Mathias Samwel

Mathias Samwel

Share

Passionate about Youths, married couples, Relationship and Men. Helping them to overcome life difficulties, Renew their mind and live a life driven purpose

22/03/2026

JENGA MSINGI WAKO KWENYE MWAMBA IMARA

Mathayo 7

26 Na kila asikiaye hayo maneno yangu asiyafanye, atafananishwa na mtu mpumbavu, aliyejenga nyumba yake juu ya mchanga;

27 mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, pepo zikavuma, zikaipiga nyumba ile, ikaanguka; nalo anguko lake likawa kubwa.

Jumapili njema

22 March 2026

Youth with Purpose

11/03/2026

AYA YA LEO

Mathayo 6
1 Angalieni msifanye wema wenu machoni pa watu, kusudi mtazamwe na wao; kwa maana mkifanya k**a hayo, hampati thawabu kwa Baba yenu aliye mbinguni.

UJUMBE

Kila unapotenda jambo jema ,lifanye kwa manufaa ya yule umtendeaye au mhitaji na si kutaka watu wakuone ukifanya jambo hilo.
Usiache kutenda Mema Siku zote.

Mathias samwel
11 March 2026

Youth with Purpose

10/03/2026

TABIA ZINAZOUA HATIMA YA KIJANA

Habari za muda huu Ndugu na jamaa zangu.Leo napenda tujifunze tabia nne tu miongoni mwa nyingi zinazoua hatima ya kijana.Fuatana nami hapa chini 👇

1.MATUMIZI YA DAWA ZA KULEVYA🌬️

Matumizi ya dawa za kulevya ni hatari sana katika maisha ya kijana na huua hatima ya kijana kwa haraka na hàkika.

Dawa za kulevya Zina adhari kubwa za moja kwa moja kisaikolojia 🧠 na kimwili.

Dawa za kulevya huharibu uwezo wa kufikri,kumudu hisia (Emotional control) ,Hujenga mtazamo hasi katika Mambo mbalimbali na hupelekea mtu kuugua magonjwa ya Akili na mwili na hivyo kuua hatima ya mtu kabisaa.

Matumizi ya dawa za kulevya
Mfano Bangi , Co***ne, Ma*****na, Heroine na morphine, Yameua hatima ya vijana wengi sana.
Vijana wengi wamekuwa tegemezi, wagonjwa wa Afya ya Akili na mwili, wezi ,wabakaji ,wenye fujo na wauaji kwa sababu ya kutumia dawa za kulevya.

Hivyo kijana ishi maisha yenye kusudi ili kufikia hatima yako iliyo njema.

2.ULEVI🍾🥂🍻

Matumizi ya pombe Yana madhara makubwa sana katika maisha mtu katika umri wowote .

Katika kipindi Cha Ujana Afya yako inaweza kuharibika kabisaa kutokana na matumizi ya pombe, pombe inaweza kuharibu Ini,moyo ,mapafu na hatimaye baada ya muda tu kidogo hapo mbele Mtu anakuwa dhaifu sana na inakupelekea kuugua ugonjwa wa Muda mrefu au hata kufa kabla ya wakati (Premature Death).

Hata hivyo pombe hupunguza Utendaji na ufanisi wa kazi,huchajiza matumizi mabaya ya rasilimali alizonazo mtu.

Pombe hupelekea mtu kuacha au kuachishwa kazi, kuvunja ndoa🚻, Kuua mali zake mbali mbali kwa dhumuni la kupata fedha ya matumizi ya pombe au kulipa madeni yaliyotengenezwa kwa sababu ya ulevi .

Vijana wengi pia wameharibika kisaikolojia 🧠 kwa sababu ya Uraibu wa Pombe na hivyo kupoteza morali ya kutaka kufanikiwa na kubaki wanaishi tu bila malengo yeyote.Kijana amka ,sh*tuka pombe imeua hatima ya wengi sana.

3.UVIVU 🛌

Tabia ya kijana Kuishi bila kufanya kazi yoyote ya kuingiza kipato au kusaidia jamii imeua hatima ya vijana wengi sana .

Kijana anaweza kujishughulisha kwa kufanya biashara ,kazi ya kuaajiriwa ,kulima na kazi yeyote halali .

Kijana anapaswa kutengeneza hela kwa ajili ya sasa na baadaye,fedha inasaidia kutatua changamoto nyingi sana japo si zote lakini ni Muhimu sana kuwa nayo.

Matumizi mabaya ya fursa zinazokuja mbele yako hupelekea kujutia baadaye maana kuna muda Nguvu ulizonazo zitaisha,Afya ulionayo inaweza kudhoofika na fursa unazopata sasa zinaweza zisipatikane tena.

