Stawi Ministries

Stawi Ministries Karibu katika ukurasa wa huduma ya Stawi. Huduma hii ni kwa ajili ya kufundisha Neno la Mungu

Mtu mwenye imani ni UPGRAGE ya mwanadamu. Lakini, imani chanzo chake ni KUSIKIA NENO LA KRISTO.NENO LA KRISTO ni Neno la...
19/08/2026

Mtu mwenye imani ni UPGRAGE ya mwanadamu. Lakini, imani chanzo chake ni KUSIKIA NENO LA KRISTO.

NENO LA KRISTO ni Neno la Msalaba, ni Neno la ukamilifu wa kazi aliyokuja kuifanya Kristo ili wewe upate kuokolewa!!!

Bila Neno la Kristo hakuna imani; kunaweza kuwa na dini, au mazoea au sheria, vigezo na masharti na matendo mema. Lakini HAKUNA IMANI BILA KUSIKIA NENO LA KRISTO.





Enjoy the videos and music you love, upload original content, and share it all with friends, family, and the world on YouTube.

IMANI NI HAKIKA YA MAMBO YATARAJIWAYO.HAKIKA NI "SUBSTANCE". Hakika ni mashiko. Ni kuyang'ang'ania mambo unayoyatumainia...
18/08/2026

IMANI NI HAKIKA YA MAMBO YATARAJIWAYO.

HAKIKA NI "SUBSTANCE". Hakika ni mashiko. Ni kuyang'ang'ania mambo unayoyatumainia, unayoyatarajia.

Ukweli ni kwamba mambo unayoyatumainia, YAPO!!!

Kuamini ni kutumia rasilimali zisizo za kimwili, ni kuungana na uwanda usio wa kimwili. Ni jambo la juu.

Ile HAKIKA ikikaa sana ndiyo yenye kuyafanya mambo yatarajiwayo, kutoka huko yalipo (Rohoni) na kuja katika uwanda wa mwili au wa mambo yanayoonekana.





Enjoy the videos and music you love, upload original content, and share it all with friends, family, and the world on YouTube.

Kuamini ni kujiunga na ulimwengu usioonekana, usio wa kimwili, na mambo yasiyoonekana na mambo yasiyo ya kimwili, lakini...
16/08/2026

Kuamini ni kujiunga na ulimwengu usioonekana, usio wa kimwili, na mambo yasiyoonekana na mambo yasiyo ya kimwili, lakini yana mashiko, au yapo.
Kuamini ni kuyafanya mambo ambayo yapo katika uwanda wa roho kuonekana katika uwanda huu wa damu na nyama.
Mtu wa imani haenendi kwa jinsi ya kuona, hayazingatii mambo yanayoonekana, anayazingatia mambo yasiyoonekana; kwamba mambo hayo YAPO.

Mambo yasiyoonekana YAPO.

Kuamini si kuyafanya mambo ambayo hayapo, yawepo; bali ni kuyafanya mambo ambayo yapo katika ulimwengu usioonekana kuwapo katika ulimwengu unaoonekana.

Imani ni MASHIKO ya mambo yasiyoonekana; ni BAYANA ya mambo yatarajiwayo.

Jambo la msingi kujua hapa ni kwamba YAPO mambo katika uwanda usioonekana. YAPO!!! Na mambo hayo ndio halisi kuliko mambo yanaoonekana.





Enjoy the videos and music you love, upload original content, and share it all with friends, family, and the world on YouTube.

15/08/2026

Mwamini Mungu! Ni mfululizo wa kujifunza juu ya kumwamini Mungu. Nimeanza na utangulizi ili kufungua pazia la kile tutakachoendelea kujifunza zaidi.

Ujuzi Huleta Majivuno
14/08/2026

Ujuzi Huleta Majivuno

Enjoy the videos and music you love, upload original content, and share it all with friends, family, and the world on YouTube.

03/08/2026

Tumaini pekee la mtu kuupata utukufu wa Mungu ni kupitia Yesu Kristo. Utukufu ni kilele cha utimilifu wa Mungu.

Yesu Kristo ni utukufu wa Mungu ulioshikika, ulioonekana kwa macho, ulioishi na watu wa damu na nyama. Sasa utukufu huo upo ndani ya wale waliomwamini wakazaliwa na yeye.



02/08/2026

USHIRIKA NA MUNGU

01/08/2026

Mtu aliyeokoka huwa anakuwa na ushirika na Mungu. Kuna mambo ambayo Mungu anamshirikisha. Jambo la kwanza ni asili yake ya uungu. Mtu anapewa asili mpya, asili ya Mungu.

Mtu huyo amepewa kuungana na Mungu katika roho. Yaani, anakuwa ameungwa na Bwana, na anakuwa Roho mja naye.
2
Anakuwa ameungwa na Mungu moja kwa moja, kila siku, kila saa. Hakuna wakati ambapo mtu huyo anapokuwa nje ya Mungu, au anapokuwa ametengwa na Mungu. Mtu huyo haungani na Mungu wakati wa maombi tu, bali ameungwa na Bwana 24/7

K**a umeokoka, unaishiriki asili ya Mungu, ya uungu. Una asili ya Mungu. Unafanana na Mungu; unamiliki, unatawala, unatiisha, unaumba (unazaa), anaongezeka.





Mtu aliyeokoka ameshiriki kifo na ufufuo wa Bwana Yesu.

Mambo niliyoyaelezea hapo juu ni matamu sana kusikia kwenye masikio. Lakini kwa wengine yatakuwa magumu sana. Soma tu 2 Petro 1:3-5.

Mambo hayo ni matamu masikioni, lakini hayadhihiriki kwa kila mtu. Tena, ni Yesu peke yake aliyeyadhihirisha kwa asilimia mia. Mimi na wewe hatujadhihirisha chochote bado. Hatua ya kwanza ya kuyadhihirisha ni kwa kuyafikirifikiri mambo ya Mungu yaliyo kwenye Neno la Mungu, k**a haya ninayokuandikia. Utakapoanza kwa kukubali, itakuwa hatua kuu sana, hautojilaumu kwa kupata huo ufunuo.

Agizo kuu la Bwana Yesu lilikuwa ni, "Mkawafanye mataifu kuwa wanafunzi, mkiwafundisha kuyashika yote niliyowaagiza".   ...
27/07/2026

Agizo kuu la Bwana Yesu lilikuwa ni, "Mkawafanye mataifu kuwa wanafunzi, mkiwafundisha kuyashika yote niliyowaagiza". Fuatilia mafundisho ya uanafunzi, kupitia link ya youtube hiyo hapo chini

Kwa usahihi, title ya somo hili ingekuwa uinjilisti kwa njia ya kufundisha. Njia yenye uhakika wa kuwaimarisha watakatifu ni ya kuwafundisha kuyashika yote a...

Address

P. O Box 12345
Dar Es Salaam
0255

Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00
Tuesday 09:00 - 17:00
Wednesday 09:00 - 17:00
Thursday 09:00 - 17:00
Friday 09:00 - 17:00
Saturday 09:00 - 17:00
Sunday 09:00 - 17:00

Telephone

+255768979282

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Stawi Ministries posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The School

Send a message to Stawi Ministries:

Shortcuts

Share

Category