15/06/2017
بسم الله الرحمن الرحيم
{FIQHI YA FUNGA NO 13}
naam bado tupo katika kuelezea mambo yanayoharibu funga,baada ya kutazama kigawanyo cha kwanza cha mambo yenye kuharibu funga na kuwajibika kulipia siku hiyo,sasa tuangalie kigawanyo cha pili ambacho ni:
ما يبطل الصيام ويجب القضاء والكفارة: {وهو الجماع لا غيره}
MAMBO YANAYOHARIBU FUNGA NA NI WAAJIB KULIPA NA KAFARA,[nalo ni jimai pekee]
k**a tulivyoashiria mwanzo kwa aya kua mwanzoni mwa kufaradhishwa ibada ya funga ilikua hairuhusuwi baada ya ftari mtu kukutana na mkewe,ila ikaja aya na kuondoa kifungu kile na allaah akaruhusu usiku watu kukutana na wake/waume zao,hivyo kwa mchana wa ramadhani haifai kukutana na mke/mume na ikimpitikia mtu akakutana na ahli yake ni waajib kufanya kafara ya kuacha huru mtumwa,au kufunga siku 60 mfululizo,akishindwa alishe maskini 60,tuangalie tukio lilotokana na swahaba abuu hurayrah r.a asema:
"tulikua sisi tumekaa na mtume s.a.w punde akatujia mtu akasema mtu huyo: "ewe mjumbe wa allaah nimeangamia mie" mtume s.a.w akamuuliza: "UNA NINI WEWE/KIMEKUANGAMIZA KIPI?" akajibu yule bwana: "NIMEMUINGILIA MKE WANGU MCHANA WA RAMADHANI HALI YA KUA MIMI NIMEFUNGA" mtume s.a.w akamuuliza: "UNAWEZA KUACHA HURU MTUMWA"? yule bwana akajibu: "HAPANA" mtume s.a.w akamuuliza: "UNAWEZA KUFUNGA MIEZI MIWILI MFULULIZO"? yule bwana akajibu: "HAPANA" mtume s.a.w akamuuliza: "JE UNAWEZA KULISHA MASKINI 60"? yule bwana akajibu: "HAPANA" mtume s.a.w akanyamaza muda ule ule na sie tumekaa mara akaletewa mtume s.a.w chombo chenye tende,akauliza mtume s.a.w "YUKO WAPI YULE MUULIZAJI"? yule bwana akajibu: "MIMI HAPA" mtume s.a.w akampa tende kisha akamwambia: "CHUKUA TENDE HIZI UTOE SWADAQA" yule bwana akamwambia mtume s.a.w "HIVI YUPO MTU MASKINI KULIKO MIMI EWE MJUMBE WA ALLAAH?NAAPA KWA ALLAAH BAINA YA NCHA MBILI ZA MADINA HAKUNA NYUMBA YA FAMILIA MASKINI KULIKO YANGU" mtume s.a.w akacheka sana mpaka meno yake yakaonekana kisha akamwambia: "KATOE SWADAQA KWA FAMILIA YAKO,WAPE WAO" [bukhar1936,muslim 1111]
katika hadithi twapata mafunzo mengi mno kubwa ni mfumo wa kafara ya mtu alokumbwa na janga la kumuingilia mkewe mchana wa ramadhani,pia funzo jengine la kuvutia ni utoaji wa swadaqa kwa familia,zama zetu swadaqa imekua kwa baadhi ya watu kutoa kwa fakhari,mtu familia yake hali duni lkn nje asifika kwa ukarimu,mtu wazazi wake hawakumbuki kwa kutengeneza mambo yao[mahitaji]tena pengine wana hali ngumu kweli lakini nje kwa watu kando huyu bwana asifiwa kwa ukarimu,laa swadaqa ianzie kwako ikiwa wahitaji wapo,
jumhuur ya wanachuoni ikapita kua hakika kuingilia kwa mfungaji katika mchana wa ramadhani kwa makusudi na kwa kuamua kwa kukutana tupu mbili kisha kikazama kichwa katika moja ya njia mbili[njia ya halali tupu ya mbele,au njia ya haramu tupu ya nyuma]mtu huyu hua ameharibu funga,na ni waajib juu yake kulipa na kufanya kafara iwe ametoa manii au hakutoa manii.
asema abuu maalik msimamo wa jumhuur katika kuwajibisha kulipa kwa huyu mwenye kuingilia mchana wa ramadhani kuna ziyada ilopokelewa katika baadhi ya hadithi kwa njia tofauti tofauti,nayo ni kua mtume s.a.w amesema mwisho wake:
"NA AFUNGE SIKU KULIPIA SIKU ILE" [daara qutwniyy 190] na wasema wanachuoni kua nyongeza hiyo ni dhaifu haikuthibiti,hivyo akapita ibn hazim kua ni waajib juu ya mtu huyo kafara tu.
