turiani_youth_group

turiani_youth_group Turiani youth group ni kikundi kisicho cha kiserikali NGO

25/10/2022

Coming soon....

25/10/2022

Coming soon..

Kilimo ni ajira kwa vijana.Karibu nyumbani kumenoga
25/07/2022

Kilimo ni ajira kwa vijana.
Karibu nyumbani kumenoga

09/06/2022
 youth foundation
09/06/2022

youth foundation

pichani ni mizinga ya nyuki ya vijana wa turiani youth group ikiwa inanyuki wa kutosha na muda mchache itakuwa tayari kw...
01/05/2022

pichani ni mizinga ya nyuki ya vijana wa turiani youth group ikiwa inanyuki wa kutosha na muda mchache itakuwa tayari kwa kulina, Vijana wa turiani youth group tunaendelea kupambana ili kufikia malengo yale tuliyo jiwekea k**a kikundi ndani ya mwaka mmoja. Hizi ni fursa za vijana hivyo vijana tupambazuke kiakili ili kujikwamua kiuchumi
Vijana tuunde vikundi kwa ajili ya kujikwamua kiuchumi na kuinua uchumi wa jamii husika na vijana kiujumla.

10/03/2022

534

Ufugaji wa nyuki unaweza kuwa chanzo kizuri cha kipato cha ziada kwa wakulima wadogo wadogo. Uzalishaji wa asali nchini Tanzania umekuwa ukitegemea sana wafugaji wadogo wadogo, wanaotumia njia za kiasili k**a vile mizinga ya magogo au vyungu, kwa nyuki wa kiafrika ambao ni wengi sana kwenye mapori.
Mkulima ambae anahitaji kufuga nyuki ni lazima awe na uelewa wa mzunguko wa maisha ya nyuki. Anaye anza ni lazima aulize wafugaji wenzake ambao wana uzoefu wa kutosha, au kujiunga katika kikundi cha ufugaji ili apate ufahamu zaidi juu ya ufugaji wa nyuki.
Tafuta sehemu salama kwa ajili ya mzinga
Ni vizuri kutafuta mahali pazuri, salama, na penye sifa ya kufugia nyuki. Vifaa vyote vikishapatikana jambo linalofuata ni kuchagua mahali gani pa kuweka mzinga. Ni vizuri sehemu hii ikawa mahali ambapo makundi ya nyuki hukusanyika mara kwa mara.
Ni wapi pa kuweka mzinga!
Mara nyingine kupata eneo sahihi ni tatizo. Ni vizuri kuzingatia yafuatayo:

Kulingana na hali ya kujilinda ya nyuki wa Afrika, haishauriwi kuweka mzinga shambani au karibu na shamba (weka umbali wa mita 150-200 kutoka kwenye mazao au nyumbani)

Mzinga ni lazima uwekwe sehemu ambayo haitasababisha upotevu wa nyuki wanaporudi kutoka nje ya mzinga (wasiingie kwenye kundi lisilokuwa lao)

Mizinga isiwekwe mbalimbali sana ili kuepusha usumbufu wa kutembea mbali kwa mfugaji wakati anapokagua. Eneo la kuweka mizinga ni lazima liwe :

Kimya na mbali ya jumuia (hospitali, shule, na viwanja vya michezo) na maeneo ya biashara au viwanda.

Karibu na maji masafi-kandokando ya mto, mabwawa ya samaki, mabeseni ya maji au sehemu ya matone.

Iwe karibu na chakula cha nyukimimea inayochanua, miparachichi, n**i, euculptus, migunga n.k

Iwe sehemu ambayo ni kavu na isiwe sehemu ya tindiga kwani unyevu unyevu husababisha ugonjwa wa ukungu (fungal disease) na pia huzuia utengenezaji mzuri wa asali.

Iwe mbali na watu waharibifu na iliyojificha kuepuka waharibifu.

Inaendelea

Watoto wa nguruwe wachomwe sindano ya madini ya chuma (Iron injection) baada ya siku moja au mbili toka kuzaliwa.Hii ni ...
10/03/2022

Watoto wa nguruwe wachomwe sindano ya madini ya chuma (Iron injection) baada ya siku moja au mbili toka kuzaliwa.
Hii ni muhimu sana vinginevyo wanaweza kufa wote Kata meno (tooth clipping) baada ya miezi mitatu Unaweza kuhasi madume (castration) baada ya miezi miwili.

MAGONJWA YA NGURUWE

Kuna aina nyingi za magonjwa katika ufugaji wa nguruwe lakini yapo yale yaliyozoeleka ambapo ni lazima kukabiliana nayo ili kuwa na ufugaji wa nguruwe wenye tija.

1. Ugonjwa wa miguu na midomo

Ugonjwa huu huathiri nguruwe sehemu za miguu na midomo Ni ugonjwa ambao hushambulia nguruwe mara kwa mara hasa wasipokuwa na matunzo mazuri Ugonjwa wa miguu na midomo hudhoofisha nguruwe kwa haraka sana ikiwa ni pamoja na kupungua uzito.

