07/10/2024
UCHAMBUZI WA KINA WA MWAKA MMOJA WA VITA MPYA YA GAZA NA ISRAEL TANGU TAREHE 7 MWEZI WA 10 MWAKA 2023
UTANGULIZI
Naomba nianze na andiko hili kwa kunukuu moja ya hotuba ya katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ndugu Antonio Guterres, alioitoa mwaka jana 24/10/2023.
"It is important to also recognize the October 7 attacks by Hamas did not happen in a vacuum. That Palestinian people have been subjectad to 56 years of saffocating occupation"
"They have seen their land steadly devoured by settlement and plagued by violance, their economy stilied; their people displaced and their homes demolsihed. Their hopes for political soluton to plight have been vanishing"
Tafsir huru ya nukuu ya Gutterres, anaelezea ya kwamba.
Ni vema pia kutambua shambulizi la Hamas la October 7 halikutoea tuu k**a ombwe (halijaja bila sababu) ambapo kwa zaidi ya miaka 56 wapalestina wananyanyasika kwa kutokupumua kwa uvamizi unaofanywa kwa ardhi yao.
Wameshuhudia ardhi yao ikithibitiwa na kumezwa na wavamizi na wakichukua kwa mabavu, uchumi wao ukiibwa na watu wao wapalestina wakikosa makazi huku nyumba zao zikiharibiwa.
Matumaini yao yakisiasa kutatua hali zao mbaya yametoweka na hawana matumain tena.
NINI KILITOKEA OCTOBER 7?
October7 mwaka jana itakumbuka kwa waisrael na wapalestina na maeneo ya mashariki ya kati na dunia kwaujumla baada ya wanamgambo wa Hamas kuvamia Israel na kushambulia haswa sehemu mbali mbali za kambi za jeshi, makaz ya askari na maeneo mengine ya umma na raia na kuteka raia mbali mbali walokuwepo nchini humo.
Maelezo yanasema zaid ya wasirael 1,400 na vifo vya watoto zaid ya 20 waliuwawa kati shambulzi hilo, ambapo badae jeshi la Israel likatangaza vita Rasmi na Hamas kwa itawatokomeza wote na itadhibit upya ukanda wa Gaza, pia kuwarudisha mateka wote waliotekwa ambao ni zaid ya 130.
Ni mwaka sasa umepita ambapo Israel inafanya wanachsema vita dhidi ya Hamas, uko Gaza lakin hadi leo bado vita vinaendelea, bado hawajaithibid Gaza na bado hawajakomboa mateka wote, ambapo mateka waliowakomboa ni walifanya makubaliano 'prisoner swaps" na mmoja pekee ndo wamemuooa.
Mwaka mmoja wa vita ni wapelestina elfu 40 wamefariki uku watoto zaid ya elfu 18 wamefariki, sijasema wanawake na vikongwe, sasa sijaelewa k**a watoto tena vichanga na wazee vikongwe nao wanashika silaha pigana na Israel.
UHALISIA WA HII VTA
Uhalisia wa hii vita lazima turudi tuisome tena nukuu ya katibu mkuu Antonio Gutteres ambapo ndo uhalisia, ni mpumbavu pekee atatazama mgogoro huu kwa kutazama tarehe 7 tuu ya mwez wa 10, na akiacha tazama miaka 56 nyuma nini kilikuwepo.
Tuwe wawazi tuu, siungi mkono tukio la tarehe 7 lakini tukubali wapelestina kwa miaka na miaka wamekua watumwa ndani ya nchi yao, hakuna tofauti ya Afrika kabla hatujapata uhuru wetu na nchi namna Palestina anvyopitia, hakuna tofauti wavyoteseka wasauzi Afrka wa manyanyaso ya wakaburu na jinsi leo Palestina anvyonyanyasika na ukaburu wa Israel.
Wapo ndani ya nchi yao lakini hawana mamlaka, hapa nikazie bora kinachotokea Congo au vita maeneo mbali mbali hapa duniani mana ni migogoro ya ndan au mapandikiz toka nje lakin wapo huru na wanajtawala wenyewe na bado vikosi vya umoja wa mataifa vipo, vikosi mbali mbali vipo.
Lakin Palestina haina huo msaada, wao wanatawaliwa na Israel wao hawana msaada wowote ule k**a dunia imeitenga Palestna, hata msaada wa kibinadamu tuu muda wa vita anaemuru uingie ni Israel, huduma za kijamii wao ndo wanamua ziwepo au laa, uku Western bank ndo aibu mnoo.
Western Bank maeneo yote yanatawaliwa na Israel japo kuna Rais wa Palestina, wao ndo wanamua walale saangap, wao ndo wanakagua mipaka na njia toka sehemu nyengine nenda sehemu nyengine, jee huu sio utumwa?
Wachofanya Hamas ni kuikumbusha dunia ambayo ishasahau Palestina, na ishakubali wasrael wafanye wanachotaka, Hamas wamefanya kukumbusha dunia kwamba wamechoka na mateso ya wasrael na wanaona wanaenda toweka katika ramani ya dunia.
Israel na washirika wake wote wamewahadaa nchi za kiarabu ambapo na wao walishakubali Palestina kutoweka kwenye sura ya dunia, bila october 7 dunia isingejali tena kuhusu Palestina.
Leo hii dunia imeamka na sasa wanataka uwepo wa taifa huru la Palestina, leo hii dunia imeamka toka usingiz mzito na kukurupuka sasa wote tunajua kuna Palestina yahitaji uhuru wake.