tukiangalia upande wa mke nae je:
هل تجب الكفارة على المرأة كالرجل؟
JE NA MWANAMKE NAE ANAWAJIBIKA KAFARA K**A MWANAUME?
naam ukiangalia hadithi iliyotangulia utaona kua mtume s.a.w amemuamuru mwanaume kufanya kafarana akanyamaza kwa mwanamke ambae aloingiliwa,je anawajibika nae kufanya kafara au yeye hawajibiki?
jambo hili lina qwali kadhaa,,,QAWLI YA KWANZA:
ليس على المرأة كفارة مطلقا:
MWANAMKE HANA KAFARA YA MOJA KWA MOJA;
nayo ni mapito ya imaam shafi na qawli ya imaam ahmad,kua inawatosheleza wao kafara moja nayo ni kwa mwanaume kinyume na mwanamke kwa fahmu ifuatayo:
[1]hakika mtume hakuamuru kafara kwa mwanamke pamoja na kua ndie aloingiliwa,na kitendo kimetokea kwa mume na mke pamoja,wakatoa dalili kua ingekua mtume s.a.w kaona kuna uwajibu wa kafara kwa mwanamke angemlazimisha wala asingenyamazia jambo hilo.
[2]hakika haqqi ya kafara ni mali na mali amekhusishwa nayo mume k**a ilivyo katika mahri.
tukitazama QAWLI YA PILI NI KUA:
أنّ على المرأة كفارة كالرجل:
MWANAMKE NAE ANAWAJIBIKA KWA KAFARA K**A MWANAUME:
na hii ni qawli ya jumhuur,abuu hanifa,maalik,na qawli ya imaam shaafi,na qawli ya imaam ahmad katika qawli yake swahihi zaidi katika riwaya zake mbili,kwa ikhtilaaf na upambanuzi wao kuhusiana na mwanamke huru na mtumwa,na mwenye kukubali kufanyiwa kitendo na mwenye kuchukia[alojizuia ila akaingiliwa kwa kubakwa] wakasema:
[1]hakika mwanamke huyu amevunja funga yake ya ramadhani kwa kuingiliwa huko,na ni waajib juu yake kafara k**a mwanaume,na sheria imekua sawa kwa watu katika mambo ya kihukmu ispokua katika sehemu ambazo imekuja dalili ya khaasw,kukhusisha baadhi na kuwaacha baadhi,ikawa imelazimika kwak kuilipia siku hiyo kwa kule kuharibika funga hiyo,basi anawajibika na kafara k**a ilivyo kwa mwanaume.
[2]ama suala la mtume kutomuamuru mwanamke kufunga katika simulizi hii hii simulizi haikuenea mpaka kwa mwanamke,ukiangalia imesimuliwa upande mmoja ambao ni wa mume tu,na mume alivyosimulia kasema "nimeangamia" wala hakusema "tumeangamia"[kumjumiasha na mkewe] hivyo yawezekana ikawa mkewe hakua mwenye kufunga siku hiyo,kwa udhuru wa maradhi au safari,au mke alikua mwenye kuchukia ila mume akatumia mabavu,au yawezekana mke alijisahau k**a kafunga,n.k
[3]jambo la tatu ni kua mke hakwenda kumuuliza mtume s.a.w aloenda ni mumehivyo alojibiwa ni muulizaji ambae ni mume
[4]na imechukuliwa pia sababu ya mtume s.a.w kunyamaza ni hekma baada ya kuona maneno ya huyu mume kila aulizwalo hawezi ikiwa mume hawezi je kwa mke itawezekana vipi?
ama tukiangalia jambo hili QAWLI YA TATU:
أن يجزيهما كفارة واحدة إلا إن كانت الكفارة بالصيام فعليهما:
INAWATOSHELEZA WAO KAFARA MOJA[kuacha huru mtumwa,au kulishiza maskini 60}ISPOKUA IKIWA KAFARA YA KUFUNGA BASI WATAWAJIBIKA KILA MMOJA AFUNGE:
na haya ni mapito ya al awzaaiiy.
na qawli yenye nguvu kwa hili ni qawli ya jumhuur ambayo ni no 2,na qawli ya imaam shafi haiko mbali na hiyo.
