🌫️🌺🪐🎙️Daka Lulu Chap Chap
Alhabiib sheikh mwinyi (JLT)
17 March 2021
Mbagala, MADIMBA
Katika vitu ambavyo muridi wanashindwa kupanda na kufika kwa mungu ni kutokuji control na ibada. Utakuta mtu yupo katika daira ama kikazi cha kumtaja mungu lakini muda mwingi anashughulishwa na simu, mara aende nje akaipokee, mara anyanyuke nyanyuka
Yote hii inatokana na kutokuji control yeye kwa yeye
Na ukitaka kujua faida ya kuji control watizame muridi wa zamani. Zama za kina juneyd baghdad,sirri saqatwi, syd abdulqaadiri jeylan,sheikh uweys ahmad nk.
Hata naqshaband (TWARIYQATUL) ukiwatizama katika majaalis zao wakishaanza tu ibada au uradi basi wanaachana na mambo yote ya kujishughulisha na nje ya mungu. Huwaoni wakipokea simu wala wakinyanyuka nyanyuka kwenda sehemu
Lakini ajabu ya muridi wa sasa! wakikaa katika daira basi muda wote wako na simu,mara wanyanyuke kutoka nje
Ukiwauliza nini kinachowanyanyua nyanyua utaskia naenda kupokea simu nje, hii ni AJABU!
Ibada ni ibada, na ibada yatakikana utulivu
Kwanini wakati wa swala yoyote ya faradhi au ya sunnah huachi swala na kupokea simu? au katika taraweh!
Hufanyi hivyo kwa sababu unajua upo direct ( moja kwa moja ) unazungumza na mola wako, basi na katika daira napo uwe hivyo hivyo, na tukitulia khaswaa katika madaira. Tukiwa na khushui ya hali ya juu khabbar zetu zitatupitia papo hapo, sio mpaka tulale usingizi.
Ibn syd othman aljamalullayl....✍🏼🐪
AFISA HABARI
ZAWIYANI KUNDUCHI
الحبيب الشيخ موني - Alhabiib sheykh mwinyi
Sufism
Want your school to be the top-listed School/college in Dar es Salaam?
Click here to claim your Sponsored Listing.
Click here to claim your Sponsored Listing.
Location
Category
Contact the school
Website
Address
Kanani
Dar Es Salaam