Mwongozo tumbo lisilo shiba

Mwongozo tumbo lisilo shiba

Share

Pata mwongozo wa hadithi zote za tumbo lisilo shiba

04/01/2022

WAHUSIKA

Mzee Mago

Ni mzee anayemiliki mkahawa mshenzi. Watu huja mkahawani kunywa chai na kuzungumzia mambo muhimu yanayowahusu. Anahusika katika kutetea haki za wanyonge.

· Umuhimu: kielelezo cha watu wanaotetea haki za wanyonge katika jamii;

· Mpenda haki/mtetezi - hakupuuza ule uvumi bali alijaribu kuutafutia suluhisho.

· Mwenye bidii - shughuli ya kupigania na kuzuia mipango ya watu wakubwa sio rahisi. Ilibidi mzee Mago ajinyime, awatafute wenzake wazungumze na kulijadili jambo hili ambalo lilikuwa nyeti sana kwao.

· Mshawishi - aliwashawishi wanyonge wenzake watafute wanasheria waaminifu ili wasaidie kufafanua vipengele vigumu vya sheria k**a njia ya kuwavukisha vikwazo ili wapate suluhisho.

· Mzinduzi - aliwazindua wenzake na kuwapa nasaha kuhusu maendeleo. Aliwazindua kwamba maendeleo yanahitaji mchango wa kila mtu - wa k**e kwa wa kiume, wadogo kwa wakubwa n.k. Aidha, aliwatahadharisha kwamba wachunguze ni maendeleo gani yatakayowanufaisha.

· Mzalendo – anawanasibi wananchi wenzake wakubali maendleo yanayopiga hatua nchini mwao.

· Mwoga – anajawawa na wasiwasi anapozungumza na jitu lilokuja mkahawani (uk. 7).



Kabwe

Ni mmoja wa wenyeji wa Madongoporomoka. Tunampata mkahawani akifanya mazungumzo na kina Mago.

· Mshirika - alishirikianana wanyongewenzake katika kutafuta ufumbuzi wa kunyakuliwa kwa ardhi yao.

· Mtumainifu - anaamini kuwa sheria inaweza kuwa suluhisho la matatizo yao.

· Mpenda amani na haki - alitaka watafute suluhisho linalofaa kwa watu wa Madongoporomoka.

Bi. Suruta

· Ni hodari katikakutoahojakwenye mashauriano. Anawapiku wanaume wote.

Bi. Fambo

· Mwanamke mojawapo wa wanyonge.

· Ni mwelewa masuala ya unyanyasaji.

· Anaeleza bayana kwamba wakubwa hawajali wanyonge wakihamishwa kwenye ardhi watakwenda wapi.

Jitu la miraba minne

Ni jitu linalokuja mkahawani kula.

· Kubwa – ni dovu la mtu; lina shingo

04/01/2022

MAUDHUI

Ukatili/Dhuluma

· Wakazi wa Madongoporomoka wananyanganywa ardhi yao. Tabaka la mabwanyenye linawatoa katika ardhi yao na kuwavunjia vibanda vyao pasipo hata kuwalipa fidia.

Utabaka

· Hadithi hii inasawiri kuwapo kwa matabaka katika jamii. Kuna tabaka la mabwanyeye na tabaka la wanyonge. Tabaka la mabwanyenye linaendesha dhuluma dhidi ya wanyonge.

· Jitu kubwa linaonekana likisimamia shughuli ya ubomoaji wa vibanda vya wakazi wa Madongoporomoka. Tabaka hilo la mabwanyeye linatumia vyombo vya dola k**a askari wa baraza la mji na askari polisi katika kuwakandamiza wanyonge.

Ukosefu wa Haki

· Katika jamii iliyojaa dhuluma hakuna haki. Watu wa Madongoporomoka wanaporwa haki yao ya kumiliki ardhi. Ardhi inatwaliwa na wenye nacho.

· Wanaposhauriana kutafuta wanasheria waaminifu bado wanashindwa kuwapata. Wanasheria wamezibwa midomo kwa fedha za mabwanyenye.

Umoja na Mshik**ano

· Wakazi wa Madongoporomoka wanaapa kuwa fujo hazitasaidia.

· Baada ya wiki tatu za fujo hiyo, wanaungana na kurejesha vibanda vyao.

04/01/2022

Hadithi hii imepewa kichwa ambacho kinasadifu Yale yaliyomo. Wananchi wa Madongoporomoka walisikia uvumi kwamba kulikuwa na mpango wa kubomoa makao yao ili kutoa nafasi ya upanuzi wa jiji. Walijadiliana mara kwa mara wakiwa katika mkahawa mshenzi wa kiongozi wao Mzee Mago. Walijadili nini? Walitaka wapate suluhisho ili kujiauni na janga hilo, hawakuwa na makao mengine.

1. Wakiwa katika mgahawa huo wanaagiza vyakula mbalimbali. Linatokea jitu moja kubwa likatoa agizo kwamba lipewe vyakula vyote vilivyokuwa vimeandaliwa wateja wengine. Lilitishia kwamba wapende wasipende angejitwalia vyakula hivyo.

