Al murabbi media

Al murabbi media

Share

Ushauri wa Malezi ya Kiislamu
Wazazi | Watoto | Vijana
Mafunzo ya kujenga kizazi bora

11/04/2026
07/04/2026

“Ukimlea mtoto kwa dunia tu, utampoteza akhera yake…
Lakini ukimlea kwa Akhera, dunia itamfuata bila kuitafuta.”

25/03/2026

✨️⚖️KESI YA KIHISTORIA DHIDI YA MITANDAO YA KIJAMII🌱
🗞📎🔨



Leo nimekutana na habari nzito sana kutoka Los Angeles, ambapo jopo la majaji limezikuta kampuni za teknolojia k**a Meta Platforms na YouTube na hatia ya kuchangia madhara ya afya ya akili kwa kijana mmoja.
Mahak**a imeziamuru kulipa fidia ya dola milioni 3, kutokana na kile kinachoitwa “addictive design” — yaani mifumo ya majukwaa inayomfanya mtumiaji akae muda mrefu bila kujitambua.
Hii si kesi ya kawaida. Wataalamu wanasema ni “landmark case” — kesi ya kihistoria ambayo inaweza kubadilisha kabisa namna kampuni za mitandao ya kijamii zinavyowajibishwa, hasa linapokuja suala la watoto na vijana.
❗ Swali la kujiuliza: Je, mitandao ya kijamii ni chombo tu cha mawasiliano, au imeanza kuwa hatari kwa afya ya akili zetu na watoto wetu?
Ni wakati wa sisi wazazi, walezi na jamii kwa ujumla: ✔️ Kufuatilia matumizi ya watoto ✔️ Kuweka mipaka ya muda wa kutumia simu ✔️ Kuelimisha kuhusu matumizi salama ya teknolojia
Teknolojia ni neema… lakini bila mipaka, inaweza kuwa mtihani.

03/03/2026

🌙 Makosa ya Wazazi Ramadhani ⚠️

🌱 Epuka kunafanya makosa haya kwa watoto wako ndani ya mwezi mtukufu wa Ramdhani ✨

Mwezi mtukufu wa Ramadhani ni fursa ya malezi bora kwa watoto. Hata hivyo, wazazi wengi wanakosa hatua muhimu:

1️⃣ Kutojumuisha Kiimani
Watoto wanakula sahur(daku) na iftar bila kuelewa dua na shukrani.
💡 Dondoo: Somesha dua fupi kabla ya kula. Fanya pamoja!

2️⃣ Kutozingatia Ratiba na Nidhamu
Hakuna schedule ya ibada, kusoma Qur’an, au muda wa kujifunza.
💡 Dondoo: Weka ratiba rahisi, rahisisha mtoto kufuata.

3️⃣ Kuzingatia Chakula Zaidi ya Malezi
Chakula kizuri, lakini mtoto haelewi maadili ya Ramadhani.
💡 Dondoo: Shirikisha mtoto kuandaa chakula, soma dua pamoja, fundisha shukrani.

4️⃣ Kutochukua Muda wa Familia
Iftar bila familia, hakuna hadithi za Kiislamu, hakuna mazungumzo ya malezi.
💡 Dondoo: Fanya iftar na familia, soma hadithi, uliza maoni ya mtoto.

5️⃣ Kudumisha Tabia Mbaya
Wazazi wanavumilia tabia mbaya bila kufundisha jinsi ya kurekebisha.
💡 Dondoo: Pongezi tabia njema, elezea adhabu kwa upendo, si hasira.

✨ Ramadhani si tu kufunga, bali kujenga tabia, kiimani na maadili

Want your school to be the top-listed School/college in Tripoli?

Click here to claim your Sponsored Listing.

Location

Website

Address


Tripoli