09/07/2017
ISTIQAAMA OPEN SCHOOL (IOS) ni kituo kinachotoa mafunzo ya sekondari ya miaka miwili na mafunzo maalum kwa wanafunzi wanaohitaji kurudia mitihani ya kidato cha nne na kidato cha sita kwa michepuo yote yaani: science, art, and business (sayansi, sanaa, na biashara)
Kituo kipo eneo la Nyakato Sokoni, Wilaya ya Ilemela, Jijini Mwanza sambamba kabisa na Msikiti wa Nyakato Sokoni.
Kituo kina walimu na wakufunzi wazoefu na waliobobea katika fani ya elimu huria na masafa (Open and Distance Education), waliopata mafunzo kutoka Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima (IAE)
Kituo pia kinatoa mafunzo ya ziada (TUITION) kwa wanafunzi wa Sekondari. Kidato cha Kwanza mpaka Kidato cha Sita kwa Michepuo yote (Art, Science, and Business)
Mafunzo haya, yaani TUITION yanatolewa pia kwa wanafunzi wa Shule za Msingi za kawaida (SWAHILI MEDIUM) na za ENGLISH MEDIUM.
Kupitia kitengo cha Istiqaama Vocational Training College (IVTC), mafunzo ya ufundi wa aina mbali mbali yanatolewa. Mafunzo hayo ni ya ufundi wa Umeme majumbani (Domestic Electrical Installation), Ufundi wa Uchomeleaji na Uyeyushaji Vyuma (Welding and Metal Fabrication), Ufundi Magari (Motor Vehicle Mechanics), Uhudumu wa Hotel na Uongozaji Watalii (Hotel and Tourism Management), Ualimu wa Chekechea na Vituo vya Kulelea Watoto (Nursery School Teaching and Day Care Centres), na Ufundi wa Computer na Electronics (Computer Maintenance and Electronics)
Mafunzo Maalum ya Ufahamu wa Lugha za Kiingereza na Kiarabu pia yanatolewa. Kuna Darasa Maalum la Kujifunza Lugha ya Kiingereza cha Kuongea na Kuandika kwa Watu Wazima na Wanafunzi wa Sekondari na Vyuo. Wanafunzi watapangiwa muda wa kuhudhuria darasani kutokana na majukumu waliyonayo na muda ambao hautakuwa kikwazo kwao.
Kituo kipo wazi kuanzia saa MOJA NA NUSU ASUBUHI (07:30 am) mpaka saa MBILI NA NUSU USIKU (08:30 pm)
Kwa maelezo zaidi tembelea Ukurasa wetu wa Facebook www.facebook.com/istiqaamaopenschool au tumia namba za simu zifuatazo:
0687 447 447, 0784 414 212, 0767 414 312, 0767 984 798, na 0714 000 016
NYOTE MNAKARIBISHWA
ISTIQAAMA OPEN SCHOOL, KNOWLEDGE AND SERVICE (MAARIFA NA HUDUMA)
Istiqaama Open School (IOS) ni kituo cha Elimu kilichopo Wilaya ya Ilemela, Jijini Mwanza, Mtaa wa Nyakato Sokoni, Sambamba na Msikiti wa Istiqaama.