TAFAKURI
Karibu tujifunze lugha adhimu na adimu ya Kiswahili
Uhusiano wa Sintaksia na Matawi mengine ya Isimu
Dhana ya sintaksia imejadiliwa na wanazuoni mbalimbali ;
Massamba na wenzake (1999:34) anasema “sintaksia ni utanzu wa sarufi unaojihusisha na uchunguzi wa mpangilio wa maneno katika sentensi na uhusiano wa vipasho vyake”. Wanaendelea kusema, utanzu huu huchunguza sheria au kanuni zinazofuatwa katika kuyapanga maneno ili yalete maana inayokubalika na kueleweka katika lugha husika.
Habwe na Karanja (2004) wanasema “sintaksia ni utanzu wa isimu unaoshughulikia muundo wa sentensi na elementi nyingine zinazounda sentensi k**a vile kategoria za maneno, vikundi na vishazi”
TUKI (2004)anasema “sintaksia ni tawi la isimu linaloshughulikia uchanganuzi wa taratibu na kanuni za mahusiano baina ya maneno katika tungo” kwa ufupi sintaksia ni tawi la isimu ambalo linachunguza muundo wa tungo pamoja na uhusiano wa vipashio hivyo vinavyounda tungo ambayo ni nukta pacha, neno, kirai na kishazi.
Kwa ujumla sintaksia ni tawi la isimu ambalo linahusu namna maneno yanavyoungana na kuhusiana kirai, kishazi na sentensi. Sintaksia inachunguza namna maneno yanavyojipanga katika sentensi kwa kuzingatia kanuni za sarufi ya lugha husika.
Kwa hiyo kutokana na kwamba sintaksia pia ni kitengo mojawapo kinachounda maarifa ya lugha, kwamba, sintaksia haiwezi kutenganishwa na vitengo vingine vya lugha kutokana na uhusiano mkubwa uliopo baina ya vitengo hivi. Vitengo hivi hutegemena na kuathiriana. Hivyo basi tunaweza kuonesha jinsi sintaksia isivyoweza kutenganishwa na vitengo vingine vya lugha yaani fonolojia, mofolojia na semantiki k**a ifuatavyo:
Uhusisno uliopo kati ya sintaksia na fonolojia.
Massamba na wenzake (1999:34) wanasema “fonolojia ni uchambuzi wa mfumo wa sauti katika lugha mahususi” Ni jinsi ambavyo vitamkwa au sauti za lugha zinavyoungana ili kujenga maneno yanayokubalika k
Eston's Online
Education for liberation
Samahani kwa wale mnaotembelea page hii na kuku hakuna muendelezo wa mada, kuna vitu naweka sawa then tutaanza kunufaika na page hii...kuanzia next week...🙏🙏🙏
Eston online
Friday,
Maana ya lugha
MAANA YA LUGHA
UTANGULIZI
Lugha imewahi kufafanuliwa kwa jumla k**a mfumo wa sauti za nasibu za kusemwa zinazotumiwa na watu wa jamii Fulani wenye utamaduni unaofanana kwa madhumuni ya mawasiliano katika jamii hiyo.
Wataalamu wengi wa isimu (sayansi ya kuchanganua lugha na kuieleza jamii) kamusi ya kiswahili sanifu TUKI 1981 oxford press uk. 86 na lugha wanaelekea kukubaliana kwamba lugha ni mfumo wa sauti nasibu ambazo hutumiwa na jamii kwa madhumini ya mawasiliano kati yao ( massam ba D.P.B na wenzake 1999, TUKI).
Lakini inaeleweka ya kwamba viumbe vingine navyo vinaweza kutoa sauti za aina mbalimbali na aghalabu kwa madhumuni hayo hayo ya mawasiliano viumbe hivyo vinaweza kuwa kuku, amwonapo mwewe kuna lugha au sauti anayoitumia kuashilia hatari Fulani ama mbuzi anapokuwa na mtoto .
Cha kujiuliza hapa ni je, hizi nazo zinaweza kuitwa lugha? Aidha binadamu na viumbe vingine huweza kutoa ishara mbalimbali kwa madhumuni ya mawasiliano. Hizi nazo zimekuwa zikiitwa lugha kutokana na dhima yake ya kuwezesha mawasiliano baina ya viumbe hivyo swali linalohitaji kuulizwa tena katika hatua hii ni je ni kweli hizi zote ni lugha kwa maana ile ile?