Chanjo: Chanjo kwa ajili ya ugonjwa wa midomo na miguu (FMD vaccine) hutolewa kila baada ya mwaka mmoja Hii inasaidia kuwaweka nguruwe wako katika hali nzuri zaidi bila kushambuliwa na magonjwa hayo.

Tiba: Ugonjwa huu hauna tiba halisi Inapotokea nguruwe wakawa wameshambuliwa kinachofanyika ni kutibu magonjwa nyemelezi kwa kutumia antibiotics.

2. Homa ya Nguruwe (Swine fever)

Virusi vinavyosababisha ugonjwa wahoma ya nguruwe huenea kwa haraka sana miongoni mwa makundi ya nguruwe na huua kwa haraka sana lakini hauna madhara kwa binadamu na hauambukizwi kwa binadamu.
Nguruwe walioambukizwa wana shikwa na vindonda ama mapunye kwenye ngozi Pia masikio na ngozi huwa mekundu.
Chanjo: Ugonjwa huu hauna chanjo wala tiba Kinachofanyika mlipuko unapotokea ili kuwa salama ni kuwateketeza nguruwe wote walioathirika na kuanza upya ufugaji wa nguruwe Unaweza kuteketeza nguruwe kwa kuwachoma moto.

Muhimu: Baada ya kuwateketeza nguruwe wagonjwa safisha banda kisha nyunyiza dawa aiana ya Acon au Ectomin na uache banda wazi kwa kipindi cha wiki moja kabla ya kuanza ufugaji wa nguruwe wengine.

3. Ugonjwa wa mapafu (Pneumonia)

Huu ni ugonjwa unaoshambulia sehemu za koo na mapafu ya nguruwe ambapo husababisha kukohoa na kupumua kwa shida.

Home » Blog » Ufugaji wa Nguruwe Kibiashara TanzaniaUfugaji wa TanzaniaUfugaji wa Nguruwe Kibiashara TanzaniaWauzajiFe...
10/03/2022



Home » Blog » Ufugaji wa Nguruwe Kibiashara Tanzania

Ufugaji wa Tanzania

Ufugaji wa Nguruwe Kibiashara Tanzania

Wauzaji

February 27, 2022



UFUGAJI WA NGURUWE TANZANIA

Ufugaji wa nguruwe ni wa watu wa kada zote, wafugaji wadogo wadogo na hata wakubwa pia ufugaji wa nguruwe huweza kumpatia mfugaji kipato pamoja na chakula kwa familia, na hauhitaji gharama kubwa.

VITU VYA KUZINGATIA KATIKA UFUGAJI WA NGURUWE

1. BANDA LA UFUGAJI WA NGURUWE

Nguruwe wanahitaji kuwa na banda lililojengwa kwa vifaa nafuu Unaweza kutumia mchanga na simenti kuweka sakafu, ama ukatumia udongo wa mfinyanzi kwa ajili ya kuweka sakafu.
Ukubwa wa banda unategemeana na idadi ya nguruwe na aina ya ufugaji wa nguruwe unaotaka kufanya. Mita 3 kwa mita 2.5 zitawaweka guruwe 8-10 wanaonenepeshwa kwa soko au nguruwe jike mmoja na nguruwe ndume mmoja.

2. CHAKULA CHA NGURUWE

Katika ufugaji wa nguruwe ulishaji wake ni rahisi kwa kuwa wanakula aina mbalimbali za vyakula kulingana na mazingira wanayofugwa Unaweza kuwalisha kwa kutumia majani laini ya aina mbalimbali na pia hulishwa kwa kutumia masalia ya nafaka (pumba).

Unaweza kuwalisha kwa kutumia mashudu au pumba aina ya Wheat Poland Pia unaweza kuwalisha kwa kutumia mabaki ya jikoni.

3. KUZALIANA KWA NGURUWE

Nguruwe hubeba mimba kwa kipindi cha siku 114, ambazo hugawanyika kwa miezi 3, wiki 3 na siku 3 Nguruwe mmoja ana uwezo wa kuzaa watoto 6 hadi 14 kwa mara moja Watoto wa nguruwe (piglets) huanza kula chakula cha kawaida wanapofika umri wa mwezi mmoja na nusu mpaka miezi miwili.

Endapo nguruwe watapata matunzo mazuri, baada ya miezi 8 wanakuwa na uzito kati ya kilo 50-70 na wanaweza kuuzwa.

4. MATUNZO YA NGURUWE

Katika ufugaji wa nguruwe Baada ya nguruwe kuzaa anatakiwa kupatiwa chakula cha kutosha na cha kutia nguvu ili kupata maziwa ya kutosha kwa ajili ya watoto wake. Watoto wa nguruwe wachomwe sindano ya madini ya chuma (Iron injection) baada ya siku moja au mbili toka kuzaliwa.
Inaendelea

Address

Diongoya
Mvomero
KARIBUNISANA

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when turiani_youth_group posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The School

Send a message to turiani_youth_group:

Shortcuts

Share

Category