Elizabeth David

Elizabeth David Mwalimu, Mwandishi na Mshauri Pokea mafundisho upate uzima

MAZURI YOTE ,MABAYA  YOTE, HUTOKA MOYONIMoyo wa mtu ni mdanganyifu , una ugonjwa wa kufisha.  Mawazo ya mwanadamu ni mab...
19/08/2026

MAZURI YOTE ,MABAYA YOTE, HUTOKA MOYONI

Moyo wa mtu ni mdanganyifu , una ugonjwa wa kufisha. Mawazo ya mwanadamu ni mabåya tangu utoto wake. Kinywa cha mtu huyanena yaujazayo moyo wake. Mtu mwema katika Akiba njema hutoa mema, bali mtu mbaya katika Akiba mbaya huta mabaya .
Kwa sababu hio hakuna mti mzuri unaotoa matunda mabaya, wala hakuna mti mbaya unaoweza kutoa matunda mazuri.
Ina maana k**a ukipanda maembe na kutarajia kupata ndizi, matarajio yako yatakuangusha. Ukipanda mti wa mpera utapata mapera. Utavuna kile ulichokipanda hio ni sheria ya kupanda. Muda nchi idumupo majira ya kupanda na mavuno , wakati wa baridi na wakati wa hari , wakati wa kaskazi na wakati wa k**i , mchana na usiku , havitakoma.
Yanayotoka katika mayo wako ndiyo hayo unayajenga , k**a ni kwenye mwamba au mchanga.
JINSI GANI UTATOKA HAPA?
1.Ingia katika upendo. Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nguvu zako zote na kwa akili yaka yote na kwa roho yako yote.
Na k**a unavyotaka watu wakutendee wewe, watendee vivyo hivyo. usiwaze mabaya juu ya jirani yako..
Usihukumu kwa kuona kwa macho ya damu na nyama. bali hukumu ya kweli inayotoka katika kweli.
Usimnyoshee mtu kidole, ondoa kwanza boriti iliyoko ndani yako, hapo ndipo utakapoona vema kukitoa kibanzi kilichopo katika jicho la ndugu yako..
2.EPUKA KUKAA BILA YA KUFANYA JAMBO , KUONGEZA UJUZI WA KAZI YAKO, KUSOMA VITABU MBALIMBALI.
K**a huna jambo la kufanya , hapo ndipo mawazo mengi huja ili kukufanya upotee kabisa. Utaanza kutazama watu, kuwahukumu, kuwabeza, kuwadharau. kwa nini ? Huna kitu cha kufanya.
Adui anatumia sana akili ya mtu ambayo iko wazi , isiyokuwa na cha kufanya. wakati mwingine mbele yaka kuna uchafu mwingi, nyumba yako ni chafu. Badala ya kuinuka ufanye kazi , utaanza kuita mfanyakazi afanye kitu ambacho kingekuwa ni faida kwako, lakini unamfaidisha mfanyakazi.
Mimi niligundua hiki, kila kitu mfanyakazi yupo atafanya n. kumbe unamwachia adui ili akuteke mawazo yako.
Maovu hutoka Moyoni kwa sababu, kabla hujafanya jambo lolote. Lazima lianzie huko ndani, katika fikra yako. Namaanisha, kabla hujatenda dhambi , uliwaza kwanza Moyoni mwako. Sasa hapa kuna wanaoshinda wachache. lakini wengi huishia kuwaza mabaya mabaya.
3.Soma neno la Mungu likae kwa wingi ndani yako ili likusaidie kujibishana na mawazo yako.
Mungu atusaidie sisi tuweze kuwaza k**a ambavyo anawaza Yeye.
Baba usitutie majaribuni, bali tuokoe na yule mwovu..

MAKWAZO YAMEANGUSHA WENGI.Umewabeba watu , umewatoa mahali pabaya, lakini kila siku ni kulalamika, kunung'unika,  ukiwaf...
15/08/2026

MAKWAZO YAMEANGUSHA WENGI.

