Harun Abdallah

Harun Abdallah Harun Abdallah
Email address :-
[email protected] Sunni - muslim

17/07/2026

POLISI WAUZINGIRA MSIKITI WA IJUMAA MAGOMENI NA KUZUA HALI YA HOFU NA TAHARUKI !

🇹🇿 Dar es Salam Tanzania // Jeshi la Polisi limeuzingira Msikiti wa Kichangani uliopo Magomeni, Dar es Salaam, hivi leo kufuatia taarifa zilizosambaa kwenye mitandao ya kijamii zikidai kuwa aliyekuwa Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Sheikh Walid Omari Kawambwa, angehudhuria Swala ya Ijumaa katika msikiti huo baada ya kusimamishwa na BAKWATA.

Swala ya Ijumaa imehudhuriwa na idadi kubwa ya waumini kuliko ilivyo kawaida, huku baadhi wakilazimika kuswali nje ya msikiti kutokana na ufinyu wa nafasi.

Baadhi ya waumini wamesema kuwa walikuwa wakisubiri kumuona Sheikh Walid au kusikia kauli yake kufuatia hatua za kinidhamu zilizochukuliwa dhidi yake.

Hata hivyo, Swala ya Ijumaa ilianza k**a ilivyopangwa saa 6:30 mchana bila uwepo wa Sheikh Walid, ambaye hakuongoza ibada wala kutoa hotuba.

Sheikh Walid alisimamishwa uongozi na Baraza la Ulamaa la BAKWATA pamoja na masheikh wengine wawili wa mikoa ya Singida na Kigoma kwa tuhuma za ukiukaji wa maadili.

Swali wanalojiuliza watu ni je, polisi wamekuja Kichangani kufanya kazi gani ?

Je, palikuepo uvunjifu wa amani au hali hatarishi ya kiusalama iliohitaji msaada wa polisi ? au je, lengo limekua kuwatia uoga tu waislamu ?

ALIEFAA KUMRITHI SHEIKH WALID NI SHEIKH UTHMAN MAALIM !🇹🇿 Zanzibar City, Zanzibar // Kuna wimbi la kuwavunjia mashekhe w...
17/07/2026

ALIEFAA KUMRITHI SHEIKH WALID NI SHEIKH UTHMAN MAALIM !

🇹🇿 Zanzibar City, Zanzibar // Kuna wimbi la kuwavunjia mashekhe wa kiislamu hadhi na hishma yao mbele ya macho ya umma.

Wimbi hili limemfuata Sheikh Nurudin Kishky , Mola akalizima

Kisha likamfuata Sheikh wetu Walid Alhad Kawambwa....

Shekhe aliebaki tunaemhofia ni Sheikh Uthman Maalim...

Huyu msimguseni na ovu kwa ihsani yenu.

Aidha kwa ilmu aliokua nayo, huyu ndie Shekhe aliefaa kupewa nafasi ya Shekhe Mkuu wa mkoa wa Dar es Salam baada ya Sheikh Walid kuvuliwa wadhifa huo.

Sheikh Uthman ana uwezo na tajriba kubwa mno kuwaweka watu wote pamoja na kuleta mwafaka baina ya madhehebu yote na dini tofauti......

Mwishoni mwa miaka ya 70, Sheikh Abdallah Swaleh Alfarsy ambae ni raia wa Zanzibar na kadhi mkuu wa Zanzibar nyakati zile alipewa wadhifa wa Kadhi mkuu wa Kenya na serikali ya Kenya na akaushikilia kwa msaada mkubwa wa Kenya

Ni vyema tukakumbuka hili nalo

Nani ananiunga mkono kwa hili ?

Twamuomba Mwenyeezi Mungu amhifadhi Shekhe huyu na kumwepusha na kila wenye niyyah mbaya

Amiin 🤲

HOSPITALI KUU YA MKOA WA MAWENI YAMTESA MTOTO KWA KUMZUILIA HOSPITALINI  MIEZI TISA !!!🇹🇿  Kigoma, Tanzania // Hospitali...
17/07/2026

HOSPITALI KUU YA MKOA WA MAWENI YAMTESA MTOTO KWA KUMZUILIA HOSPITALINI MIEZI TISA !!!

🇹🇿 Kigoma, Tanzania // Hospitali kuu ya mkoa wa Maweni inamtesa kiakili na kisaikolojia mama na mwanawe

Khadija Ramadhani Idd, mkazi wa Kitongoji cha Lugongoni A, Kata ya Nguruka, Mkoa wa Kigoma, ameomba msaada kutoka kwa wasamaria wema ili aweze kulipa deni la matibabu linalomzuia kumchukua mtoto wake ambaye bado amelazwa katika Hospitali ya Mkoa wa Maweni.

