08/04/2017
Nakumbuka kipindi nipo mdogo wazee wangu waliniambia mwenetu soma sana kwani ukisoma sana utakuwa na maisha mazuri katika hii dunia ,kiukweli nilisoma nikiamini maneno ya wazee na kujiaminisha kuwa ni kweli mafanikio only yanapatikana shuleni tu lakini hadi hii leo mwaka 2017 sina hata kimoja nilichonacho k**a asset katika maisha yangu bado nimekuwa mtu wa kuhangaika huku na kule bila mafanikio kiasi kwamba hata wenzangu tuliosoma pamoja baadhi yao wana maisha mazuri na hawakuyapata kupitia shule , inatokea baadhi ya siku najilaumu sana kwa kupoteza muda mwingi eti nikiamini mafanikio yanapatikana shuleni tu kumbe sio sahihi ,sikujua kuwa shule inanipelekea kutafta kazi badala ya kutafta pesa hivi leo nipo chuo mwaka wa mwisho eti nasoma elimu ya juu bila kujali elimu ya juu sio suluhisho la kuwa na maisha bora ? Hivi ni yupi mwenye mafanikio ya kimaisha kati ya mtu mwenye elimu ya juu sana na mtu mwenye hela ? Mafanikio ya mtu yanapimwa kwa kuwa na elimu au pesa ? Je elimu inamart sana mtu kuwa na mafanikio katika maisha ?/
27/02/2017
26/02/2017