Fasihi Kwa Shule Za Upili

Fasihi Kwa Shule Za Upili

Share

kujifunza lugha na fasihi kwa ajili ya matayarisho wa mtihani wa kitaifa

30/05/2024

Taashira Katika ndoto ya Mangwasga.

Jinyama kubwa ni ishara ya viongozi wanaowakandamiza wanyonge
Jinyama jeusi ni ishara ya viongozi waliojaa maovu
Jinyama kutoa sauti k**a radi ni ishara ya mamlaka ya viongozi
Ulimi mrefu mwekundu ni ishara ya tamaa ya viongozi
Mangwasha alikimbia lakini mkimbio wake ukatatizwa na nguvu isiyoeleweka ni ishara ya vikwazo vinavyowekewa wanyonge ili wasipate haki
Moto uliotoa miale mikali ni moto ambao ungewachomea watu wa matango nyumba
Moto kuwaka bila moshi ni kuwachoeawaketwa nyumba bila hatia
Noti za elfu ni vishawishi vya Lesulia na Sagilu
Jinga la moto ni mbinu ambazo wanyonge wanatumia kujikomboa

23/05/2024

Maelezo mseto kuhusu mbinu ya Taswira.

Taswira ni picha inayojengeka akilini mwa msomaji au msikilizaji wa kazi anuai za fasihi.

Kuna aina tofauti tofauti za taswira. Ni K**a vile:

1.Taswira oni –inajitokeza unapopewa picha ya mahali, mtu, kitu au hali na dhana tofauti .
Mathalan:
Halima amejikunyata kwenye kochi.
Picha nzuri zimetundikwa ukutani.
Moto mkubwa uliteketeza makao yao.

2.Taswira sikivu-hapa unawahi picha akilini kwa kigezo cha kusikia kwa masikio .
Mathalan:
Malenga mteule akikariri shairi kwenye Msiba wa Kujitakia.
Mangwasha anasikia sauti za wakimbizi wengine nje ya kanisa.

3.Taswira mwonjo-aghalabu huhusishwa na picha dhanaifu ya kima fulani k**a ulaji wa milo au viambata au chochote cha ladha fulani kwa kutumia ulimi.
Mathalan.
Jasho lake lilikuwa sawa na chumvi nilipompa pambaja.
Chakula hichi ni asali.

4.Taswira mnuso – ni picha inayokuzwa kwa uwezo wa pua zinapobainisha harufu za namna fulani.
Mathalan:
Mitungi ya gesi ya plastiki ilichomeka na harufu kutapakaa kila mahali.
Tulihisi mapishi yenyu ya mahamri tukiwa bustanini.

5.Taswira hisi – huegemea hisia za wastani za binadamu k**a vile huruma, hasira, furaha,huzuni, jazba na kadhalika.
Mathalan:
Njaa ilimkeketa matumbo na kumdhoofisha kabla ya kuzirai.
Mgonjwa alighuna kwa uchungu mkubwa.
Kumbuka: Taswira zaidi ya moja zinaweza kuwa kwa kauli moja.

6.Taswira Mguso – msomaji huwahi hisia za kuguswa kwa viganja vya mkono au mikono au vitu visio hai ilivyo kawaida tu kwa hali tofauti.
Mathalan:
Halima alimpapasa Ali na kumlaza kitandani taratibu.
7. Taswira mwendo- aghalabu huhusisha kubadili makao kwa mtu, kiumbe mwingine au kitu.
Aghalabu hujenga Taswira oni moja kwa moja.
Mathalani:
Halima alisimama na kuelekea pembezoni mwa bahari k**a malaika.
Tawi lilininginia kwa madaha kisha kuyumbishwa ghafla kabla ya kuangoka na kuanguka chini.

Ubainifu wa Taswira katika ushairi na kazi zingine huweza kuchimuzwa kwa mbinu hizi za lugha:

Takriri au urudiaji ainati-neno au muundo(usambamba)
Kwa mfano:
Walisima k**a kigingi cha umeme kwa hofu. Hofu ya kutojua kesho. Hofu ya kutojua mgeni wao usiku huo alileta zawadi gani. Hofu ya kutojua nina wao yu wapi.

Tashbihi.
Kwa mfano:
Yerimina amesimama wima sawa na jenerali.
Istiara.
Kwa mfano :
Maisha ni bembea.

Jazanda.
Kwa mfano:
Ndoa ni bembea.
Dunia ni mtihani mkuu. Hamna aliyefuzu stashahada hii mia fi mia.
Naomba mnoe maelezo haya na myajaze zaidi yawe mkufu wa kuvishwa wanagenzi na wakufunzi ili sote tufanikishe jahazi la elimu. Shukran.

23/05/2022

Kwa wanafunzi wa kidato cha pili na tatu. Ikumbukwe kuwa kwa wanafunzi wa kidato cha tatu wa mwaka huu watafanya Riwaya ya Chozi la Heri Wala si Nguu za Jadi.

23/02/2022
Photos from Fasihi Kwa Shule Za Upili's post 13/02/2022

Jumuiya ya Afrika imeunga mkono kwa kauli moja Kiswahili kutumika K**a mojawapo wa lugha rasmi katika mikutano na shughuli za Jumuiya hiyo. Kiswahili Tukienzi.

