31/12/2025
UTAWALA WA SHERIA, HAURUHUSU VYOMBO VYA UCHUNGUZI NA MAHAKAMA, KUVUNJA HAKI ZA KIKATIBA NA SHERIA, KATIKA UTOAJI HUKUMU ZAKE (Kesi ya THADEY KWEKA)
Nimesoma HUKUMU ya Kesi ya THADEY KWEKA ambayo imetolewa jana kinyemela hata bila yeye mwenyewe kujitetea au kutetewa na Mawakili wake tangu kuk**atwa kwake, Ninasikitika Kuona kwamba hata Mahak**a kupitia Hakimu imejielekeza Vibaya Kutoa HUKUMU husika
Raia Wanategemea Mahak**a itende Haki na sio kushirikiana na Vyombo Vya Uk**ataji na Uchunguzi kuminya Haki za KIKATIBA za Mtuhumiwa k**a ambavyo nitaeleza Juu ya Sakata la THADEY KWEKA k**a nyaraka zinavyojifafanua, binafsi nitaandika kwa ufupi na straight to the point
Kitendo cha Ofisi ya DPP kufungua kesi dhidi ya Mtuhumiwa (Thadey Kweka) ya kuitaka Mahak**a kutoa Amri dhidi ya KWEKA ili atoe Nywila(Password) yake ili Polisi na Ofisi ya DPP kufanya Uchunguzi, na kesi Kusikilizwa na Mahak**a hata bila Mtuhumiwa kupewa wito ili kuwepo kwa utetezi au kutetewa na Wakili wake, Kunaibua maswali Mengi ya kisheria dhidi ya Vyombo Vya Uchunguzi pamoja na Mahak**a yenyewe
Mosi, Kesi umesikilizwa Upande mmoja kwa hati ya dharura bila mtuhumiwa wala Wakili wake kujulishwa kwa wito wa Mahak**a huku kesi iliyofunguliwa ikiwa Inter-Parte Application (Kwamba Mtuhumiwa alipaswa kupewa wito kwa utetezi) na sio Exparte Application (Kwamba kesi isikilizwe Upande mmoja kulingana na nyaraka zilizofailiwa
Ukisoma Wito wa Mahak**a( Chamber summons) hauonyeshi kwamba kesi hii ilikuwa ya Kusikilizwa Upande mmoja (Exparte Application) hivyo, Thadei alipaswa kuwakilishwa na Wakili au kujiwakilisha katika utetezi wake ili Kutekeleza Haki ya Asili ya Kusikilizwa inayolindwa na Katiba ya Nchi kabla ya Mahak**a Kuja na Uamuzi uliotolewa
Bahati Mbaya sana Hakimu aliyetoa Uamuzi anakili kwamba kesi hii ilikuwa kwa hati ya dharura ili isikilizwe Upande mmoja kinyume na nyaraka zilizowasilishwa Mahak**ani na Hakimu anaamua kesi husika bila kutii Katiba ya Nchi na Sheria zake k**a nitavyofafanua hapa;
Mahak**a hazina Mamlaka ya ku-dis regard Haki za Msingi za Kikatiba mathalani haki ya Faragha (Right to privacy) bila Kutoa Haki ya Kusikilizwa kwa Mtuhumiwa (Principle of Natural Justice) k**a ambavyo Hakimu alivyojielekeza vibaya katika Uamuzi wake unaopswa kukatiwa Rufaa haraka iwezekanavyo
Pia Kifungu cha 32 cha Sheria, Cyber Crime Act, licha ya kwamba Kifungu hiki kimeipa Mamlaka Mahak**a Kutoa Amri husika, Sheria husika haijaipa Mamlaka Kufanya Maamuzi kwa KUVUNJA Sheria na Katiba ya Nchi, hususani kukinzana na matakwa ya Katiba juu ya Haki ya Kusikilizwa (Fair hearing) kabla ya uamuzi
Ifahamike kuwa, Polisi na DPP hawezi Kumk**ata Mtuhumiwa kwa tuhuma hewa za jinai ( kupublish Taarifa za UONGO (False nformation) bila kuzitaja in specific k**a Kifungu cha 32 cha Sheria ya Cyber crime Act kinavyotaka
Ni Bahati mbaya sana Hakimu huyu wa Mahak**a(RMC) ametoa HUKUMU ya Amri ya Mtuhumiwa Kutoa nywila zake bila kujua ziitwazo Taarifa za UONGO ni zipi ambazo zilipelekea Mtuhumiwa kuk**atwa k**a Sheria inavyotaka
Ni takwa la Sheria zetu kwamba,Mahak**a katika Kutoa HUKUMU au Uamuzi wake haswa katika kesi ya Jinai inapaswa kuongozwa kanuni ya kuthibitisha bila Shaka (Prove Beyond Reasonable drought), kwenye hili Mahak**a imejielekeza Vibaya hivyo Uamuzi husika unapaswa kukatiwa Rufaa haraka
Hatuwezi tukawa na Mahak**a ambazo Hakimu anaamua kesi ya Jinai bila kujua in specific( details za kosa (criminal offence), bila kumpa Haki Mtuhumiwa kujitetea au kutetewa na Wakili wake (Fair hearing) na Kutoa Maamuzi
Hii ruling inapaswa kukatiwa Rufaa haraka, Ni Muhimu Mahak**a zetu kujiongoza vyema katika Kulinda Haki za Binadamu ambazo zinalundwa na Katiba ya Nchi yetu