Tabia ya kijana kulala muda mrefu, kuangalia TV muda mrefu,kuchati tu muda mrefu , kufanya kazi kwa mikono milegevu imeua hatima ya vijana wengi sana Duniani.

Kijana Lazima uwe na kazi ya kufanya na ni lazima uifanye kwa bidii ili ilete matunda/faida.

4.MAHUSIANO YA KIMAPENZI 💑
Kijana anapaswa kuwa na Mahusiano yenye Afya kwa maana ya kuwa na mke au mme ,kujenga familia na kuweka malengo yatakayo itoa familia yako kutoka hatua ilipo hadi hatua zaidi iliyobora kabisaa.

Tabia ya vijana kuwa na wapenzi wengi ,kuwa na michepuko ,kujiuza kwa wadada, imeharibu hatima ya vijana wengi sana Duniani.

Kupitia kuwa na wapenzi wengi Nidhamu ya maisha hushuka na pia siyo standard ya Mungu, kunaleta matumizi holela ya rasilimali fedha.

Kuwa na wapenzi wengi hatima ya wengi imekufa kutokana na Magonjwa yanayopatikana kupitia kujamiana .

Ndoa za vijana wengi zimekufa kwa sababu ya michepuko au watu wa pembeni.

Wadada wengi wamepoteza maisha au kuishi na maradhi ya muda mrefu kwa sababu ya kujiuza.
Tunza hatima yako kwa Mahusiano yenye tija.
Usikubali utu wako utwezwe
Usinunue mafanikio kwa uchi wako
Usitafute kazi kwa uchi wako.
Usitafute amani kwa uchi wako .
Usitatue Matatizo kwa uchi wako.

Usishushe thamani yako ,usishushe Ukubwa wa kusudi ambalo Mungu ameweka ndani ya Maisha yako.

Katika kuepuka mambo hayo yote usisahau kuweka maisha yako kwa MUNGU huyo ndiye anaweza kuyaongoza maisha yako, usizitegemee akili zako mwenyewe.

Mathias samwel
10 March 2026.

Youth with Purpose.

09/03/2026

A WAKE UP CALL

Ezekiel 36:26 I will give you a new heart and put a new spirit in you; I will remove from you your heart of stone and give you a heart of flesh.

Message
Ask almighty God to refresh your spirit, soul ,mind and body . Allow him to create something new in you,he is always ready for this.

Mathias samwel
Life Transforming Ministry (LTM)
09 March 2026.

Youth with Purpose

08/03/2026

KIJANA USIKATE TAMAA

Je!Kuna jambo umekuwa ukitamani
Kufanikisha mara nyingi? Umekuwa ukimuomba Mungu lakini bado hujafanikiwa?Ni huduma pengine unayoifanya ipo vile vile?

Je ! Umejitahidi mara nyingi kuacha kutenda dhambi fulani ,mfano Uzinzi , Uasherati, Uongo na Wizi Lakini umeona imeshindikana ,umekuwa ukijilaumu na kujutia nafsini mwako kwa sababu ya hili?

Je! Kuna tabia mbaya unatamani kuiacha lakini bado inakutumikisha?

Je! Umeweka bidii sana katika biashara yako/zako lakini kila siku Uchumi wako unazidi unashuka,mambo mapya yanaibuka yenye kuhitaji pesa?

Je! Umeugua muda mrefu sasa bila kupona? Umetumia dawa na kubadilisha matibabu mara nyingi bila mafanikio?

Leo nina ujumbe wako kuwa USIKATE TAMAA,USIKOSE TUMAINI TENA, YESU KRISTO MUWEZA WA YOTE YUPO PAMOJA NA WEWE.

Kamwe fikra ya kushindwa ikatae,usiiweke katika akili na moyo wako .Lile kusudi MUNGU ameweka ndani yako lipo pale pale,usikubali kushindwa kwa sababu ya mazingira yasiyo rafiki au ya kukatisha tamaa.Usikate tamaa songa mbele kwa imani .

Ninakuombea leo Yesu kristo akufungue kifungo chako ,yeye peke yake ndiye anaweza KUKATA kiu ya dhambi na kukusaidia kuacha kabisaa.

Yesu kristo ndiye kila kitu,anasema njooni kwangu wenye mizigo na kulemewa nami nitawapumzisha (Mathayoe11:29-30).

Usichoke kumuomba MUNGU kila siku, Wakati usioujua Mungu atakujibu maombi yako yote, wakati usioujua Mungu atainua huduma yako juu kwa kila jambo kuna majira yake (Mhubiri 3:1).

Acha kuona unaweza kwa nguvu zako mwenyewe,weka Tumaini lako kwa Mungu yeye ambaye hajawahi kushindwa tangu Enzi na Enzi.

