01/02/2024
PHOTOCOPY MPYA 2024
✍️Leo Mkuu wa shule Mwl Mariam J. Salumu kwa kushirikiana na Mwenyekiti k**ati ya shule, walimu na wanafunzi wamepokea Photocopy machine mpya kutoka Kwa Mmiliki wa CHUO CHA SANT MAXCIMILLIAN Madame E. Nkonyoka.
✍️Mkuu wa shule amesema kwa upatikanaji wa machine hii utaongeza ufaulu kwa kuwa watafanya mazoezi ya kutosha
19/10/2023
✍️Asante Mh. Rais Dr. Samia Suluhu Hassan tunakushukuru na Tunasema asante sana mama kwa kutujali watoto wa Tabora,
✍️Asante sana Mkuu wa Mkoa Mh. Balozi Dr. Batlida S.B Kwa upendo, tunawatakieni majukumu mema.
WILSON [Mwanafunzi]
19/10/2023
Tumefurahia kuimba mbele ya Mh Rais Dr Samia Suluhu Hassan katika kuweka jiwe la msingi chuo cha VETA Igunga Tabora
14/07/2023
CHA TPC TABORA
✍️Leo kwaya ya shule ya Msingi Majengo iliialikwa kutumbuiza katika mahafali ya tisa ya chuo cha Tabora Polytechnic college[MUSOMA UTALII].
✍️Mkurugenzi wa chuo hicho Ndg Shaban Mrutu ametoa Talakilishi k**a zawadi kwa shule ya Msingi Majengo.
✍️Mkuu wa shule Mwl Mariam Salumu ameshukuru kwa niaba ya Walimu wote.
11/07/2023
✍️Mradi wa Ujenzi wa Vyumba vitatu vya madarasa na matundu matatu ya Vyoo
✍️Hii ndio hatua ambayo imefikiwa hadi leo tarehe 11.07.2023
07/06/2023
UNAENDELEA 07.06.2023
✍️Shule ilipokea jumla ya Tsh 84,600,000 kutoka katika mradi wa BOOST, ikiwa Tsh 78,000,000 ujenzi wa vyumba vitatu vya madarasa na Tsh 6,600,000 ujenzi wa matundu matatu ya vyoo.
✍️Ujenzi umefikia mahali pazuri na unaendelea kwa kasi na kwa ubora wa hali ya juu
06/06/2023
✍️Kwaya ya Wanafunzi wa shule ya Msingi Majengo wakitumbuiza katika uwanja wa A.H. MWINYI Kwenye ufunguzi wa UMITASHUMITA, UMISETA NA FEASA Hapa Mkoani TABORA
✍️Mgeni Rasmi ni Makamu wa Rais Dr P. I. Mpango Kazi iendelee
01/05/2023
✍️Leo siku ya wafanyakazi katika maadhimisho ya mei mosi Mkoa wa Tabora yamefanyika katika Wilaya ya Sikonge na Mkuu wa shule hii amekuwa mfanyakazi bora wa Mkoa.
✍️Amesema mkurugenzi Dr Peter M. Nyanja Manispaa ya Tabora "Hongera mwalimu Mariam Salum MKUU WA SHULE YA MSINGI MAJENGO KWA KUTEULIWA KUWA MFANYAKAZI BORA WA MKOA NA MKUU WA MKOA MH. DR BATILDA S BURIANI, CHAPA KAZI NA KAZI IENDELEE"
✍️Walimu wa majengo tunasema asante sana na kazi iendelee
26/04/2023
✍️Leo tar 26.04.2023 Walimu na Kwaya ya shule imeshiriki katika kusheheresha sherehe za Muungano wa Tanganyika na Zanzibar
✍️Maadhimisho kimkoa yamefanyika katika viwanja vya Brigedi Karibu na ofisi za mkuu wa mkoa.
✍️Mgeni rasmi katika maadhimisho hayo alikuwa mkuu wa Mkoa Balozi Batlida Burian
24/04/2023
✍️Leo Mwenyekiti wa malezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Tabora ndg. MWAMBA ZUBERI BUNDALA ameongoza k**ati ya siasa kata ya Mpela, Ofisi ya Mtendaji, Walimu sambamba na wanafunzi katika zoezi la Upandaji miti kuzunguka eneo la shule ya MAJENGO.
✍️Kwa kushirikiana na ofisi ya kata ndg MWAMBA ZUBERI MWAMBA na Mtendaji wa Kata Ndg Mathew Dastan wamesema watahakikisha miti hiyo inastawi vema.
✍️Aidha Mkuu wa shule Mwl Mariam J. Salumu amewashukuru na kuwaahidi kuisimamia kwa kila hatua.
10/04/2023
DOGO ASIKAE CHINI
✍️Leo Mkuu wa shule Mwl Mariam J. Salumu. Amepokea madawati 20 Ambayo yametolewa na MDAU WA ELIMU
✍️Mkuu wa shule amesema bado Kuna upungufu mkubwa sana wa madawati unaoikabili shule, hivyo anawakaribisha wadau wengine popote walipo Ili waweze kuchangia.
✍️Mtendaji wa kata, mwenyekiti wa mtaa na wadau walifika kuyapokea madawati hayo leo jioni
ASANTE SANA MDAU WETU NA MUNGU WA MBINGUNI AKUBARIKI