Institute of Accountancy Arusha-Songea Campus

Institute of Accountancy Arusha-Songea Campus Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Institute of Accountancy Arusha-Songea Campus, College & University, TTCL Building, Sokoine Road P. o box 800, Songea.

25/08/2026
Naibu Mkuu wa Chuo Mipango, oFedha na Utawala, Dkt. Grace Idinga  ametembelea Banda la Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA) kwe...
24/07/2026

Naibu Mkuu wa Chuo Mipango, oFedha na Utawala, Dkt. Grace Idinga ametembelea Banda la Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA) kwenye Maonesho ya Saba Wiki ya Elimu ya Juu Zanzibar, yanayoendelea katika Uwanja wa Gombani kisiwani Pemba.

Tunawakaribisha watu wote kutembelea banda letu kwenye maonesho haya ambayo yameanza tarehe 23 Julai 2026 na yatahitimishwa tarehe 27 Julai 2026, ili kupata taarifa mbalimbali kuhusu IAA, ushauri kuhusu kozi na kufanya udahili kwa ajili ya kujiunga na IAA kwa ngazi ya Stashahada (Diploma), Shahada (Degree) na Shahada ya Uzamili (Masters Degree). Dirisha la maombi liko wazi kwa ngazi zote.

.

Wananchi kutoka maeneo mbalimbali Zanzibar wakipata huduma walipotembelea banda la Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA) katika ...
20/07/2026

Wananchi kutoka maeneo mbalimbali Zanzibar wakipata huduma walipotembelea banda la Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA) katika maonesho ya Wiki ya Elimu ya Juu Zanzibar yaliyoanza tarehe 14 Julai 2026 na kuhitimishwa leo Julai 20, 2026 katika Viwanja vya Mnazimmoja, Unguja.

Aidha, Chuo cha Uhasibu Arusha tutashiriki Maonesho ya Wiki ya Elimu ya Juu Pemba yatakayofanyika katika Viwanja vya Gombani Pemba, kuanzia tarehe 23-27 Julai 2026.

Tunawakaribisha watu wote kutembelea banda letu ili kupata taarifa mbalimbali kuhusu IAA, ushauri kuhusu kozi na kufanya udahili kwa ajili ya kujiunga na IAA kwa ngazi ya Stashahada (Diploma), Shahada (Degree) na Shahada ya Uzamili (Masters Degree). Dirisha la maombi liko wazi kwa ngazi zote.

.

RC MJINI MAGHARIBI APONGEZA IAA, AITAKA KUONGEZA NGUVU MAFUNZO YA MUDA MFUPIMkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi kwa sasa ni ...
19/07/2026

RC MJINI MAGHARIBI APONGEZA IAA, AITAKA KUONGEZA NGUVU MAFUNZO YA MUDA MFUPI
Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi kwa sasa ni Mhe. Moh'd Ali Abdalla ametembelea Banda la Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA) katika Maonesho ya Wiki ya Elimu ya Juu Zanzibar yanayoendelea katika Viwanja vya Mnazi Mmoja Unguja.

Mhe.Abdalla ameipongeza IAA kwa kazi nzuri inayofanya ya kutoa elimu katika fani mbalimbali na akatoa rai kwa IAA kuongeza jitihada katika utoaji wa kozi za muda mfupi (short courses) ili kuwaongezea maarifa na kuwajengea uwezo watendaji katika sekta Uhasihu, Fedha, Benki, Uchumi, TEHAMA na maeneo mengine.

" Mnafanya vizuri kwenye diploma, bachelor degree na master's degree muone namna ya kuongeza nguvu kwenye hizi short courses ili kuwaongezea maarifa watendaji wetu, na hii itaendelea kutangaza vema Chuo chenu" , amesema Mhe. Abdalla.

Tunawakaribisha watu wote kutembelea banda letu ili kupata taarifa mbalimbali kuhusu IAA, ushauri kuhusu kozi na kufanya udahili kwa ajili ya kujiunga na IAA kwa ngazi ya Stashahada (Diploma), Shahada (Bachelor Degree) na Shahada ya Uzamili (Masters Degree).

.

PROF SEDOYEKA AKUTANA NA IAA SC NA KUWAPONGEZA KUFUZU CHAMPIONSHIPMkuu wa Chuo Cha Uhasibu Arusha IAA Prof. Eliamani Sed...
18/07/2026

PROF SEDOYEKA AKUTANA NA IAA SC NA KUWAPONGEZA KUFUZU CHAMPIONSHIP

Mkuu wa Chuo Cha Uhasibu Arusha IAA Prof. Eliamani Sedoyeka amekuna na timu ya IAA Sports Club na kupata nao chakula cha mchana akiwapongeza kwa heshima waliokipa Chuo kwa kufuzu kucheza Championship msimu wa 2026/2027

Akitoa pongezi kwa Uongozi, benchi la ufundi, na wachezaji Prof. Sedoyeka amesema ni vyema maono waliyokuwa nayo yameanza kutimia huku akiwataka wachezaji kuendelea kupambana kwani lengo sio kuishia hapa bali ni kufika na kucheza Ligi kuu ya Tanzania

“Tufikishieni salamu zetu kwa Tff, Bodi ya Ligi na Chama cha Soka hapa Arusha, tunamipango mingi mikubwa hivyo watuzoee Kwani tutaendelea kufanya vizuri mpaka tufikie malengo tuliyojiwekea ” amesema

Kwa upande wake CEO IAA SC Nadhiru Abdunuru ameishukuru manejimenti ya Chuo, watumishi na mashabiki kwa kuwaunga mkono huku akiahidi kuwa moto wao ni uleule hivyo watahakikisha wanafanya vizuri mpaka kufikia malengo ya kucheza Ligi kuu

Ombeni Sefuye mshambuliaji wa IAA SC ameushukuru Uongozi wa Chuo uliopo chini ya Prof. Sedoyeka na kuahidi wao k**a wachezaji jukumu lao ni kuhakikisha wanaipambania nembo ya taasisi na kuendelea kufanya vizuri kwenye hatua zinazofuata.