Kwa mujibu wa mama Khadija, changamoto zake zilianza mwezi Oktoba 2025 aliposhikwa na uchungu wa kujifungua kabla ya muda akiwa na ujauzito wa miezi saba. Baada ya kupatiwa huduma katika Kituo cha Afya Nguruka, alipewa rufaa kwenda Hospitali ya Mkoa wa Maweni, ambako alijifungua mtoto njiti kwa msaada wa madaktari.

Amesema baada ya kujifungua hali yake ya afya ilizorota na kufanyiwa vipimo vilivyobaini kuwa figo na mapafu yake vilikuwa vimeathirika. Kutokana na hali hiyo, alipelekwa kwa rufaa katika Hospitali ya Bugando kwa matibabu ya kibingwa, ambako alipatiwa huduma hadi aliporuhusiwa kurejea nyumbani mwezi Februari 2026 baada ya afya yake kuimarika.

Hata hivyo, licha ya mama huyo kupona, mtoto wake ameendelea kubaki Hospitali ya Mkoa wa Maweni tangu kuzaliwa kutokana na deni la matibabu la **Shilingi 336,600**, ambalo familia imeshindwa kulimudu.

Mama Khadija amesema bado anakabiliwa na changamoto za kiafya na kifedha. Aidha, amesema hana wazazi wa kumsaidia na mzazi mwenzake hajulikani alipo, hali iliyomfanya ashindwe kupata fedha za kulipa deni hilo na kumchukua mtoto wake hospitalini.

Kutokana na hali hiyo, mama huyo ametoa wito kwa Watanzania, taasisi za kijamii na wasamaria wema kujitokeza kumsaidia ili aweze kulipa deni hilo na kuungana tena na mtoto wake baada ya miezi kadhaa ya kutengana.

Mawasiliano kwa ajili ya msaada:

Jina:Asha Ramadhani Idd

Simu:0785 971 755

CRIME ESCALATES IN SOUTH AFRICA AS WOMAN SHOT DEAD IN EAST LONDON STREET, 🇿🇦  East London, South Africa // South African...
17/07/2026

CRIME ESCALATES IN SOUTH AFRICA AS WOMAN SHOT DEAD IN EAST LONDON STREET,

🇿🇦 East London, South Africa // South African lady named Anda "Peach" Mlondleni was fatally shot multiple times, just outside Mrhawu Holdings in Berea .

Mlondleni had joined the company in June 2024. She was suspended on July 1, 2026, pending a disciplinary hearing that was held the next day before an external chairperson. No outcome from the hearing had been communicated to her.

On July 13, she was called to the office for an 11:00 a.m. meeting. She arrived around that time and, at approximately 11:20 a.m., phoned her sister to say the meeting had finished and she was ready to be picked up.

Shortly after leaving the company premises, she was shot. Witnesses reported hearing her cry out after the first gunshot, while others saw a man with his face covered carrying what appeared to be a firearm in the area shortly before the shooting.

Her family has called for a transparent, thorough, and impartial investigation into the circumstances of her death.

Deadly crime is still being reported in South Africa despite successful deportation of immigrants from South Africa

March and March movement under Jacinta Ngombese Zuma had earlier blamed immigrants for crime

The movement said, illegal immigrants are people responsible for crime being committed in South Africa

We are asking just for clarification..... who is committing crime in south Africa after immigrants have left the country. ?

MSIKITI WA IJUMAA KICHANGANI DAR ES SALAAM UNA SIKILIZWA NCHI NZIMA HIVI LEO🇹🇿 Dar es Salam, Tanzania // Maelfu ya waisl...
17/07/2026

MSIKITI WA IJUMAA KICHANGANI DAR ES SALAAM UNA SIKILIZWA NCHI NZIMA HIVI LEO

🇹🇿 Dar es Salam, Tanzania // Maelfu ya waislamu wanatarajiwa kuhudhuria Salah ya Ijumaa ya kwanza ya mwezi Swafar hii leo katika msikiti wa ijumaa Kichangani Dar es Salam.

