22/04/2026
Jeneza halina nafasi ya vijiti wala urembo. Utakapokufa, mwili wako utaoshwa ukiwa uchi na watu ambao huenda hata hukuwafahamu. Nyash kubwa, matiti, mazuri, na uzuri wote wa nje vitakuwa havina maana tena wakati huo.
Maisha haya ya mwili ni ya muda mfup tui, na kile tunachokipambania sana leo, kesho kinaweza kisiwe na thamani yoyote. Ndiyo maana si busara kujivunia sana muonekano wa nje au mali za dunia, ukasahau utu na wema kwa wengine.
Watendee watu vizuri, heshimu kila mtu, na jenga tabia njema. Hujui ni nani atakayesimama karibu yako siku ya mwisho, au ni nani atakayehusika na taratibu zako za mwisho. Dunia ina mzunguko wake, leo una nguvu na nafasi, una cheo kikubwa serikalini una ustaa lakini kesho mambo yanaweza kubadilika.
Kumbuka, watu hawatakukumbuka kwa uzuri wako au ulivyovaa, bali watakukumbuka kwa matendo yako, maneno yako na namna ulivyowatendea. Hivyo chagua kuwa mtu wa wema, heshima na huruma, kwa sababu mwisho wa siku, utu wako ndio utakaobaki kuwa kumbukumbu yako duniani. @ copied.
28/12/2025