IAA YAHIMIZA TAFITI ZISITUNZWE MAKABATINI BALI ZIWALETEE WANANCHI SULUHISHOTafiti zinazofanywa katika taasisi za elimu y...
17/07/2026

IAA YAHIMIZA TAFITI ZISITUNZWE MAKABATINI BALI ZIWALETEE WANANCHI SULUHISHO

Tafiti zinazofanywa katika taasisi za elimu ya juu, ikiwemo Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA), hazipaswi kubaki kwenye machapisho au maktaba pekee, bali zinapaswa kusambazwa kwa jamii na wadau ili ziwe sehemu ya utatuzi wa changamoto katika sekta mbalimbali, ikiwemo kilimo.

Hayo yamesemwa leo, Julai 16, 2026, na mwakilishi wa Mkuu wa Chuo Taaluma, Utafiti na Ushauri wa Kitaalamu, CRN Charles Rafaeli, wakati akifungua warsha ya usambazaji wa matokeo ya utafiti kuhusu uundaji wa jukwaa la kujifunza kwa njia ya mtandao kwa kutumia akili unde (AI) katika kilimo cha vitunguu maji na vitunguu swaumu. Warsha hiyo ilifanyika katika ukumbi wa PGB wa IAA.

Aidha, amebainisha kuwaIAA imeendelea kuwekeza katika tafiti shirikishi, ubunifu, matumizi ya teknolojia za kisasa na kuimarisha ushirikiano na jamii ili kuleta matokeo chanya katika sekta mbalimbali, hususan kilimo, akiongeza kuwa jitihada hizo zinalenga kujenga uchumi shindani na kuunga mkono utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Kwa upande wake, Afisa Kilimo wa Wilaya ya Arusha, Mhandisi Chrisben Saria, aliwahimiza wakulima na wadau wa sekta ya kilimo kutumia vifaa vya kielektroniki, hususan simu janja, kujifunza teknolojia mbalimbali zinazosaidia kuongeza tija na kutatua changamoto katika uzalishaji wa mazao, ikiwemo vitunguu maji na vitunguu swaumu, akisema matumizi ya teknolojia za kidijitali yanaweza kuwasaidia wakulima kupata taarifa sahihi kwa wakati, kuboresha mbinu za uzalishaji na kuongeza mavuno.

Naye mtafiti mkuu na mhadhiri Godson Mshana amesema utafiti huo uliofadhiliwa na Mradi wa HEET umetekelezwa kwa kipindi cha miaka miwili na miongoni mwa matokeo yake ni uundaji wa jukwaa la kujifunza kwa njia ya mtandao linalotumia akili unde (AI), lijulikanalo k**a PataIntel, ambalo litawawezesha wakulima na wadau kupata maarifa na taarifa kwa wakati kuhusu kilimo cha vitunguu maji na vitunguu swaumu.

.

MAONESHO YA WIKI YA ELIMU YA JUU ZANZIBAR Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA) tunashiriki Maonesho ya Wiki ya Elimu ya Juu Zan...
15/07/2026

MAONESHO YA WIKI YA ELIMU YA JUU ZANZIBAR

Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA) tunashiriki Maonesho ya Wiki ya Elimu ya Juu Zanzibar ambayo yameanza tarehe 14 Julai 2026 katika Viwanja vya Mnazimmoja, Unguja na yanatarajiwa kuhitimishwa Julai 20, 2026

Aidha, tutashiriki Maonesho ya Wiki ya Elimu ya Juu Pemba yatakayofanyika katika Viwanja vya Gombani Pemba kuanzia tarehe 23-27 Julai 2026.

Tunawakaribisha watu wote kutembelea banda letu ili kupata taarifa mbalimbali kuhusu IAA, ushauri kuhusu kozi na kufanya udahili kwa ajili ya kujiunga na IAA kwa ngazi ya Stashahada (Diploma), Shahada (Bachelor Degree) na Shahada ya Uzamili (Masters Degree).

Timu ya Mpira wa miguu ya Chuo Cha Uhasibu Arusha IAA Sports Club  imefanikiwa kufuzu kucheza michuano ya Championship m...
11/07/2026

Timu ya Mpira wa miguu ya Chuo Cha Uhasibu Arusha IAA Sports Club imefanikiwa kufuzu kucheza michuano ya Championship msimu ujao 2026/2027 baada ya kumaliza michezo yake ya playoff hapa katika Dimba la Mkwakwani Mkoani Tanga

IAA SC imepata sare ya Goli 1-1 kwenye mchezo wa pili wa playoff dhidi ya African Sports ya Tanga ambapo mchezo wa kwanza Arusha waliibuka na ushindi wa Goli 2-1

Ni rasmi sasa kuwa IAA SC itashiriki michuano ya Championship msimu ujao wa mashindano 2026/2027

Address

TTCL Building, Sokoine Road P. O Box 800
Songea

Opening Hours

Monday 08:00 - 16:00
Tuesday 08:00 - 16:00
Wednesday 08:00 - 16:00
Thursday 08:00 - 16:00
Friday 08:00 - 16:00

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Institute of Accountancy Arusha-Songea Campus posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share