NANI MSHINDI HADI SASA KATI YA HAMAS NA IDF
Kwenye vitabu viwili vya wanamikakati mashuhuri na wananadharia wa vita wakongwe namanisha kitabu cha 'ON WAR' cha Karl von Clauswitz na kile cha 'ART OF WAR' cha Sun Tzu..
Ndani ya vitabu hivi wamekubaliana au gongana kimtazamo juu ya swala la Malengo ya vita na ushindi wa vita.
Ambapo wote wanaeleza malengo ya vita yanaendana sambamba na malengo ya kisiasa na ushindi ndani ya vita ni pale malengo ya kisiasa yanapotimzwa ndani ya vita ndo mana watalamu wasuala ya mikakati ya kivita wanaamin Urusi ashamaliza mchezo muda tuu ila leo hatupo na mrus.
Tunapotazama vita vya Gaza basi tunatazama malengo ya kisiasa yaliyowekwa na je yametimizwa, kuboa majengo na kuuwa uwa raia waso na hatia hata wenye hatia haifanyi Israel iwe ndo mshindi sababu malengo yao hadi sasa hayatimia.
Malengo ya Israel yalikua matatu ambapo moja kuokoa mateka walotekwa na Hamas, ambapo hadi sasa mateka zaidi ya 100 hawajaokombolewa.
Lengo la pili kuiangamiza Hamas yote na kuitokomeza na hadi sasa Hamas ipo na inaendelea na mashambulizi.
Lengo la 3 ni kuithibiti Gaza na kuwa chini ya uangalifu wao lakini hadi sasa bado Gaza haipo chin ya uangalfu wa Israel.
Tunaweza sema ndani ya mwaka mmoja Israel haijashinda na imepoteza mana dunia kwa sasa yataka Palestina iwe huru na uanzshwaj wa nch mbil zenye kuheshimaina, Hamas hadi leo wameweza washkiria mateka ambapo Israel alijinasibu haitopita meizi mateka wote watakombolewa.
Lakini pia bado Hamas wapo na utawala ndan ya Gaza ambapo bado Israel anaangaika kuapatawala.
Kwanin malengo ya kisiasa ndo hutupa ushind wa vita?
Naomba nianze na mfano wa vita vya 1979 hapa ardhi ya Afrka Mashariki ambapo Tanzania walipigana na Uganda ambapo Tanzania alishinda.
Malengo ya yalikua dhibiti na kurudisha eneo la mtukura, pia kumuondoa madarakan, aliekua Rais wa Uganda Iddy Amin Dada, ivyo basi Tanzania hata ingebomoa na kuwa kila mwanajesh au raia wa Uganda k**a wasingerudsiha ardh ya mtukura, na kumfurumusha Dada basi bado wasingejinadi wameshinda vita.
Mara zote vita ni matokeo ya wanasiasa na sababu za kisiasa iyo malengo yasipofikiwa bado vita ujashnda, ni wazi nasema Israel ameshindwa vita hii achoweza fanya ni uharibifu na uuaji wa wasio na hatia.
Na ndoma japo ya kubomoa bomoa ovyoo majengo na kuuwa ovyo ovyo bado anaendelea na vita ambapo kwa jicho la juu juu utasema mbona haina haja tena mana Gaza ishachakazwa mbona bado anabomoa?
Sababu ni anachofanya sawa sawa na wachezaj wa mpira wenye njonjo na makeke lakini bado hawajapata goli ivyo wanasak**a lango la wapinzan wao na hamas ni sawa na team au wachezaj waliopata goli afu wanalilinda, ivyo mchezo ukiisha Hamas ni washind japo Israel ndo aliutawala mchezo na mbwembwe zote uwanjan. na hapa ndpo Von Clauswitz na Sun Ztu wanaelezea kuhusu 'role of offensive an defensive'
Ambapo jeshi linalojilinda vizur japo dogo kwa mashambuliz ni bora jeshi kubwa linaloshambulia sana, Hamas anashambulia kwa kuvizia lakin amewekeza mua wake mwngi kwenye kujilinda, ndo mana leo wapo wanaendelea na vita.
MWISHO
Wengi waliofungwa na udini huzungumzia kidini na wengi huchagua upande sababu ya udini, ni upungufu wa utimamu na uelewa wa uhalisia wa mambo lakini siwez hukumu, kinachtokea kule hakihusaini na dini japo dini imetumika sana wa muda mwing kleta mgawanyiko, ukwel yanayotoea ni ubabe tuu na dhuruma kwa kuhadaa watu waone wababe ndo wenye haki na wanaoonewa ni wakosaj ivyo wababe wanahaki ya kufanya anachofanya.
Tazama mgogoro huu njee ya udin uliolishwa uje na mtazamo sahihi, ondo chuki au mapenz unapotazama jambo hili, ndo mana Sauz Afrika yeye bega kwa bega na wanaoonewa mana anajua machungu yake.
Nashukuru Mungu dunia inaanza elewa nani mgomvi na nan mchokoz, ndo mana tumeshuhudia maandamano makubwa dunia nzma yakiunga mkono Palestna na kusimama nao huu ushind kwa Palestina ambapo miaka mingi walisuswa na dunia japo wanakufanya nyanyaswa sababu ya propaganda na uzushi.
Ni mimi Drim Bway Defya