Umewabeba watu , umewatoa mahali pabaya, lakini kila siku ni kulalamika, kunung'unika, ukiwafanyia jambo zuri , likipita tu wanasahau, wanaanza tena kukulalamikia na kunung'unika.
Musa katika kitabu cha Hesabu 20 yote ukisoma , hapo ndipo utaona kwa nini Musa na Haruni walikasirika hata wakasahau agizo la Mungu.
Mungu aliwaambia wakauambie mwamba mbele ya macho ya wana wa Israel utoe maji yake.
Lakini Musa alikasirika akainua mkono wake akaupiga ule mwamba kwa fimbo yake. mara mbili. maji yakatoka mengi.
Kuna mambo ambayo tunatakiwa kuwa makini tunapokuwa tunabeba watu, au kuwasaidia watu. Ukitazama kwa ndani hapa tunaona Musa alikasirika kutokana na tabia za hao watu aliokuwa anawaongoza.
ukirudi nyuma kidogo utaona jinsi gani walivyo mwangukia Mungu kwa ajili ya hao watu na malalamiko yao. Lakini Mungu akawapa haja yao kupitia maombi ya Kiongizi wao.
Njia za Mungu ni za ajabu mno. mawazo ya Mungu ni ya juu sana kuliko mawazo yetu.
Mungu anaweza akamhifadhi mtu au watu kwa kusudi lake litimie. hata k**a wanatenda mambo mabaya kiasi gani. ndio maana tunaambiwa usihukumu usije ukahukumiwa wewe. usimunyoshee mtu kidole, ukiwa umesimama angalia usije ukaanguka mwenyewe.
Mungu huwa anasubiri. maana ukienda mbele kidogo hapo KITABU CHA HESABU 21 hao hao ambao walitolewa maji, walianza tena kunung'unika, kwa Musa na Mungu kwa sababu ya njia mbaya , wakafa moyo tena. hapo ndipo Bwana Mungu alipotoa nyoka za moto. alitaka kuwajaribu k**a wapo wenye imani. watu wengi wakafa. lakini Musa alienda tena kuwaombea, ndipo Mungu akasema jifanyie nyoka wa shaba. ukamweke juu ya mti. kila mtu aliyeumwa akitazama huyo nyoka atapona.
Kumbuka Yesu alikuja akasema , makwazo hayana budi kuja lakini huna budi kuyashinda.
Watu hawa walikuwa na makwazo mengi. lakini ukiangalia hata leo , hata sasa kuna makwazo mengi kila mahali.
Yesu anakuambia huna budi kuyashinda. ili usikose taji yako uliyowekewa siku ya mwisho.

MWAMINI  MUNGU KILA KITU KINAKUJA KWA WAKATI.Haijalishi unapitia kitu gani kwa sasa, kila kitu kina wakati wake na majir...
12/08/2026

MWAMINI MUNGU KILA KITU KINAKUJA KWA WAKATI.

