02/09/2023
Kwa sisi wahenga
1. Wali na nyama ilikuwa ni kwa ajili ya chrismas au tukio fulani la kusherehekea
2. Mpira wa miguu half time ilikuwa inaamuliwa na idadi ya magoli, kwa mfano bao tatu geugeu. Msipofungana no half time.
3. Jezi ilikuwa timu moja kuvua mashati na nyingine kuvaa.
4. Njumu hazikuwa zinaruhusiwa uwanjani.
5. Goli likizidi kimo cha kipa siyo goli.
6. Penalt inaweza kutengwa hata k**a faulo imefanyika katikati ya kiwanja ilimradi ni faulo mbaya.
7. Wachezaji wote ni waamuzi wenye kushawishi kwa kelele zaidi hushinda
8. Mwenye mpira lazima apewe namba.
9. Mpira utaisha kwa sababu tatu. Mwenye mpira kuitwa nyumbani, giza kuingia au ngumi
10. Kulikuwa na nguo rasmi za jumapili na ndiyo siku ambayo kila mtu ataoga.
Nikumbusheni mengine.
Muhenga Moses