29/03/2020
*KILIMO CHA MCHICHA*
_UTANGULIZI_
Mchicha ni zao lililoka kwenye Jamii ya mboga za majani na linatambulika kwa kiingereza k**a Amaranth.Inaaminika aina nyingi za mchicha zilizosambaa dunian asili yake ni Amerika ya kati na kusini. Kuna aina nyingi za mchicha na zinatofautiana kwa vigezo mbali mbali kwa mfano Miiba ,rangi ya majani ,shina na kadhalika.Pamoja na mchicha kutumika k**a mboga ,pia ni mbegu za baadhi ya aina ya mchicha zimekuwa zikitumika k**a nafaka Kwa Tanzania yameanzia Mikoa ya Arusha ,Manyara ,Kilimanjaro na Dodoma
*UMUHIMU WA MCHICHA*
Nchini Tanzania mchicha umetumika k**a mboga ya majani inayojitosheleza bila kuchanganywa na mboga nyingine .Huliwa na vyakula vingine vya wanga k**a Ugali au Wali . Pia Mchicha katika kupikwa umekuwa ukichanganywa na mboga nyingine k**a vile dagaa,nyama,Samaki na mboga nyingine. Katika hali hiyo mchicha unatumika kuboresha na kukamilisha milo katika Familia mbalimbali ,migahawani ,mahotelin,shuleni na vyuo
Mchicha k**a mboga ya majani ina Vitamini na madini ya kutosha . Mchicha nafaka una virutubisho Lishe vingi zaid k**a vile Protini ,wanga ,chuma ,Chokaa,na mafuta ukilinganisha na mahindi.Pia zao hili la mchicha ni chanzo cha kipato kwa wakulima ,wafanyabiashara na wakala wa pembejeo za kilimo
```MAANDALIZI YA SHAMBA```
Shamba la mchicha linaandaliwa kwa kutifua ardhi kwa kina na kuondoa magugu yote.Kisha samadi ya mifugo ,mboji au makapi ya Tumbaku husambazwa na kuchanganywa na udongo kwa kutifua na husawazisha shamba vizuri.Maandalizi mazuri ya shamba ni muhimu kwa kuwa mchicha ukishapandwa hautarajiwi kupalilia hadi kuvunwa
*UPANDAJI WA MCHICHA MBOGA*
Mchicha huota na kukua vizur wakati wa joto .Mvua zikizidi mchicha hauoti vizuri na mwingi unakufa.Kipindi cha baridi baadhi ya aina za mchcha hazioti na kukua vizur .Mchicha kwa ajili ya kuvunwa k**a mboga hupandwa kwa kutawanya mbegu zikiwa zenyewe au zikiwa zimechanganywa na mchanga .
*```UKUAJI NA HUDUMA MUHIMU~*
Mchicha mboga huchukua kati ya siku 21 hadi 30 tangu kuota had kuvuna. Hata hivyo baadhi ya aina ya mchicha hasa wa kienyeji huchukua muda mrefu zaid kukua.Huduma muhimu kwa ukuaji wa mchicha ni umwagiliaji wa maji mara mbili kwa siku Hasubui na Jioni hasa kipindi cha Jua kali. Mbolea ya samadi ya kuku au mbolea za viwandani aina ya nitrojeni inaweza kutumika mchicha unapokuwa na wiki moja tangu Kuota ili kuongeza kasi ya ukuaji wa majani
šKilimo and na ufugaji kwanzaš±
For more updates