Pugu Boys Secondary and High School

Pugu Boys Secondary and High School P. O. Box 9090,
Dar Es Salaam. School Motto: Aim At Excellence. Docebit Vos Omnia.

Meet PUGU SECONDARY SCHOOL ALUMNI, Mr Karim Biomanda Karim Boimanda 📍Afisa habari wa Bodi ya Ligi Kuu Tanzania Bara NBC ...
17/08/2026

Meet PUGU SECONDARY SCHOOL ALUMNI, Mr Karim Biomanda Karim Boimanda

📍Afisa habari wa Bodi ya Ligi Kuu Tanzania Bara NBC Premier League 🇹🇿


15/08/2026

MADAM CONSOLATA BLASI MIONGONI MWA WALIMU WALIOPATIWA MAFUNZO YA SAYANSI KWA UENDELEVU NA USALAMA WA CHAKULA

Walimu wa masomo ya sayansi na kilimo kutoka shule tano za sekondari za mikoa ya Pwani na Dar es Salaam walipatiwa mafunzo na maarifa mapya kuhusu namna ya kufundisha wanafunzi elimu ya sayansi inayozingatia uchunguzi, uendelevu na usalama wa chakula.

Mafunzo hayo yaliandaliwa na Ubalozi wa Israel kwa kushirikiana na Kitivo cha Elimu cha Chuo Kikuu cha Bar-Ilan pamoja na Taasisi ya Elimu Tanzania (TET), na yalifanyika katika Shule ya Sekondari ya Wavulana Kibaha.

Miongoni mwa walimu walioshiriki mafunzo hayo ni Madam Blasi, mwalimu wa somo la Biolojia, pamoja na Mr. Mahagi, mwalimu wa somo la Kilimo kutoka PUGU BOYS SECONDARY AND HIGH SCHOOL

Credit: AzamTV

Ungana nasi katika safari hii ya kihistoria na yenye kuacha alama.Hakuna mchango mdogo wala mkubwa. Kila mchango una tha...
13/08/2026

Ungana nasi katika safari hii ya kihistoria na yenye kuacha alama.
Hakuna mchango mdogo wala mkubwa. Kila mchango una thamani. Utasaidia kuboresha miundombinu na mazingira ya kujifunzia, kubadilisha maisha ya wanafunzi wenye mahitaji maalum, na kujenga urithi wa kudumu kwa vizazi vijavyo.

CHANGIA KUPITIA:
Jina la Akaunti: Pugu Secondary Alumni Group
CRDB Akaunti: 10355320109
Lipa Namba (CRDB): 118168695
Jina: Pugu Secondary Alumni

Kwa michango isiyo ya fedha taslimu, wasiliana na viongozi kupitia namba za simu zilizo kwenye kipeperushi.

Pamoja Tunaijenga Upya Pugu!

  2006Muda umepita, sura zimebadilika, maisha yameendelea… lakini kumbukumbu bado zinaishi. One picture. Many faces. A t...
13/08/2026

2006

Muda umepita, sura zimebadilika, maisha yameendelea… lakini kumbukumbu bado zinaishi.

One picture. Many faces. A thousand memories. 📸
Form Four, Class of 2006.

Some moments become memories, and some memories become priceless. Before these memories became history… there was this moment.


13/08/2026

Rai hiyo imetolewa na Mkuu wa Shule Mwl. Patrick Sinyinza wakati akipokea msaada wa Bima ya Afya, Viti mwendo na Kompyuta kutoka Kampuni ya ALC Group kwa ajili ya wanafunzi wenye mahitaji maalum.

Credit:


ALC Group, wauzaji wa vilainishi vya Flying Horse Lubricant, wametoa msaada kwa wanafunzi wenye mahitaji maalum wa Shule...
13/08/2026

ALC Group, wauzaji wa vilainishi vya Flying Horse Lubricant, wametoa msaada kwa wanafunzi wenye mahitaji maalum wa Shule ya Sekondari Pugu, ikiwemo bima ya afya kwa wanafunzi 50, viti mwendo pamoja na kompyuta.

Msaada huo unalenga kuwawezesha wanafunzi hao kupata huduma za afya kwa wakati, kushiriki kikamilifu katika masomo na kurahisisha shughuli zao za kila siku.

Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo, Mkuu wa Idara ya Elimu Maalum Mwl. Elvis Lyimo, amewashukuru ALC Group kwa msaada huo na kutoa wito kwa kampuni binafsi, taasisi na wadau mbalimbali kuendelea kusaidia wanafunzi wenye mahitaji maalum kwa kuwapatia huduma za afya, vifaa saidizi na mahitaji ya kielimu.