Haijalishi unapitia kitu gani kwa sasa, kila kitu kina wakati wake na majira yake.
hujapandishwa cheo?, biashara yako haina faida?, huduma yako haikui?, ugonjwa unakusumbua muda mrefu? maumivu yamekaa muda mrefu? Hujaoa au kuolewa? , unatafuta kupata mtoto ? USIOGOPE.
hata k**a unapitia wakati wa huzuni, tambua utakuja wakati wako wa furaha, amini tu, Tambua na kufahamu kuwa k**a kuna wakati wa kuzaliwa , kuna wakati wa kufa. k**a kuna wakati wa kupanda basi kuna wakati wa kuvuna , amini tu.
K**a kuna wakati wa Kubomoa , kuna wakati wa kujenga pia. wakati wa kucheka , pia uko wakati wa kulia. Usiogope unapopitia nyakati hizi.
Ndio kuna wakati wa kutupa mawe, lakini uko wakati wa kukusanya hayo mawe.
Kuna wakati wa kutafuta na upo wakati wa kupoteza . K**a kuna wakati wa kunyamaza , kuna wakati wa kusema pia. Kuna wakati mwingine utachukia, lakini utakuja wakati wa kupenda. Kuna amani nyingi , utakuja wakati wa vita. hata vikombe vikikaa kabatini vitagongana tu.
Kumbuka kuwa kila kitu, kila wakati na nyakati , Mungu amezifanya nzuri kwa wakati wake.
Ni vema k**a tukivumbua haya kuwa ni kazi yake Mungu ameifanya tangu mwanzo hadi mwisho wake. Muhubiri 3.
UNAPITIA NINI SASA?
Kumbuka kila kitu kina muda wa kuwepo na kina muda wake wa kuondoka. Kina mwanzo na kina mwisho wake.
Basi acha kujisumbua , kukosa amani, kufikiri sana, kuchanganyikiwa, bali katika kila neno, kila jambo, kila wakati, kila nyakati zinapotokea , OMBA, SALI, SHUKURU. NA HAJA YA MOYO WAKO IJULIKANE NA MUNGU.
Na amani ya Mungu ipitayo akili zote, itakuhifadhi moyo wako na nia yako katika Kristo Yesu.
Wafilipi 4.
Mwamini Mungu katika kila jambo unalopitia . Mtegemee Yeye, usichoke . Mkabidhi Yeye kila nyakati.
Mungu atusaidie. mwambie na rafiki yako na ndugu yako na wote uwapendao.
Yesu ni Bwana.

SITAKUPUNGUKIA WALA SITAKUACHA.Je si mimi niliyekuamuru? uwe hodari na moyo wa ushujaa; usiogope wala usifadhaike, kwa k...
07/08/2026

SITAKUPUNGUKIA WALA SITAKUACHA.

Je si mimi niliyekuamuru? uwe hodari na moyo wa ushujaa; usiogope wala usifadhaike, kwa kuwa Bwana Mungu wako, yu pamoja nawe kila uendako.
MATHAYO 6:25
Kwa sababu hio nawaambieni, msijisumbue maisha yenu , mle nini mvae nini. maisha je si zaidi ya chakula na mavazi?
Basi msisumbukie ya kesho, kwa kuwa kesho itajisumbukia yenyewe. yatosha kwa siku maovu yake.
WAFILIPI 4:6
Msijisumbue kwa neno lolote, bali katika kila neno , kwa kusali na kuomba pamoja na kushukuru. haja zenu zijulikane na Mungu.
Mungu wa mbinguni akupe macho a masikio ya ndani.
Usiogope amekushika kwa mkono wake wa kuume wenye nguvu.
AMINI TU.

NENO NI DAWA.Unaweza ukawa unafundishwa neno la uzima  , lakini halikuingii  moyoni mwako. , linapita tu sikio  moja na ...
06/08/2026

NENO NI DAWA.

