05/01/2023
Life long learning
Kuhusu ukurasa wetu wa facebook
Ukurasa huu ni wa wana chuo wa Taasisi ya elimu ya watu wazima makao makuu ya Dar -es- salaam, ni kwa ajili ya kufikisha maudhui kwa walimu, wanafunzi, wazazi na jamii kwa ujumla kuhusiana na kuelimisha juu ya elimu kwa watoto wa kitanzania kupitia picha , michezo na video.
Stadi za maisha
Kuhusu maisha yetu ya kila siku pamoja na kukataa vitendo vya kikatili kwa watoto wetu.
Elimu
Elimu inakua na changamoto kubwa katika maendeleo ya Tanzania tangu uhuru
Wasichana, watoto masikini zaidi, watoto wenye ulemavu na watoto wanaoshi katika jamii ambazo hazijahudumiwa wako katika hatari zaidi ya kuacha shule au kutokwenda shule, mimba za utotoni na ndoa. Utafiti uliofanywa na shirika la UNICEF unaonesha kwamba mimba za utotoni zilisababisha karibu wasichana 3700 kuacha elimu ya msingi na secondary mwaka 2016, zaidi ya theluthi moja ya wasichana wameolewa wakiwa na umri chini ya miaka 15 , zaidi ni wasichana kutoka katika familia za kimasikni ambapo wana uwezo kuliko wasichana wanaotoka katika familia za kutahiri kuolewa.
Suluhisho
Kikundi cha life long learning group no 6 linaunga mkono juhudi za serekali kuhakikisha kila mtoto wa kitanzania anapata elimu bora ya msingi. Hili ili lifanyike watoto watahitajika kuwa tayari kwa kujitunza , walimu wawe tayari kufundisha na shule ziwezeshwe kutoa elimu bora.