2. Jitu lilikula aina zote za vyakula na kunywa chupa kadhaa za soda. Mwishowe lililipa na kuahidi kwamba lingehitaji chakula mara mbili zaidi kesho yake. Siku iliyofuata, lile jitu litifika kuja 'kula ardhi' ya Madongoporomoka. Lile tumbo halishibi si chakula tu, bali rasilimali za raia k**a ardhi.

3. Tumbo lisiloshiba husimamia wenye mamlaka ambao hawatosheki —wanamiliki mali nyingi lakini bado wanahitaji kumiliki kite kidogo walicho nacho wanyonge. Usasa na maendeleo yameleta ahueni kwa wananchi wachochole au yamezidisha unyanyasaji?

Hadithi hii pia imepewa kichwa ambacho kinasadifu yaliyomo.

1. Wakiwa katika mkahawa wa Mzee Mago linatokea jitu moja kubwa likatoa agizo kwamba lipewe vyakula vyote vilivyokuwa vimeandaliwa wateja wengine. Jitu lilikula aina zote za vyakula na kunywa chupa kadhaa za soda. Mwishowe lililipa na kuahidi kwamba lingehitaji chakula mara mbili zaidi kesho yake.

2. Siku iliyofuata, lile jitu lilifika kuja 'kula ardhi' ya Madongoporomoka. Lile tumbo lake halishibi si chakula tu, bali rasilimali za raia k**a ardhi.

3. Wawekezaji wa jiji wanajenga majengo mengi hadi wanakosa kuacha nafasi ya mtu kuvuta pumzi. Hawatosheki (uk. 4).

Tanbihi: Tumbo lisiloshiba husimamia wenye mamlaka ambao hawatosheki - wanamiliki mali nyingi lakini bado wanahitaji kumiliki kile kidogo walicho nacho wanyonge.

DHAMIRA

• Mwandishi amedhamiria kuonesha namna tabaka la juu linavyokandamiza haki za wanyonge. Tabaka hili linajilimbikizia mali na kutwaa rasilimali za wanyonge bila kushiba.

12/12/2021

Hadithi inaanza kwa taharuki kuhusu uvumi uliogeuka mnong'ono ukaeneza wasiwasi-hofu. Wasiwasi ulikuwa vibanda vitabomolewa vote. Watu wakubwa walitaka kuchukua makao ya watu ili kuendeleza ujenzi wao. Kwa Mzee Mago ndiko kituo cha kuzungumzia juu ya haki zao. Yeye huwakusanya wenzake iii wajadili juu ya haki zao za kuishi pale wanapochagua. Wanahojiana mambo juu ya:

1. Kustahili kuishi kwa amani na furaha popote nchini mwao.

2. Namna ya kuruka vikwazo vya sheria vilivyowekwa ili watu wadogo wasiweze kupoteza mali zao.

3. Kushawishiana watafute wanasheria waaminifu iii kutatua (mazonge ya sheria). Wanadai kuwa wanasheria waaminifu wameadimika — Bhakuna haki siku hizi.

4. Kunasihiana na kuamshana juu ya kukubali maendeleo yanayopiga kasi nchini mwao.

5. Maendeleo yanahitaji mchango wa kila mtu — mdogo kwa mkubwa, wa k**e kwa wa kiume.



Mtu hawezi kukimbia ukweli, upya na usasa hutazamiwa kuleta mafanikio kwa watu wote. Mzee Mago huwaonya wauchunguze huo upya na usasa waujue jmst uhvyokaa —utaleta faida au hasara. Umaskini sio ujinga. Watu maskini wangeshauriwa wangeweza kuonyesha watakavyochangia maendeleo ya nchi yao. Watu wadogo hukasirika kwani wao hufanywa kuwa k**a takataka. Hasira yao ndiyo inayowapa motisha wa kusema na kujitetea. Wakubwa walidai kuwa jiji limejaa na halina nafasi tena, suluhisho ni kubomoa baadhi ya mitaa. Jiji limejaa hoteli, mikahawa, majumba ya Mall, maduka n k. Kwa hiyo, suluhisho la uhaba wa nafasi jijini ni kubomoa sehemu zingine.



Mzee Mago aliwaleta wenzake pamoja kupigania haki za hapo Madongoporomoka —pasibomolewe.

Baadhi ya wanyonge hawa wanataka wapewe visenti vyao vichache vaondoke. Wengine wanadai, hakuna kuondoka. Wanataka vvabaki pale pale na kupigania haki zao. Kabwe alisisitiza kwa nguvu kuwa wakubwa hawataweza, kwani wanaogopa umma wa Madongoporomoka. Bi. Suruta aliwatahadharisha kuwa wakubwa hawaogopi kitu chochote.



Wakati mjadala ukiendelea, chakula cha pale mga

Want your school to be the top-listed School/college in Nairobi West?

Click here to claim your Sponsored Listing.

Location

Category

Website

Address


Nairobi West