22/09/2022
Tambua kwamba *Mafanikio yetu* asilimia kubwa,
Yamejificha katika tabia tunazo fanya *kila siku,*
Ukiona mtu *amekuzidi* kwenye jambo fulani,
Basi ujue kuna tabia ambazo *anazo* wewe hauna.
Hivyo basi tabia zifuatazo,
Zitakusaidia sana kuwa katika list ya *top 20%,*
Ya Watu walio fanikiwa katika *field Yako.*
🉑 Kuwa na *Malengo.*
Malengo ya muda mrefu pamoja na malengo madogo madogo.
Malengo ni k**a muongozo katika maisha,
Usipo kuwa na muongozo maisha yatakuongoza.
🉑 Kuwa mtu wa *matokeo* zaidi.
Vipi utakua mtu wa matokeo?
➡️ *Pangilia* siku yako,
➡️ Thamini *muda* kuliko kitu chochote.
➡️ Kuwa na *vipaumbele*
➡️ Andika *mikakati* yako ya kila Siku.
➡️ *Jihamasishe* mwenyewe kufanya kazi kwa bidii,
Usisubiri mtu akuhamasishe.
➡️ Fikiria kuhusu malengo yako kila *unapo amka* na pindi unapo *enda kulala.*
🉑 Fikiria zaidi kuhusu *Watu,*
Kila unapo amka fikiria ni *thamani gani* ambayo,
Utapeleka kwa Watu au *wateja wako,*
Fikiria zaidi katika kutatua *matatizo* Yaliyopo katika jamii,
Mafanikio yapo katika *kutatua matatizo* ya watu.
🉑 Kuwa *Mwaminifu.*
Kuwa mwaminifu kwa *wateja wako* na *Watu* wanao kuzunguka kwa ujumla.
🉑 Kuwa na *Nidham binafsi,*
Kwa ufupi nidham
binafsi,
Ni Uwezo wa kufanya kile unacho paswa kufanya bila kusimamiwa na mtu,
Haijalishi *unakipenda* kitu hicho au *haukipendi,*
Kila biashara ina nidham binafsi Zake,
Inaweza kuwa *kujisomea* , *kujitangaza* n.k.
*