Ili kujibu swali hili pengine ni muhimu kwanza kubainisha missingi ya tofauti kati ya lugha hizi zilizotajwa msingi mkubwa wa tofauti baina ya hizi “lugh” ni jinsi utoaji na utumiaji wa sauti na ishara husika vinavyochochewa kwa mfano inajulikana kwamba wakati binadamu kwa kiasi kikubwa hujifunza kutoa na kutumia sauti na ishara viumbe vingine vyote hutegemea mno silica zao katika kutoa na kutumia sauti na ishara. Hii ndio pengine ndio sababu humchukua mtoto wa binadamu takribani miaka mitatu kuweza kumudu lugha.
AINA ZA LUGHA
Wataalamu wamefikia kutenga aina kuu mbili za lugha. Hizi ni lugha asili na lugha unde.
Lugha asili ni ile inayohusisha mfumo wa sauti zinazotolewa kwa kutumia ala katika chemba yam domo wa binadamu.
Lugha unde kwa upande mwingine ni ile inayo
Jinsi ya Kuandika MAKALA Kitaalam
Tambua ya kuwa miundo ya kuandika Makala ipo ya aina tofauti, ila zote zina mfumo au njia zinafwata. Waandika makala wakubwa hua wana njia ambayo hutumia kuandika makala zao.
Kulingana na umakini wako, mbinu yako, makala yako inaweza kuwa na tofauti kidogo, lakini katika hayo kuna mbinu ambayo yanaweza fanya machapisho au makala kuwa na nguvu sana na muonekano mzuri. Mbinu hizo chache unaweza fuata ni..
1. Kichwa cha habari kinachovutia.
Ikiwa unataka kuandika makala kubwa kwa ajili ya blogi, tumia wakati kuunda kichwa cha habari, kinachowavutia wasomaji, na kuwaacha wakitamani ushauri, au maelekezo yako. “Hii ni hatua ya kwanza (na ya mwisho) kabla ya kuchapisha makala.”
Vitu vya kuzingatia katika kuandika kichwa cha habari:
a. Chagua mada yenye mvuto
Hakikisha mada utakayoiwasilisha iwe na wasomaji na hao watajisikia kulazimishwa kubonyeza na kupata suluhisho la kile wanachokipenda au kuwasumbua.
b. Chambua makala za watu wengine
Kuchunguza makala za wengine zinakupa muongozo wa kile ambacho wewe una mpango wa kukiandika.
c. Onjesha
Kichwa cha habari kinapaswa kimpe msomaji hamasa ya kuja kusoma makala yako. Usimpe msomaji majibu kwenye kichwa cha habari.
d. Punguza maneno, weka maneno yenye mvuto zaidi.
Kichwa chako cha habari kifanye kuwa kifupi na chenye nguvu iwezekanavyo. Ondoa maneno dhaifu na weka maneno ya nguvu yenye msisimko.
2. Andika utangulizi wenye msisimko
Inapokuja kwenye mtandao – urefu wa umakini wa watu ni mdogo zaidi kuliko makala ya kuchapishwa, hivyo aya yako ya ufunguzi ni muhimu. Waandishi wa habari wanalitambua hili. Msomaji huanza kuridhishwa na maelezo ya mwanzo wa makala na maelezo hayo humfanya msomaji aendelee kusoma.
Vitu vya kuzingatia katika kuandika utangulizi
a. Ingia kwenye akili ya msomaji
Ingia ndani ya viatu vyao na uandike kutoka kwa au kulingana na mtazamo wao. Waonyeshe unaelewa vizuri wanayopitia. Tambua nia ya msomaji k**a vile wewe ni msomaji.
b. Washawishi waso
KWA MAKALA...ZOTE ZA KISWAHILI NOTES ZOTE ZA ADVANCE NA O'LEVEL...NA JINSI YA KUANDIKA MAKALA BORA TEMBELEA PAGE HII
Click here to claim your Sponsored Listing.
Location
Category
Website
Address
Bukoba
Dar Es Salaam
P.O.BOX239
Opening Hours
| Monday | 09:00 - 17:00 |
| Tuesday | 09:00 - 17:00 |
| Wednesday | 09:00 - 17:00 |
| Thursday | 09:00 - 17:00 |
| Friday | 09:00 - 17:00 |
| Saturday | 09:00 - 17:00 |
| Sunday | 09:00 - 17:00 |