na hawawezi kufika popote pale!
Unatakiwa kujua kwamba historia yako imebeba mengi sana kuhusu maisha yako na ndiyo imekufanya uwe hivyo ulivyo!
Mbali na hilo kuna watu wanaamini kwamba hawawezi kufanikiwa eti kwa vile kwenye ukoo wanaotokea hakuna mtu aliyewahi kufanikiwa...
Pia kuna watu wengine utawakuta wakisema siwezi kufanikiwa kwa sababu niliambiwa mimi ni mjinga, nimezaliwa kwenye familia maskini, mimi ni mweusi, Mimi ni mfupi, familia yetu ina laana na mikosi n.k
Ndugu wakati uliokubalika ndiyo Sasa, unachopaswa kufanya ni kufuta fikra zote hizo hasi, ili kubadili kabisa historia ya maisha yako!
Unatakiwa kujua kwamba wewe unaweza na ulizaliwa ili uje uwe mtu mkuu, unayestahili uishi maisha yenye furaha, amani na mafanikio!
2. Mazingira.
Ni nguvu isiyoonekana ambayo humtawala binadamu kifikra, kimawazo, kitabia, kimienendo pamoja na kimtizamo!
Unatakiwa kujua kwamba unaweza ukawa na mawazo makubwa lakini k**a mazingira uliyopo siyo supportive hakuna cha maana utakachofanya.
Pia kuna baadhi ya watu wamekufa kifikra kwa sababu ya kuzungukwa na mazingira yaliyojaa uhaba na ukomo...
Mbali na hilo kuna watu wanajiona hawawezi, hawastahili, hawatafika popote pale na hawatabadili chochote kile kwa sababu mazingira waliyopo yamewafanya wawe hivyo!
Unatakiwa kujua kwamba mazingira yana Nguvu sana katika kupima kila kinachotokea maishani mwako!
Ukitaka kujua Nguvu ya mazingira fanya hili, mchukue papa Halafu muweke kwenye chumba kidogo, katika kukua kwake papa huyo hatakua mkubwa kuzidi chumba alichomo, ila mchukue papa huyohuyo halafu muweke kwenye bahari kubwa atakua mkubwa mpaka uatashangazwa...
Hii inamaanisha kwamba mazingira ya bahari hayajampa papa Ukomo wa kukua ukilinganisha na mazingira ya chumbani alimowekwa mara ya kwanza...
Ni wakati wa kuhama na kwenda kwenye mazingira mengine, k**a mazingira uliyopo siyo rafiki Kwako!
3. Watu wako wa karibu!
Kwa mujibu wa tafiti za kisaikolojia kuwahi kufanyika zimeonesha kwamba hivyo ulivyo ni wastani wa watu sita unaoshinda nao kila siku!
Hii inamaanisha kwamba k**a watu wako unaoshinda nao watakuwa ni waoga, hawajiamini, ni watu hasi, basi na wewe utakuwa k**a wao...
Hivyo unachopaswa kufanya ni kuepuka mazima kushinda na watu hasi kwani na wewe mwisho wa siku na wewe utajikuta unakuwa k**a wao!
Ndugu epuka kushinda saa zima na mtu wa kushinda naye dakika moja..
Epuka kushinda siku saba na mtu wa kushinda naye masaa saba..
Epuka kushinda 30 na mtu wa kushinda naye siku tatu...
Epuka kushinda siku 365 na mtu wa kushinda naye siku 30..
Epuka! Epuka! Epuka! Kwa usalama wa maisha yako!
Kumbuka watu wako wa karibu ni k**a ngazi! Kwamba wanaweza kukupandisha au kukushusha !
Daima chagua watu hawa kwa Makini ili uwe na fikra chanya..
4. Maono Yako..
Kuna watu wameathirika kifikra kutokana na kuwa maono hafifu. Maono ni nini labda? .... ndiyo upo sahihi maono ni picha kamili ya maisha yajayo ya mtu fulani.
Hii inamaanisha kwamba k**a hauna maono bado hujaanza kuishi... Na utaanza kuishi siku ukipata maono kuhusu maisha yako!
Watu wengi wanaishi lakini hawana picha kamili juu ya kile wanachotaka wakikamilishe maishani mwao...
Kutokana na hilo hujikuta wanaishi ili mradi tu wanaishi ila hakuna kitu cha maana wanachoyafanyia maisha yao.
Sasa k**a una maono hafifu utatoa wapi fikra nzuri?
Na utatengeneza fikra nzuri ili upate nini?
Ndugu ni huu ni wakati wa kutengeneza maono na kuanza kuyapigania!
5. Exposure!
Kuna watu wameathirika kifikra kwa Sababu exposure yao ni ndogo sana kwa watu!
Najua hujanielewa namaanisha hivi kuna watu wana uwezo wa kufanya mambo makubwa ila hawaoneshi watu wengine kile ambacho wanaweza kukifanya, kutokana na hilo wanaishia kujiona ni watu wa kawaida tu...
Huenda kuna mtu yupo anaangalia jumbe zangu hizi na anajua sana kuandika lakini haandiki, mtu huyo manake ana uwezo lakini hajiexpozi kwa watu...
Pia usiwe reluctant wa mazingira ongeza exposure yako kwa watu kwa kujaribu kufanya mambo mbalimbali katika mazingira tofauti tofauti!
Na huu ndiyo mwisho wa somo la leo!
Ndimi Emmanuel Samuel King'ung'e: mwandishi, muelimishaji katika eneo la maendeleo Binafsi, life coach and consultant!
Unaweza kuwasaliana nami kupitia Whatsapp no+255744284329