ANGALIZO:
ikiwa mwanamke hakupenda jambo hilo,bali akabakwa,au akashiriki hali amejisahau k**a kafunga,hawajibiki kutoa kafara,pia ni hivyo hivyo kwa mwanaume akijisahau wala hana hukmu hiyo au nae akibakwa wala hawajibikiwi na kafara,na haya ni mapito ya abuu hanifa,shaafi,na ahmad [[al mughniy 3/27]
هل تجب الكفارة على الترتيب؟
JE NI WAAJIB KAFARA KWA MPANGILIO?
wamepita jumhuur ya ulamaa kua uwajibu wa mpangilio katika kafara wala hauhami kutoka katika kufunga miezi miwili mfululizo ila itapotokea mtu huyu ameshindwa kutoa huru mtumwa,na wala mtu halishi maskini 60 mpaka aada ya kua ameshindwa kufunga miezi miwili mfululizo,kwa uwazi wa hadithi iliyotangulia..
ama imaam maliki yeye asema mtu huyo ana khiyari kwa hadithi itokanayo na abuu hurayrah r. "أن رجلا أفطر في رمضان فأمره النبي صلى الله عليه وسلم أن يكفر بعتق رقبة،أو صيام شهرين متتابعين،أو إطعام ستين مسكينا"
"hakika mtu mmoja aliharibu funga yake ktk ramadhani[kwa jimai]mtume akamuamuru afanye kafara ya kuacha huru mtumwa au kufunga miezi miwli mfululizo,au kulisha maskini 60 [muslim 1111]
wakasema wanachuoni kua hadithi ilopokelewa na imaam bukhari hailazimishi mpangilio hakika katika suali hili mtu atafanyia kazi kwa kuchagua,imechukuliwa kua kuongoza kwake ktk kuacha huru mtumwa inakua ni karibu zaidi kuipitisha kafara,na wakachukua baadhi ya wanachuoni.
ama jumhuur ya wanachuoni wakapita mpito wenye nguvu kua hadithi iloweka mpangilio na ilokuja kwa khiyari hadithi iloweka mpangilio ndio ina nguvu zaidi,kwani walopokea hadithi hiyo ni wengi,pamoja na mmoja mmoja katika mapokezi,na hadithi ya khiyari inageuka geuka katika matamko,na qawli ya mpangilio ina nguvu zaidi na ndio ilochukuliwa[na mpangilio ni huu:]
KUACHA HURU MTUMWA
KUFUNGA SIKU 60 [miezi miwili]MFULULIZO
[3]KULISHA MASKINI 60.
tumalize kipengele hiki kwa kufafanua jambo hili:
هل تتكرر الكفارة بتكرر الجماع؟
JE ITARUDIWA KAFARA KWA KURUDIWA JIMAI[yaani kafara itakua zaidi ya moja ikiwa jimai imekua zaidi ya moja]?
[1]MWENYE KUINGILIA MCHANA WA RAMADHANI KISHA AKATOA KAFARA,KISHA SIKU INAYOFUATA AKAINGILIA TENA NI WAAJIB JUU YAKE KAFARA NYENGINE.
[2]MWENYE KUINGILIA KATIKA MCHANA MMOJA WA RAMADHANI ZAIDI YA MARA MOJA HUKMU YAKE NI KAFARA MOJA.
[3]MWENYE KUINGILIA MCHANA WA RAMADHANI N IKAWA HAJATOA KAFARA KISHA AKAINGILIA TENA SIKU INAYOFUATA,,,,katika hili kuna qawli mbili:
[1]NI WAAJIB KWAKE KILA SIKU KUTOLEA KAFARA KWANI KILA SIKU ALOINGILIA NI IBADA YA PEKE YAKE,[na ni qawli ya imaam shafi a malik na jamaa]
[2]WAAJIB KWAKE KAFARA MOJA MAADAM HAKUA AMEITEKELEZA KAFARA HIYO YA MWANZO,NAYO NI QAWLI YA ABUU HANIFA NA AWZAAIIY NA ZUHRIYY,wao wamefanya qiyaas ktk haddi ya zinaa,mzinifu alozini mara moja sawa na mzinifu alozini mara 20 na wakipatwa wana hukmu moja,sio kumuhesabia huyu wa 20 na masiku ambayo hakukutwa kua ndio apigwe bakora 2000 hapana atapigwa 100 tu,NA UKIANGALIA QAWLI MBILI HIZI UTAPATA QAWLI YA KWANZA INA NGUVU ZAIDI,KWANI KILA SIKU NA IBADA YAKE YA FUNGA HAIWEZEKANI HARIBIKO LA FUNGA YA LEO LIKAHARIBU YA KESHO,HIVYO HUYU MTU KAHARIBU LEO,NA KAHARIBU KESHO HIVYO ZOTE MBILI ATAWAJIBIKA.
mtumishi wenu
alfaqeer said saalim el bakry