27/05/2026
السَّلَامُ عَلَيْكُمْ وَرَحْمَةُ اللَّهِ وَبَرَكَاتُهُ
Kwa niaba ya uongozi na walimu wa shule, tunapenda kuwapongeza wazazi na walezi wote katika Sikukuu ya Eid Al-Adh’ha.
Tunamuomba Mwenyezi Mungu awajaalie afya njema, rehma, amani na mafanikio katika familia zenu.
Asanteni kwa kuendelea kushirikiana nasi katika malezi mema na elimu ya watoto wetu.
عِيدُكُمْ مُبَارَك وَكُلُّ عَامٍ وَأَنْتُمْ بِخَيْرٍ
01/05/2026
Assalaamu ‘alaykum warahmatullahi wabarakaatuh.
Kwa heshima na furaha kubwa, napenda nyote katika maadhimisho ya Wafanyakazi Duniani, Mei Mosi. Tunatambua kwa dhati mchango wenu mkubwa katika kuendeleza elimu yenye maadili ya Kiislamu, kujenga tabia njema kwa wanafunzi, na kusimamia majukumu yenu kwa uaminifu na kujituma.
Kazi mnayoifanya si tu ajira, bali ni ibada yenye malipo makubwa mbele ya Mwenyezi Mungu. Kila juhudi mnayoweka katika malezi, nidhamu, na utoaji wa elimu bora ni sehemu ya sadaka yenye kuendelea.
Nawahimiza kuendelea kufanya kazi kwa bidii, uadilifu, na mshikamano, tukilenga kuleta mabadiliko chanya katika jamii kupitia elimu ya Kiislamu.
Mwenyezi Mungu awabariki katika kazi zenu, awaongezee afya njema na mafanikio zaidi.
_Heri ya Sikukuu ya Wafanyakazi!_
S.O Mwangu.