Idadi hiyo kubwa ya waumini wakiwemo vijana wa Magomeni hatimae watafanya maandamano mafupi na kuzungumza na wanahabari kuelezea hisia zao

Msikiti huo ambao khatibu wake na Imam NI Sheikh Walid Alhad Kawambwa aliekua Shekhe Mkuu wa mkoa wa Dar es Salam ni msikiti utakaoangaziwa sana hivi leo nchini Tanzania na duniani kote hasa jamii za watanzania wanaoishi Marekani, ulaya, bara arabuni na nchi tofauti za afrika

Waandishi wa vyombo tofauti vya habari wanaelekea Kichangani hivi sasa

Vijana wa Dar es Salam wamesema wataujaza msikiti huo hadi barabarani hivi leo

Idadi kubwa ya waumini wakiwemo wanahabari wanafuatilia kusikia atakayoyasema Sheikh Walid Alhad kwa mara ya kwanza tangu avuliwe cheo cha Sheikh Mkuu wa mkoa wa Dar es Salam na kadhia ya fitna inayomwandama.

Wengi wa wanahabari wanainyemelea fursa ya mahojiano baada ya Salah kumhohi Sheikh Walid.

CHETI HALALI CHA NIKAHA KATI YA SHEIKH WALID NA BELLA CHAONEKANA !🇹🇿  Dar es Salam, Tanzania //  Cheti cha ndoa ya halal...
16/07/2026

CHETI HALALI CHA NIKAHA KATI YA SHEIKH WALID NA BELLA CHAONEKANA !

🇹🇿 Dar es Salam, Tanzania // Cheti cha ndoa ya halali kati ya Sheikh Walid na mtalikiwa wake dada Bella kimepatikana .

Cheti Hicho kinamrejeshea hishma Sheikh Walid na kumwondolea lawama zilizoibuka mitandaoni kuhusu hishma ya Sheikh.....lawama zilizopelekea yeye kuvuliwa cheo chake cha Shekhe Mkuu wa mkoa wa Dar es Salam

Kwa mjibu wa cheti hicho, Sheikh Walid alimuoa mwanamke huyo kisheria na katika taratibu za Kiislamu tarehe 16-10-2024, ila alimtaliki baada ya miezi 3

Utata upo kwenye uhalisia wa mtoto...ambapo mwanamke huyo anadai ni damu ya Sheikh.....lakini Sheikh anapinga hilo na kusema mtoto huyo hatokani na yeye.

Sheikh amesisitiza lazima vipimo vya DNA/ vifanywe kubaini k**a kweli mtoto huyo ni damu yake, ila mwanamke huyo amekataa jambo hilo

Waraka huu wa nikaha utawaaibisha watu wanaotumia mitandao ya kijamii hasa tiktok, facebook na YouTube kumpaka tope Sheikh kuwa alienda kinyume na maadili

Cheti hiki aidha kimeiletea fedheha kuu Bakwata.

Waislamu wote nchini Tanzania wanaamini kuwa ugomvi wa mwanamke huyu na Sheikh ndio uliopekekea Bakwata kumvua cheo cha Sheikh Mkuu wa mkoa, Shekhe Walid.

Sasa ni wazi kuwa Sheikh hakufanya uchafu na mwanamke huyo....alikua mkewe wa halali

Hivyo wanaotumia mitandao ya kijamii kumtia doa Sheikh Walid... tafadhali, komeni, Sheikh ni msafi k**a pamba

La zaidi mumuombe msamaha na maghfirah Mola wenu kwa kumchafulia jina na kumtuhumu vibaya na kumtia aibu Sheikh huyo.

Bella pia ni dada yetu mwislamu - anazo haki zake - lakini- amekosea kupeleka ugomvi huo mitandaoni.

Madhara yake yamekua makubwa kuliko faida yake

Angeendelea tu kutafuta haki kupitia vyombo vya sheria ila sio kuileta kadhia hii mitandaoni

Mimi binafsi nimeiona video yake akikana kuwa hakua ameolewa na Sheikh kisheria....walikua washikaji tu

Huu ni uongo !!

kausema tu ili amzalilishe Sheikh na kumtia aibu machoni mwa watanzania..

Ukweli ni kwamba huyu mwanamke ana hasira moyoni...

anayafanya haya makusudi k**a njia muwafaka kwake yeye kumpiga vita Sheikh, na kulipiza kisasi cha kutalikiwa.

Sababu ni kuwa...Sheikh alipomtaliki huyu dada hakuwa tayari kutalikiwa, alikua hataki atalikiwe...!!

Amesikika wazi wazi akisema bado anampenda Sheikh, ila Sheikh aliharakisha kumtaliki.....

