18/05/2026
Umekuwa msimu mzuri sana kwa binti yetu Hasnath kushinda vikombe viwili msimu huu na timu yake ya FC MASAR WOMEN inayoshiriki ligi kuu ya wanawake Misri. Pongezi kubwa sana kwako. Familia yote ya MOSKISA na wadogo zako wote wanajivunia sana kuwa na dada k**a wewe, hakika umekuwa kioo cha wengi.
Hongera pia tena kwako kwa kufuzu kombe la dunia kwa wanawake U20. Makubwa sana yako mbele yetu tunamshukuru Mungu sana kwa ajili yako na namshukuru Mungu kunipa nafasi ya kukulea mpaka hatua hizi ni mapenzi yake tu.