Mwl. Lyimo amesema Shule ya Sekondari Pugu ina jumla ya wanafunzi 85 wenye mahitaji maalum, ambao baadhi yao hutoka katika familia zenye uwezo mdogo kiuchumi na hivyo kukabiliwa na changamoto za kupata huduma za afya, mahitaji ya kila siku pamoja na vifaa muhimu vya kujifunzia na kujikimu.

Kwa upande wake, Mkuu wa Shule Mwl. Patrick Sinyinza, amewataka wazazi na walezi kutowaficha watoto wenye ulemavu majumbani, bali kuwapeleka shule ili wapate haki ya elimu na fursa ya kuendeleza vipaji na uwezo wao.

Akizungumza kwa niaba ya ALC Group, Ndg. Emmanuel Shija, Balozi wa kampuni hiyo na Bingwa wa WBC Muay-Thai Tanzania, amesema msaada huo ni sehemu ya utekelezaji wa wajibu wa kampuni kwa jamii.

Amesema kampuni hiyo itaendelea kugharamia bima ya afya kwa baadhi ya wanafunzi, pamoja na kutoa vifaa saidizi, ikiwemo baiskeli za magurudumu matatu, kwa lengo la kuwawezesha wanafunzi wenye mahitaji maalum kushiriki kikamilifu katika shughuli za kila siku.

Kwa upande wa wanafunzi, Thobias Masumbulko, aliyewakilisha wanafunzi wenzake, ameishukuru ALC Group kwa msaada huo, akisema vifaa walivyopatiwa vina thamani kubwa katika maisha yao na vitawasaidia katika masomo na shughuli zao za kila siku.


  2018Picha hubeba historia na kumbukumbu za matukio ambayo wakati mwingine maneno pekee hayatoshi kuyasimulia. 📸✨Hawa n...
12/08/2026

2018

Picha hubeba historia na kumbukumbu za matukio ambayo wakati mwingine maneno pekee hayatoshi kuyasimulia. 📸✨

Hawa ni baadhi ya wahitimu wa Kidato cha Sita, mwaka 2018 — kumbukumbu ya safari, urafiki na nyakati zisizosahaulika.

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wanafunzi Waliosoma Pugu, PUGU SECONDARY SCHOOL ALUMNI, Ndugu Amani Mshubi, amemkabidhi Mkuu wa...
11/08/2026

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wanafunzi Waliosoma Pugu, PUGU SECONDARY SCHOOL ALUMNI, Ndugu Amani Mshubi, amemkabidhi Mkuu wa Shule, Mwalimu Patrick Sinyinza, Lipa Namba rasmi kwa ajili ya kurahisisha, kuhamasisha na kuchochea ushiriki wa Pugu Alumni, wazazi, marafiki, wageni na wadau wengine wote wanaofika shuleni kuchangia Kampeni ya PUGU ALUMNI 2026.

Hatua hiyo ni sehemu ya maandalizi ya Pugu Alumni Day 2026, inayotarajiwa kufanyika tarehe 14 Oktoba 2026, pamoja na juhudi za kutimiza lengo la kukusanya TSh milioni 325 kabla ya tarehe hiyo..

Fedha zitakazopatikana zitalenga kuboresha miundombinu ya shule, ikiwa ni kukarabati jengo la Zahanati, Ofisi ya Taaluma, kukamilisha ujenzi wa Uzio, pamoja na kuimarisha huduma kwa wanafunzi, wakiwemo zaidi ya wanafunzi 130 wenye mahitaji maalum.

Wadau wote wanaalikwa kuunga mkono Kampeni hii kwa hali na mali ili kuwa sehemu ya safari hii ya kihistoria na yenye kuacha alama.
Mbali na fedha, kampeni hii pia inapokea vifaa vya ujenzi na ukarabati, vifaa saidizi kwa wanafunzi wenye mahitaji maalum (Vitimwendo, Fimbo maalumu za kutembelea, mafuta maalum kwa wenye ulemavu wa ngozi, Kompyuta, Vishikwambi n.k) pamoja na vifaa na thamani za ofisini na hospitalini.

CHANGIA KUPITIA:
Jina la Akaunti: Pugu Secondary Alumni Group
CRDB Akaunti: 10355320109
Lipa Namba (CRDB): 118168695
Jina: Pugu Secondary Alumni

Au wasiliana na viongozi kwa ajili ya kuwasilisha michango isiyo ya fedha taslimu..