Muombe Mungu akushindie dhambi yako leo ,Ainue huduma yako leo na ninakuombea kwa MUNGU akuvushe kwenye bonde hilo, akusaidie kupiga hatua mbele,akutakase,akuponye ugonjwa wako,aumbe jambo jipya kwako, Neema na Rehema zake ziwe juu yako katika Jina la YESU .
Amina.

Mathias samwel
08.03.2026.

Youth with Purpose.

05/03/2026

A WAKE UP CALL

On the way to your destiny, there will be circumstances that contradict what God has for you.

You know God is restoring health back to you, but the report says you won’t get well. It’s tempting to allow what’s not happening define who you are.

However, those circumstances don’t define you. Your time is coming, what God has promised you is still on the way.

God’s favor is on your life and the enemy knows that that's why increases the afflictions in you.

Pray to your father God that you can endure to all the challenges you're facing , may your faith stay firm to God in Jesus name Amen.
Amen

Mathias Samwel
Life Transforming Ministry
05 March 2026, Thursday

Youth with Purpose.

01/03/2026

THEME TITLE : I AM AND I CAN

To step ahead in your life ,you need to have an "I am " and an "I Can" attitude, fill your thoughts and your words with these confession daily and then this will be a break through for you to bring more Joy into your life.

The scripture says ;And we know that in all things God works for the good of those who love him, who have been called according to his purpose( Roman 8:28)
Those who speaks good and believe they can do ,they can achieve God's purposes installed in them, God works for them.

Proclaim ability and Speaks good for you.
Philippians 4:13 I can do all things through Christ who strengthens me.

You need to train your mind and your mouth to think and Speak more like God,work together to achieve God's purpose for your life.

You can overcome evil with good.

MathiasSamwel
1 March 2026

Youth with Purpose

08/02/2026

YOUTH AGE, THE TIME OF INNER CRISIS

This is the age of personal choice.
It is usually the time of inner crises.
At this time,there is a powerful battle for your mind, your focus and your affections as youth.

You have to overcome inner crises , establish and bold your personal choices that will take you to the next level.

Win your battle today

Youth with Purpose

Mathias samwel
08 February 2026, Sunday

05/02/2026

AYA YA LEO

Ayubu 14
1 Mwanadamu aliyezaliwa na mwanamke Siku zake za kuishi si nyingi, naye hujaa taabu.

2 Yeye huchanua k**a vile ua, kisha hukatwa; Hukimbia k**a kivuli, wala hakai kamwe.

UJUMBE

Mungu ametuleta Duniani kwa kusudi maalumu kwa kila mtu na tupo Duniani kwa muda tuu.Hivyo tuwe watu wa Kutathimini matendo yetu na kazi aliyotupa Mungu Je? tunaifanya?Tunafanya chochote kwa ajili ya Ufalme wa MUNGU?

Youth with Purpose

Mathias samwel
05 February 2026 ,Thursday.

03/02/2026

AYA YA LEO

Wakolosai 2:8

Angalieni mtu asiwafanye mateka kwa elimu yake ya bure na madanganyo matupu, kwa jinsi ya mapokeo ya wanadamu, kwa jinsi ya mafundisho ya awali ya ulimwengu, wala si kwa jinsi ya Kristo.

UJUMBE

Maisha ya mtu hutawaliwa na Mungu kwa njia ya mafundisho sahihi na shetani pia humdanganya binadamu kwa mafundisho potovu.
Hivyo Kuwa makini sana na chakula Cha kila siku Cha ubongo na Roho yako.

Mathias samwel
03 February 2026, Tuesday

29/01/2026

AYA YA LEO

Zaburi 9
1 Nitamshukuru Bwana kwa moyo wangu wote; Nitayasimulia matendo yako yote ya ajabu;

UJUMBE

Jifunze kumshukuru Mungu maana amefanya na atafanya vitu vingi kwako,tenga muda wa kumshukuru hata k**a unapitia changamoto kubwa sana.Mungu anabaki kuwa Mungu.

Youth with Purpose

Mathias samwel
29January 2026

26/01/2026

WINNING BATTLES FOR YOUTHS

The real battles of this world are about capturing the young people.
When you understand this battle,then you will understand why you are facing all the conflicts that you do as young person .

You will understand why you're confronted with all the challenges that are coming your way.

At this point you're ought to choose God or Satan but I advice you choose divine guidance (God) the one will always enable you to defeat enemies.

You can not be passive .A 'Yes ' to God is a 'NO' to the devil and fail to choose God is equally a 'welcome' to the enemy who is seeking whom he may devour.

Make choices that will have good outcomes in the years ahead.
God will help you to win the battles you are going through.Choose God Today .

Youth with Purpose

Mathias samwel

26 January 2026 , Monday

Want your school to be the top-listed School/college in Tabora?

Click here to claim your Sponsored Listing.

Location

Website

Address

Tabora