04/04/2025
KIKAO CHA BODI YA 19 SHULE YETU ACT BUNDA GIRLS SECONDARY SCHOOL.
Mhashamu Baba Askofu Dr.George M Okoth ambae pia ni Mwenyekiti wa Bodi ya shule ameongoza kikao cha bodi kilichoketi shuleni hapo, kwa ajili ya kujadili mambo mbalimbali yanayohusu Maendeleo ya shule na taaluma ya wanafunzi wawapo shuleni hapo.
Mapema kabla ya kikao wajumbe wa bodi wametembelea miundombinu pamoja na miradi inayotekelezwa na shule ili kujiridhisha na huduma inayotolewa shuleni hapo.
Akifungua kikao hicho Mhashamu Baba Askofu ametoa hotuba yake kwa wajumbe kutoka katika kitabu cha samwel 1, 3:1-10 na ujumbe mkuu ukisisitiza wito katika utumishi (Walimu ni wito) Baba Askofu amewatia moyo walimu na kuwaombea kwa kazi kubwa wanayoifanya katika kutoa taaluma kwa wanafunzi.
Aidha Bodi imeadhimia kuboresha maslahi ya watumishi ili kuwatia moyo katika kazi wanayofanya .
Mkuu wa shule Bi Tupone Mwamasage ambae ni katibu wa Bodi ameshukuru wajumbe wa Bodi kwa kuendelea kufanya kazi kuisaidia shule kutimiza adhma yake ya kutoa elimu bora kwa wanafunzi na kuahidi kutoa huduma bora shuleni hapo ,pia ameshukuru shirika la Anglican Aid pamoja na Canon Helen Hoskins kutoka Australia kwa mchango mkubwa waliotoa katika maendeleo ya shule.
Mwenyekiti wa Bodi anawakaribisha wazazi na walezi wote kuwaleta watoto shuleni hapo kujiunga na masomo kuanzia kidato cha kwanza hadi cha Nne.
MUNGU IBARIKI BUNDA GIRLS ,MUNGU IBARIKI DM
04.04.2025