Lakini yote tisa, kumi ndugu zangu watanzania....tuchungeni hishma ya Sheikh na dada huyo....kwani wote wawili Wana hasira hivi sasa

Sheikh amejizuia mno kuzungumzia kadhia hii na pia kumjibu dada huyo, ila eleweni dada huyo si msomi....anaweza kusema lolote au kuzua lolote muradi tu Sheikh apate aibu mbele ya watu

Hapa tunatazama haki mbili

1 - Haki ya Sheikh pamoja na kuilinda na kuchunga hishma yake, na huo ni wajibu wetu wa lazima katika kidini

2 - Kuichunga haki na hishma ya dada huyo hasa kwa kuzingatiwa ni mwislamu mwenzetu , tena amesilimu tu kutoka dini ya ukristo kwa ajili ya kuupenda uislamu

Dada huyo ana haki alindwe na kuhifadhiwa na waislamu wala si kuzomwa

Kwa hilo, hii ni kadhia ya mme na mke iliovuja na kuingia mitandaoni tu

Tusichukue mirengo mikali juu ya kadhia hii

Wallahi tumebanwa katikati ya haki mbili kuu mbele ya Mwenyeezi Mungu SWT

Mimi hapa naogopa tayari, hii kadhia nzito

Tumieni hikma sana tusijeni kutumbukizwa motoni kwa ajili ya kadhia hii, epukane sana jambo hili.

Tusitumieni mitandao ya kijamii kueneza habari za uongo kuwahusu, au kuwadhalilisha

Kwa sasa, wote wawili wanahitaji huruma na msaada wetu.

Tuwasitirini tu. 🙏🙏

Jamani waislamu, comment neno " Astaghfirullah ....! " ni Bora zaidi..... Afwan 🙏

16/07/2026

AFISA POLISI WA KENYA AJUTIA KADHIA YA KUEPULIWA IMAM MKUU WA MKOA WA DAR ES SALAAM !

🇰🇪 Mombasa Kenya // Afisa polisi mmoja mwislamu wa Kenya ametoa video akijutia kadhia ya kubanduliwa imam mkuu wa mkoa wa Dar es Salam Sheikh Walid Alhad Kawambwa, aliempenda sana na kufuatilia darasa zake mitandaoni.

16/07/2026

Mwanajeshi wa jeshi la kupambana na moto la Tanzania mkoani Dar es Salam akitufunza vipi tuuzime moto unapozuka katika mtungi wa gasi

Muslim Sisters Association, Lusaka, Zambia
16/07/2026

Muslim Sisters Association, Lusaka, Zambia

RATIBA YA UCHAGUZI MKUU BAKWATA 2026 NGAZI YA WILAYA NA MKOA.🇹🇿  Dar es Salam, Tanzania //  Baada ya kukamilika uchaguzi...
16/07/2026

RATIBA YA UCHAGUZI MKUU BAKWATA 2026 NGAZI YA WILAYA NA MKOA.

🇹🇿 Dar es Salam, Tanzania // Baada ya kukamilika uchaguzi wa BAKWATA na JUWAKITA pamoja na JUVIKIBA ya msikiti na kata sasa macho na masikio ya waislamu yameelekea uchaguzi

RATIBA YA UCHAGUZI WA BAKWATA NGAZI YA WILAYA

♦️Kuchukua fomu - 16.7.2026
♦️Kurudisha fomu - 20.7.2026
♦️Kupitisha majina - 22.7.2026
♦️Siku ya uchaguzi - 25.7.2026

RATIBA YA UCHAGUZI WA BAKWATA NGAZI YA MKOA

♦️Kuchukua fomu - 27.7.2026
♦️Kurudisha fomu - 30.7.2026
♦️Kupitisha majina - 2.8..2026
♦️Siku ya uchaguzi - 16.8.2026

🛑 UCHAGUZI WA JUVIKIBA NA JUWAKITA.

UCHAGUZI WA JUVIKIBA NA JUWAKITA NGAZI YA WILAYA

♦️Kuchukua fomu - 9.7.2026
♦️Kurudisha fomu - 15.7.2026
♦️Kuchuja wagombea - 16.7.2026
♦️Siku ya uchaguzi - 19.7.2026

UCHAGUZI WA JUVIKIBA NA JUWAKITA NGAZI YA MKOA

♦️Kuchukua fomu - 22.7.2026
♦️Kurudisha fomu - 28.7.2026
♦️Kuchuja wagombea - 30.7.2026
♦️Siku ya uchaguzi - 2.8.2026

Address

+255
Nairobi

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Harun Abdallah posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share