Unaweza ukawa unafundishwa neno la uzima , lakini halikuingii moyoni mwako. , linapita tu sikio moja na kupitiliza sikio lingine. Lakini nataka nikuambie wewe unaesoma makala hii , endapo kuna mlima ume simama muda mrefu hautaki kuanguka, nakutia moyo endelea kujifunza . ipo siku utakutana na neno lako la kuangusha huo mlima.
Hakika Yesu ni daktari mkuu. Amini nakuambia, kumbuka yule mtu aliyelia , akasema NAAMINI, NISAIDIE KUTOAMINI KWANGU.
Leo ni iwe wewe mwambie Yesu kwamba unaamini.
Endelea kusoma Biblia, soma vitabu vya watumishi wa Mungu vinavyohusiano na mlima wako. usisome tu kitabu cha mafanikio, au cha kuvunja vunja, vya biashara, ndoa na vingine.
Hata katika kusoma kwako Biblia , tafuta maneno ambayo yanahusiana na mlima wako. Zipo Ahadi mbalimbali za Mungu.
Kuna za imani, uponyaji, mafanikio, fuaha, Upendo, matumaini. na zingine taja.
NAKUPA USHUHUDA WANGU.
Kuna kipindi nilikuwa na mlima mkubwa ambao ulisimama kwa muda mrefu sana. Nilikuwa tayari nimeokoka, kawaida lakini, sikuwa naelewa vizuri maana ya wokovu.
Lakini katika kutafuta nikakutana na ahadi ya Mungu juu yangu katika neno. Nilienda duka la vitabu kununua kitabu cha Tenzi za Rohoni. lakini nikaona kitabu juu kimechorwa mkate, kimeandikwa , NENO LA MUNGU NI MKATE WA UZIMA.
Nilikichukua hicho kitabu huku natetemeka, nilipofika nyumbani , nilijificha, nikaanza kukisoma mpaka nik**aliza. kilikuwa sio kikubwa sana. hapo ndipo mlima ulipoanza kuanguka taratibu mpaka ukapotea kabisa.
Mistari miwili tu ambayo iliingia moyoni ni hii.
WAEBRANIA 4:14-16
Basi iwapo tunaye kuhani mkuu aliyeingia katika Mbingu, Yesu, mwana wa Mungu, na tuyashike sana maungamo yetu. kwa kuwa hakuna kuhani mkuu asiyeweza kuchukuliana nasi katika mambo yetu ya udhaifu, bali Yeye alijaribiwa sawasawa na sisi katika mambo yote......
Halafu na Waebrania 10:23
Na mlishike sana ungamo la tumaini letu, lisigeuke; maana yeye aliyeahidi ni mwaminifu.
Basi kila mahali , niwe kwenye daladala, kwenye kazi, nyumbani, ninapolala, naimba ahadi. Sasa Hili ni agano nililokutana nalo mimi, ni tofauti na wewe. unaweza ukasoma hio mistari usielewe, na usipate maana halisi. lakini mimi nilifunuliwa hapo.
Hata nikasahau kabisa k**a kulikuwa na mlima.
Huo ni ushuhuda wangu. lakini ukiangalia mifano mingi na shuhuda nyingi ndani ya Biblia, Neno la Mungu, Yesu aliwaponya wengi na hata sasa , muda huu, anaponya.
Usikate tamaa, mkaribie Mungu na moyo wa kweli.
Naomba Mungu akusaidie. akufungue macho ya ndani, ya kuweza kukutana na Agano la uzima katika kila eneo la maisha yako.

KILA KITU NI NGUVU.  NA NGUVU N I KILA KITU.Toka enzi  za Yohana  mbatizaji hata sasa, Ufalme wa Mungu  hupatikana kwa n...
30/07/2026

KILA KITU NI NGUVU. NA NGUVU N I KILA KITU.

Toka enzi za Yohana mbatizaji hata sasa, Ufalme wa Mungu hupatikana kwa nguvu. na wenye nguvu waliuteka.
Mtu yeyote aliyefanikiwa ana nguvu. ukitaka kufanikiwa pata nguvu ya Mungu.
BALI UTAMKUMBUKA BWANA MUNGU WAKO , MAANA NDIYE AKUPAYE NGUVU ZA KUPATA UTAJIRI.
Ili alifanye imara Agano lake alilokuahidi. Yeye ndiye atakayekufundusha njia ya mafanikio ya kudumu yenye faida. atakuongoza katika njia ikupasayo kuifuata.

MUNGU NI WA AJABU.Kulikuwa na watu wawili  wameenda kusali, mmoja akawa anasema mimi Bwana natoa zaka , nafunga kila wik...
27/07/2026

MUNGU NI WA AJABU.