31/01/2022

Maudhui ya ukoloni Mamboleo katika Chozi la Heri
-Baada ya miaka kumi ya Uhuru tumebaki kuwa wategemezi wakoloni hao hao walitupa Uhuru.
-Wanapoondika Wakoloni walowezi na Waafrika uwezo walimiliki mashamba yaliokuwa ya wakolini na kufanya kuwa maskwota katika usuli wao.
-Waliokuwa wakoloni ndio wanaoamua Waafrika watakuza nini katika ardhi yao.
-Waafrika wanaendelea kuwategemea wakoloni kwa lishe na ajira ambayo ni ya kijunguku jiko.
-Kampuni za kigeni zimewapa wenyeji ajira zenye mshahara mdogo.
-Viongozi wa Kiafrika wanaendeleza ukoloni katili ambaoo wanawaua vijana wa Kiafrika wanaojaribu kujikomboa.
-Waafrika wanapewa mahindi ya msaada kupunguza makali ya njaa.
-Vito na hazina za mafuta zimepewa kampuni za kibinafsi ambazo ni za kigeni na pesa zinazopatikana zinaishia katika mataifa ya kigeni.

11/10/2021

Mwandishi wa Hadithi Tumbo lisiloshiba amedhihirisha kuwa katika jamii Kuna Makabila mawili , walahohoi na walala heri. Walalaheri ,watu wenye vyeo K**a Mzee Mambo anawalaghai raia kuwa anawafanyia kazi ilhali ni waziri kivuli ambaye hujui afanyalo katika wizara hio. Anatumia magari ya serikali katika shuguli za kibinafsi na kutumia ruinga ya kitaifa kupeperusha sherehe za wanawe wawili, mmoja kwa sababu ameota jino moja na mwingine kujunga na Shule ya chekechea. Walalahoi hata hawana habari kuwa wanawindwa na hela zao wanazolipia ushuru zinapokwa, wamefika kwa wingi katika sherehe huku wakicheza nyimbo za bezo K**a vile "Mungu humpa amtakaye " wako live katika fesibuku na watisapu wakiwa na furaha kedede. DJ anayechezesha nyimbo hizo anapewa huduma za kimaingi K**a vile maji na umeme bure. Pia ana duka kubwa la madawa ambalo mtaji wake ni bohari kuu ya madawa ya serikali.

06/10/2021

TUMBO LISILOSHIBA NA HADITHI NYINGINE.

MAKINIKA!

1)Kifafa cha uzazi kilimpiga dafrau akaanguka chini; maiti. Akaiaga dunia bado mbichi k**a jani la mgomba!
a)Eleza muktadha wa dondoo (alama 4)
Haya ni maneno ya Mashaka akiwa ruyani/ndotoni kwenye kitanda chake cha mayowe; anamrejelea nina yake Ma Mtumwa ambaye alifariki pindi tu alipomzaa Mashaka.

b) Fafanua mbinu nne za lugha zilizotumika kwenye dondoo (alama 8)
Nahau~ kilimpiga dafrau- kilimwangamiza
Akaiaga dunia-Akafariki.
Kumbuka kwamba nahau nyingine zinaweza kutumika badala ya AGA DUNIA mathalan:
~Enda jongomeo
~Tangulia mbele za haki
~Ametupa mkono
~Rudi kwa muumba
n.k
Jazanda~ Kifafa cha uzazi- uchungu wa uzazi
Tashbihi~ ...k**a jani la mgomba (Dhihirisho tosha kwamba alikuwa na umri mdogo bado; hivyo kifo chake kikawa pigo kubwa kwa Mashaka)
Nidaa~ .... mgomba!
Tashihisi~ Dunia imepewa uwezo wa kutenda k**a binadamu kiasi kwamba Ma Mtumwa anaiaga.

Tanbihi
Kifafa cha uzazi kilichotajwa hurejelewa k**a:
Pakanga~ uchungu aupatao mwanamke anapokaribia kujifungua.
Zingizi~ huu nao ni uchungu aupatao mwanamke baada ya kujifungua vilevile ni uchungu aupatao mwanamke awapo mwezini (kwenye hedhi)
Aidha, ni kitokacho tumboni mwa mwanamke baada ya kujifungua yaani , 'placenta'.
Kopoa~zaa
Himila~mimba

c)Mnenani alipokaramka alianza kujihusisha na nini kwa mujibu wa hadithi? (alama 8)
√Kuchuma karafuu kwa kazi ya kibarua.
√Kumwangulia mtu n**i
√Alienda pwani kurambaza
√Alienda pwani kuokota kombe na chanje.
√Alimsaidia mtu kufyeka majani usoni pa nyumba yake.
√Alimchanjia mtu kuni
√Alimfulia mtu nguo
√Kupuga pasi nguo za mtu.
√Alizichuma mabungo au zambarau, chocha au hata fuu kwa ajili ya kuuza.

Longa nami kupitia kwa ukurasa huu.

21/08/2021

Ukabila ni kikwazo Cha maendeleo katika jumuiya ya Chozi la Heri.Dhibitisha kauli hii ukitolea mifano mwafaka. (Al.20).

21/08/2021

Kuandika insha ya methali:
1. Kisa kiwe kimoja.
2. Kichwa kisiwe cha methali mbadala.
3. Maana ya methali ijitokeze aya ya kwanza.
4. Insha izingatie seheme mbili za methali.

Want your school to be the top-listed School/college in Kilifi?

Click here to claim your Sponsored Listing.

Location

Category

Website

Address


Kilifi