Huruma siyo malezi
Radha ya Kiswahili
This is for Education material and for fun.
Kelele -zogo
Mtukutu-mtundu
Lukuki- wengi au kingi
Nyang'anya- pora
Kwida- kaba
DUMISHA LUGHA YA TAIFA
1. "Nimeona _simufifi_ yako lakini sikuwa na salio" neno simufifi maana yake ni "missed call"
2. "Samahani dada muuza mishkaki, nisaidie _kimbaka_ " neno kimbaka maana yake ni stick ya kuchokonolea meno. Tuendelee kukuza na kuendeleza kiswahili. Mchana mwema
Baniani mbaya kiatu chake dawa
Hakuna jambo baya ambalo litakosa uzuri waKe.
Mtoto wa nyoka huitwa Kinyemere.
Amu/Ami ndugu wa kiume wa baba waliyezaliwa tumbo moja
Habari za leo. Napenda kuwapa rai ndugu zangu.
Najua sisi sote humu ndani ya hili *_kundi sogozi_* tunamiliki _*simu tamba*_. Tuweni makini kwani kutumia _*sikanu*_ zetu _*mkondoni*_ kunaweza wapa mwanya wezi wa mtandaoni kutuibia. Wezi hutuma _*maunzi laini*_ yanayoweza kuharibu _*kitumi*_ chako au kuingilia _*makavazi*_ ya _*sikanu*_ yako. Wakishatuma _*maunzi laini*_ hayo nawe pasi na kujua ukibofya _*kiungo*_ kilichobeba _*maunzi laini*_ unakuwa _*umeshapakua*_ na _*kusanidi mtaliga*_ wenye uwezo wa kubadili au _*kughushi nenomsingi*_ lako na hivyo kunyima uwezo wa kuitumia _*sikanu*_ yako kwa kuifanya _*puku*_ kushindwa kutambua amri unazoipatia _*baobonye*_ ya _*kiwambagusa*_ cha _*sikanu*_ yako.
*JE KISWAHILI KITUMIKE K**A LUGHA YA KUFUNDISHIA KWA NGAZI ZOTE ZA ELIMU?*
⬇⬇⬇⬇⬇⬇⬇⬇⬇⬇⬇⬇
*Tafsiri ya maneno hayo*
1. Kundi sogozi = chatting group
2. Sikanu = smartphone
3. Kitumi=device
4. Maunzi laini=software
5. Kiungo=link
6. Kusanidi=install
7. Mtaliga=virus
8. Neno msingi=keyword
9. Puku=mouse
10.Baobonye=keyboard
11. Kiwamba gusa=touch screen
12. Makavazi=archives
13. Simu tamba=mobile phone
14. Mkondoni=online
15. Pakua=download
KISWAHILI LEO.
Mwimbaji wa taarab anaitwa *MUTRIBU*
chande
Ijumaa, 15 Mei 2015
KAMUSI YA LUGHA; MAANA, AINA, TAARIFA NA DHIMA ZAKE.
KAMUSI YA LUGHA; MAANA, AINA, TAARIFA NA DHIMA ZAKE.
MAANA YA KAMUSI
Massamba (2012:24) kamusi ni kitabu cha orodha ya maneno katika lugha, yaliyopangwa kwa utaratibu maalum, pamoja na maana au fasili zake; katika uchanganuzi wa lugha haya ni maneno ya kileksika, yaani yasiyokuwa ya kisarufi au kifonolija.
Tuki (1990:21) kamusi ni kitabu cha orodha ya maneno yaliyopangwa kwa utaratibu maalum, pamoja na maana na fasili zake.
Wamitila (2003:76) kamusi ni kitabu ambacho kina orodha ya maneno katika lugha Fulani ana ambayo hupangwa ki-abjadi au kialfabeti. Maneno haya huelezewa maana zake mbalimbali na labda hata vyanzo vyake.
Matinde (2012:273) kamusi ni kitabu chenye mkusanyiko wa maneno sanifu katika lugha mahususi yaliyoorodheshwa kialfabeti na kutoa taarifa za kifonetiki, kifonolojia, kimofolojia, kisintaksia, na hata kisemantiki.
Nyambari na Masebo (2012:179) kamusi ni kitabu cha marejeleo chenye msamiati uliokusanywa kutoka kwa wazungumzaji wa jamii fulani, na kupangwa kwa utaratibu maalumu, kisha kufafanuliwa kwa namna ambayo msomsji huweza kuelewa.
Kwa ujumla kamusi ni kitabu chenye orodha ya maneno mbalimbali yaliyopangwa vizuri kwa kufuata alfabeti na hutoa taarifa mbalimbali k**a vile maana, matamshi n.k.
MUUNDO WA KAMUSI
i) Utangulizi wa Kamusi
Hii ni sehemu ya mwanzo ambayo hutangulia matini yenyewe ya kamusi.
ii) Matini ya Kamusi
Hii ni sehemu ambayo inaonyesha vidahizo na fahiwa zake kuanzia herufi A-Z.
iii) Sherehe ya Kamusi
hizi ni baadhi ya taarifa ambazo huwa zimeandikwa mwishoni mwa kamusi. Kwa mfano majina ya nchi, lugha za mataifa duniani, vipimo vya urefu, vipimo vya uzito, ujazo n.k.
AINA ZA KAMUSI
Kwa kutumia kigezo cha LUGHA kuna aina kuu tatu (3) za kamusi
i) kamusi wahidiya
hii ni kamusi inayoandikwa kwa lugha moja
ii) kamusi thaniya
Hii ni kamusi inayoandikwa kwa lugha mbili.
iii) kamusi mahuluti
Hii ni kamusi inayoandikwa kw
KINYUME CHA NENO ITA NI = ITIKA.
Binuru ni kiitikio cha salamu Alamsiki.
Ami/amu = Ni ndugu wa kiume aliyezaliwa tumbo moja na baba yako.
Click here to claim your Sponsored Listing.
Location
Category
Contact the school
Telephone
Website
Address
Dar Es Salaam
Opening Hours
| Monday | 09:00 - 17:00 |
| Tuesday | 09:00 - 17:00 |
| Wednesday | 09:00 - 17:00 |
| Thursday | 09:00 - 17:00 |
| Friday | 09:00 - 17:00 |