MAWASILIANO:
Mwenyekiti: +255 766 029 345
Makamu Mwenyekiti: +255 757 686 331
Katibu Mkuu: +255 767 054 942
Naibu Katibu Mkuu: +255 688 899 652
Mtunza Hazina: +255 655 115 552

PUGU ALUMNI
Brothers of the Nation, Sons of Legacy 



REMEMBERING TEDSON MASATU — EGM 2003Some memories never fade. Some moments remain forever etched in the heart of a schoo...
09/08/2026

REMEMBERING TEDSON MASATU — EGM 2003

Some memories never fade. Some moments remain forever etched in the heart of a school.

Today, we remember with deep sorrow and heavy hearts the tragic loss of Tedson Masatu, a beloved student of PUGU BOYS SECONDARY AND HIGH SCHOOL, EGM, Class of 2003, whose life was brutally cut short when armed robbers invaded our school, leaving behind sorrow, shock, and a wound that has never truly healed.

The memory of that fateful night remains one of the darkest and most painful chapters in our school’s history. The shock, fear, grief, and unbearable loss of a young life are memories that time cannot erase.

Tedson was taken from us far too soon, but he will forever remain a part of the Pugu family. His memory lives on in the hearts of his fellow students, teachers, and all who knew him.

Today, we mourn. We remember. We honour his life with love and respect.

May his soul rest in eternal peace. 🕊️
Tedson Masatu — forever remembered, forever missed.


Jumuiya ya Wanafunzi Waliosoma Pugu, PUGU SECONDARY SCHOOL ALUMNI, wamelenga kukusanya Shilingi milioni 325 kwa ajili ya...
08/08/2026

Jumuiya ya Wanafunzi Waliosoma Pugu, PUGU SECONDARY SCHOOL ALUMNI, wamelenga kukusanya Shilingi milioni 325 kwa ajili ya kuchangia ukarabati na uboreshaji wa miundombinu ya shule. Mchango huo pia utasaidia kuboresha mazingira ya wanafunzi wenye mahitaji maalum, wakiwemo zaidi ya wanafunzi 130 wanaohitaji mazingira rafiki na salama zaidi ya kujifunzia.

Fedha zitakazokusanywa zitatumika katika:
* Ukarabati wa jengo la Zahanati ya Shule;
* Ukarabati wa jengo la Ofisi ya Taaluma;
* Kukamilisha ujenzi wa uzio kuzunguka eneo la shule.

Mbali na fedha, kampeni hii pia inapokea vifaa vya ujenzi na ukarabati, vifaa saidizi kwa wanafunzi wenye mahitaji maalum (Vitimwendo, Fimbo maalumu za kutembelea, mafuta maalum kwa wenye ulemavu wa ngozi, Kompyuta, Vishikwambi n.k) pamoja na vifaa na thamani za ofisini na hospitalini, kulingana na mahitaji ya shule.

Kampeni ya kuchangisha fedha na vifaa inaendelea hadi mwezi Oktoba 2026, ambapo kilele chake kitakuwa Pugu Alumni Day 2026, itakayofanyika tarehe 14 Oktoba 2026 katika viwanja vya shule. Siku hiyo itaenda sambamba na maadhimisho ya Nyerere Day, tukienzi na kukumbuka urithi wa Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, ambaye pia aliwahi kuwa Mwalimu wa PUGU BOYS SECONDARY AND HIGH SCHOOL

PUGU SECONDARY SCHOOL ALUMNI wanawakaribisha wahitimu wote wa Pugu, pamoja na wazazi, marafiki, wadau, vyombo vya habari, makampuni, taasisi na mashirika mbalimbali, kuungana nasi katika kuenzi urithi wa Pugu kwa kuchangia maendeleo ya kizazi cha sasa na kijacho.

CHANGIA LEO KUPITIA:
Jina la Akaunti: Pugu Secondary Alumni Group
CRDB Akaunti: 10355320109
Lipa Namba (CRDB): 118168695
Jina: Pugu Secondary Alumni

Unaweza pia kuchangia kwa kuscan QR Code, au kuwasiliana moja kwa moja na viongozi wa Jumuiya kwa ajili ya kuwasilisha michango isiyo ya fedha taslimu, ikiwemo vifaa vya ujenzi, ukarabati na vifaa vingine vinavyohitajika.

MAWASILIANO:
Mwenyekiti: +255 766 029 345
Makamu Mwenyekiti: +255 757 686 331
Katibu Mkuu: +255 767 054 942
Naibu Katibu Mkuu: +255 688 899 652
Mtunza Hazina: +255 655 115 552

PUGU ALUMNI
Brother of the Nation, Sons of Legacy

Address

P. O. Box 9090
Dar Es Salaam
12112

Opening Hours

Monday 07:15 - 14:25
Tuesday 07:15 - 14:25
Wednesday 07:15 - 14:25
Thursday 07:15 - 14:25
Friday 07:15 - 11:15

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Pugu Boys Secondary and High School posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share

Category