23/08/2020
Online Classes at Santa Lucia Schools.
Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Jamii Na Jumuiya, Educational Research Center, City Estate, City Estate.
To plan, organize and implement an appropriate instructional program in a learning environment that guides and encourages students to develop and fulfill their academic potential.
23/08/2020
Online Classes at Santa Lucia Schools.
Tukutane mtandaoni wadau wote wa elimu
Karibuni sana
20/04/2020
The demand for great teachers is a tangible pressing need. While our country has come a long way in education reform, we still have a long way to go. There are schools across America that are still in high need because of budgetary concerns and low teacher retention, and students still continue to drop out at alarming rates. One reason to become a teacher is to impact the education system. If you recognize the need to improve the quality of education in this country, then you may become a teacher to affect change. There is a lot of work to be done, but it is the collective effort of thousands of dedicated teachers that will make the most difference
Matumizi sahihi ya Kiswahili
KATIKA hali ya kawaida ya maisha, wanaadamu ni lazima wawasiliane. Na chombo kikubwa cha mawasiliano ni lugha. Lugha hutumiwa na jamii kuweka mawasiliano katika shughuli mbalimbali.
Katika lugha ya Kiswahili yapo maneno mengi yanayotumiwa kimakosa na kufikia kuzoeleka na kuonekana ni sahihi pasi na watumiaji kujua kwamba ni makosa.
Katika hali hiyo, Rais wa awamu ya pili wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Alhaj Alli Hassan Mwinyi aliwahi kurekebisha baadhi ya maneno ya Kiswahili yanayotumika vibaya. Neno mojawapo lilikuwa "kuonyesha" likiwa na maana ya kuonekana kwa kitu na badala yake likawa "kuonesha" ambalo ni sahihi. Kwani "kuonyesha" linalotokana na na neno "kuonya" lenye maana ya kukataza. "Kuonesha" linatokana na neno "kuona" lenye maana kutazama.
Makala haya ni mwendelezo wa kuweka sawa matumizi ya lugha ya Kiswahili. Neno nitakaloanza nalo ni "kufundisha".
Watumiaji wengi wa lugha ya Kiswahili walitumia vibaya neno hili, kinyume na asili ya neno lenyewe. Kwa mfano "Mwalimu anafundisha hisabati". Hapa kosa la kawaida ni "kufundisha". Usahihi wake ni "Mwalimu anafunzisha hisabati". Kufunzisha ni kumpa mtu maarifa mapya. Na ndio maana anayepewa maarifa hayo huitwa mwanafunzi na haitwi mwanafundi.
Hili neno "kufundisha" asili yake ni "funda". Kwa mfano "Bibi anamfunda mjukuu wake". Hapa ukiangalia kwa undani wa sentensi hii utagundua kuwa maana ya sentensi hii ni kuwa bibi anampa mbinu mjukuu wake.
Vivyo hivyo hata neno "fundisha" ni kumpa mtu mbinu mbalimbali juu ya kitu fulani. Ndio maana watu wenye ujuzi wa kitu fulani wanaitwa "mafundi". Kwa hiyo yule fundi anayewaongoza watu kuwapa ujuzi fulani ndo sahihi kusema "anafundisha".
Kwa kutoa hitimisho juu ya neno hili si sahihi kusema "mwalimu anafundisha" bali ni sahihi kusema "mwalimu anafunzisha".
Neno lingine ni "Mgeni wa heshima".
Watumiaji wengi wa lugha ya Kiswahili wanalitumia vibaya neno hili. Kwa mfano katika hafla au sherehe mbalimbali zinapoandaliwa huwa anakaribishwa mtu maalum. Mtu huyo anaweza kuwa kiongozi wa ngazi fulani, hivyo anapewa heshima ya hali ya juu katika shughuli hiyo. Tuangalie mfano ufuatao:
Wananchi wataelewa kinachokusudiwa. Lakini katika matumizi ya lugha ya Kiswahili neno mgeni wa heshima si mahala pake kutumika hapo. Na lina maana nyingine ambayo ni kinyume na kusudio na maana yake ya msingi. "Mgeni wa heshima", maana yake ni kutokuwa na heshima. Kwa maana nyingine ni sawa na kusema ni kumtusi (kumtukana).
Kwa mfano mtu ni mara yake ya kwanza kwenda Nairobi na anatokea Mombasa. Ni sahihi kusema mtu huyu ni mgeni wa Nairobi na ni mwenyeji wa Mombasa. Maana yake ni kwamba mtu huyu mji wa Nairobi haujui vizuri k**a anayouvujua mji wa Mombasa. Hivyo ukisema "mgeni wa heshima" maana yake heshima ni kitu kigeni kwake. Kwa maana nyingine hana heshima.
Neno sahihi linalotakiwa litumike badala ya "mgeni wa heshima" ni "mgeni muheshimiwa" yaani watu wa pale kwenye hafla hiyo wanamuheshimu na yeye pia anawaheshimu.
Nahitimisha kwa kusema kuwa si sahihi kumwita mtu "mgeni wa heshima" bali ni sahihi kumwita "mgeni muheshimiwa" au mgeni rasmi.
Mwalimu Yusufu