Kulikuwa na watu wawili wameenda kusali, mmoja akawa anasema mimi Bwana natoa zaka , nafunga kila wiki mara tatu, sio k**a huyu mtoza ushuru. Mungu akamwangalia tu. Lakini yule mtoza ushuru akawa anapigapiga kifua chake huku akilia na kuomba toba. Mungu alimsamehe na kumjibu maombi yake palepale. Usijihesabie haki. Kumbuka Mungu ni wa huruma. Mungu ni wa rehema kwa kila mtu amwendeae.
Umbea ulikuwepo tangu enzi za Yesu KRISTO.
Tuangalie hii hadithi huwa inanishangaza na kuniachia mshangao.
LUKA 13:1-17
Walikuwepo watu ambao walijiona wao hawana dhambi, ni wema lakini majibu ya Yesu yakawa tofauti na mawazo yao.
Maana inasemekana walikuwa wanampasha habari Yesu kuhusu wale watu ambao Pilato alichanganya damu zao na dhabihu zao.
Yesu akawaambia , hao watu hawakuwa na dhambi kuliko ninyi. angalieni msipotubu yatawarudia hayo yote. yaani na hao yatawapata k**a hao k**a wasipotubu.
TENA YESU AKAENDELEA KUWAAMBIA
Mnafikiri na wale kumi na wanane walioangukiowa na mnara huko siloamu ukawaua , mwadhani ya kwamba wao walikuwa wakosaji kuliko watu wote? nawaambia sivyo. lakini msipotubu kwa umbea wenu, yatawarudia nanyi mtaangamia vivyo hivyo.
BASI NDUGU ZANGU TUSIHUKUMU
Tuache kuwanyoshea watu vidole, Ni vizuri kusema yule ni mwenye dhambi sijui, anayejua ni Mungu.
Maana kipimo kile unachompimia mtu , ndicho utakachopimiwa.
Yesu alisema hivi,
Mbona wakitazama kibanzi kilicho ndani ya jicho la ndugu yako, na boriti iliyo ndani ya jicho lako mwenyewe huangalii?
akasema ,mnafiki wewe, itoe kwanza boriti katika jicho lako, ndipo utakapoona vema kukitoa kibanzi katika jicho la ndugu yako.
kasome taratibu utaona. mimi nimeruka ruka vipande.
Basi yoyote mtakayo mtendewe na watu, nanyi watendeeni vivyo hivyo.
Ndio maana nikasema hakika Mungu ni wa ajabu. siku zote yeye husimama katika haki. siku zote yeye ni wa rehema, ni wa huruma, fadhili zake ni za milele.
Mungu atusaidie.

USIAMINI KILA KITU UNACHOKUTANA NACHOBasi angalieni sana  jinsi mnavyoenenda ,  si k**a watu wasiokuwa na  hekima bali k...
27/07/2026

USIAMINI KILA KITU UNACHOKUTANA NACHO

Basi angalieni sana jinsi mnavyoenenda , si k**a watu wasiokuwa na hekima bali k**a watu wenye hekima, mkiukomboa wakati , kwa maana zamani hizi ni za uovu.
Tunafundishwa vitu vingi, tunaona vitu vingi, tunafikiri vitu vingi, na kutazama vitu vingi.
Kuna vitu vya k**ikia na kuviacha
kuna vitu vya kuangalia lakini usiyatie moyoni.
kuna mambo mengine ni ya kuzingatia , ili kuyafanyia kazi.
Kuna mengine ni ya kuchunguza kwanza.
Usibebe mizigo mingi, Kumbuka Yesu anasema hivi. Njooni kwangu ninyi nyote msumbukao na kulemewa na mizigo nami nitawapumzisha. Jitieni nira yangu mjifunze kwangu, kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo, nanyi mtapata raha nafsini mwenu.
Katika kila jambo , fanya kwa Jina la Yesu. kwa maana kwamba ni vizuri kumuuliza Mungu , Kuna nini hapa, Je? jambo hili linatoka kwako?, ni kwa ajili yangu?
Musa alimwambia Mungu , usipoenda nasi hatuwezi kutoka hapa.
Tunaona Daudi hakufanya jambo bila ya kuuliza, vita hii ikoje, nitashinda?
Wafalme wengi hawakwenda vitani bila ya kuuliza kwanza kwa Bwana. Lakini kila Mfalme ambaye alienda bila ya msaada wa Mungu , hakushinda vita ile.
Usiamini kila kitu unachokifikiria na kila unachokutana nacho, mambo ni mengi, ni vizuri k**a tuna uwezo wa kuchagua.
Mungu anasema, nimekuwekea leo uzima na mauti, nakushauri chagua uzima ili uishi.
Kila kitu ni cha kuchagua, usibebe bila ya kuchagua. ukienda sokoni chagua, ukienda dukani chagua, kila mahali chagua.
Maisha yatakuwa rahisi k**a tutachagua.
Mungu atusaidie k**ikia na kuangalia kutenda sawasawa katika Jina la Yesu.

