Inspirational page

Inspirational page

Share

Njoo umepata mwaidha chungu nzima.

15/12/2021

Chimbuko la Kiswahili.
Ni kufafanua namna Kiswahili kilivyoanza. Asili ya Kiswahili.
Taja nadharia tatu zinazoeleza chimbuko la kiswahili.
i. Kuwa Kiswahili ni lugha ya mseto.
Kiswahili ni tukio la maingiliano ya kibiashara, kijamii na hata kindoa baina ya wenyeji wa
Pwani na Waarabu.
Ø Haja ya Waarabu kuwasiliana na watumwa wao wa Kibantu ilisababisha kuchanganya
kwa maneno ya lugha za Kibantu na yale ya Kiarabu ili waweze kuelewana na hivyo
lugha lugha iliyochipuka ikawa ya Kiswahili(mchanganyiko wa Kibantu na Kiarabu.
Ø Shughuli za kibiashara-Waarabu walipofika kwa shughuli hizi hawakufika na wake zao
hivyo kulikuwa na uhaba wa wanawake wa Kiarabu hivyo wakaanza kufunga ndoa na
wanawake Waafrika na kupata watoto waliojifunza Kiarabu na Kibantu na lugha
iliyozungumzwa ikawa Kiswahili(lugha chotara-mchanganyiko wa Kiswahili na
Kibantu).
ii. Kuwa Kiswahili ni lahaja ya Kiarabu.
Ø Kuna idadi kubwa ya msamiati wa kiarabu katika kiswahili.
§ Ghadhabu – hasira.
§ Nadra -chache.
§ Tisa - kenda.
§ daima – milele.
Ø Lugha ya kiswahili imefungama sana na mafunzo ya dini ya Kislamu (ambayo ililetwa na
Waarabu toka Uarabuni). Vile vile miongoni mwa wale wanaojiita Waswahili ni wafuasi
wa dini ya Kislamu. Wao hutumia majina ya Kislamu k**a vile Mohammed, Rehema,
Ramadhan n.k.
Ø Nyimbo za taarab hapo awali zilikuwa zikiimbwa kwa mashairi ya kiarabu na baadaye
zikaanza kuimbwa kwa mashairi ya Kiswahili.
iii. Kuwa Kiswahili ni lugha ya Kiafrika yenye asili ya kibantu.
Mtazamo hushikiliwa na wengi. Unashikilia kwamba Kiswahili ni Kibantuk**a vile
Kikamba, Kizulu, Kiganda n,k.
Tetea kauli kwamba Kiswahili ni kibantu.
Ø Maumbo ya maneno kwa Kiswahili na lugha za kibantu yana viambishi.
k.m mu-ndu.
m-tu
Ø Kuna mfanano wa kimsamiati katika lugha ya Kiswahili na lugha za Kibantu.
k.m kuhoa, korora, kooa.
Ulimi.lulimi
Ø Lugha ya Kiswahili mara nyingi huwa na muundo wa silabi wazi/huru. Mfumo huu vile
vile hudhihirika katika lugha nyingi za Kibantu.
Kikombe/shikombe.
Kitabu/sh*tapu.
Ø No

14/08/2021

Siku njema wakenya

03/12/2020

ASILi YA KISWAHILI
Neno Swahili lina asili ya Kiarabu: Sahil ina maana ya pwani; sawahil ’’as-sawāhilī’’ ni wingi wake kwa kumaanisha yote yanayohusiana na pwani, watu au utamaduni wa eneo la pwani.

Mwanzo katika miji ya pwani
Kiswahili kilianza k**a lugha ya miji na mabandari ya biashara ya kimataifa kwenye pwani ya Afrika ya mashariki.

Tuna historia jinsi gani miji k**a vile Kilwa, Lamu na mingine kadhaa ilianzishwa na wafanyabiashara Waarabu waliooa wenyeji. Idadi ya wahamiaji kutoka Uarabuni haikuwa kubwa sana, hivyo lugha ya wenyeji ilitumika kila mahali ila tu maneno mengi yameingia kutoka Kiarabu. Kwa ujumla Kiswahili kina maneno yenye asili ya Kiarabu kati ya 30-40%

01/12/2020

Tofauti baina ya kiswahili na swshili:
Kwa nini baadhi ya watu wanasema "Swahili" na wengine wanasema "Kiswahili," na neno lipi ni sahihi? Nini maana ya "Ki" katika "Kiswahili?" Kwa nini baadhi wanaandika "Kiswahili" na wengine wanaandika "KiSwahili" kwa kuifanya "S" katikati ya neno hilo kuwa kubwa? " Ufafanuzi wake ni rahisi: "Swahili" ni istilahi ya Kiingereza kwa maana ya lugha ya Kiswahili, wakati "Kiswahili" ni istilahi inayotumiwa kumaanisha lugha ya Kiswahili kwa lugha ya Kiswahili. Tunapoandika kwa lugha ya Kiingereza tunatumia neno "Swahili" na tunapoandika kwa Kiswahili tunatumia "Kiswahili. Kiambishi "k" kinachotangulia neno la kiswahili linaashiria shina linalofuata ni jina la lugha; kwa mfano lugha ya kiswahili, kifaransa n.k.
Kwa kurejelea silabi "s" iliyoandikwa kwa herufi kubwa katika neno la kiswahili ni swali lililotia tatizo sugu. Kwa kwaida maneno ya kiswahili ni kiambishi cha awali pekee huandikwa kwa herufi kubwa.

Want your school to be the top-listed School/college in Kilimani?

Click here to claim your Sponsored Listing.

Location

Category

Telephone

Website

Address


Kilimani