AMANI YA MOYO Akili iliyotulia huyaweka maisha  katika usawa wake.Unapozingatia sana matokeo ya  nje , utakuwa unajitoa ...
23/07/2026

AMANI YA MOYO

Akili iliyotulia huyaweka maisha katika usawa wake.
Unapozingatia sana matokeo ya nje , utakuwa unajitoa mhanga kuharibu furaha yako ya ndani.
Linda furaha yako ya ndani , ambayo hio itakupa matokeo mazuri ya nje. mambo mengi yanaleta kutokuelewa na kuchanganyikiwa, kwa sababu ya matarajio uliyo nayo . lakini k**a hutakuwa na matarajio yalio nje ya uwezo wako vitu vitakuwa vinakwenda k**a kawaida bila kuchanganyikiwa.
Maisha hayana usawa hata kidogo. huhitaji kujaribu kujibadilisha, au kukua katika sekta mbalimbali za maisha yako. kwa sababu kila kitu , kila wakati vitu vinakua vyenyewe. ni kawaida . ukitaka kusukuma kitu unachokitaka kikue kwa muda wako, ndipo unapokaribisha msongo, kuchanganyikiwa na kukosa amani ya moyo.
Ishi maisha yako k**a vile unaangalia filamu. mahali ambapo huna msongo wa kujaribu kubadili hio filamu maana tayari imewekwa , lakini unafurahia kile kinachotokea wakati huo mbele yako. Haijalishi nini kitatokea katika hio filamu.
SABABU GANI INATUFANYA TUONE NI VIGUMU KUBADILIKA?
Sio kwa sababu hatufanyi bidii ya kutosha, bali ni kwa sababu tunaogopa kwamba endapo nitakifanya hiki kitu nini kitatokea?
TUMESHIKILIWA NA YALE YALIYOPITA.
Yamkini ulifanya jambo likaharibika, au uiliona mtu ameshindwa katika kitu kile kile ambacho unataka kukifanya.
Ndio maana wengi hatufiki mahali ambapo tunataka tufike leo.
Ni mawazo yetu na hofu iliyopo . Kitu kikubwa cha msingi ambacho Mungu alitushauri ni kuchagua .
Mungu atusaidie, unapofanya maamuzi, uchaguzi mzuri ili upate amani ya moyo wako.
Barikiwa , usiache kulike makala zangu na kushare kwa wengine.
onyesha upendo.

SELF FORGIVENESSIf you knew better, you would have done better. It is time to free yourself from the prison of the past ...
22/07/2026

SELF FORGIVENESS

If you knew better, you would have done better. It is time to free yourself from the prison of the past and the fear of the future. Can you forgive yourself for doing the best you could with what you had?

Address

Dar Es Salaam

Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00
Tuesday 09:00 - 17:00
Wednesday 09:00 - 17:00
Thursday 09:00 - 17:00
Friday 09:00 - 17:00

Telephone

+255756662631

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Elizabeth David posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share

Category