19/10/2024
KITABU CHA UFUNUO WA YESU: eschatology : Any concern uliza via comment au 0784811512 ) (NB humu sija-focus na tafsiri za miaka au siku, Zingatia hilo kwanza).
1. Dunia ya sasa itaendelea hadi wakati wa DHIKI KUU, na dunia ya sasa itaendelea hadi mwisho wa miaka 1000 ya utawala wa Yesu.
Ili kutimiza ahadi ya Yesu ya kutawala katika kiti cha ufalme wa Daudi na kwa ajili ya ahadi ya Mungu kwa Isreal ya jinsi ya mwili).
Romans 11:26 Hivyo Israeli wote wataokoka; k**a ilivyoandikwa, Mwokozi atakuja kutoka Sayuni; Atamtenga Yakobo na maasia yake.
Luka 1: 32 Huyo [Yesu] atakuwa mkuu, ataitwa Mwana wa Aliye juu, na Bwana Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi, baba yake.
33 Ataimiliki nyumba ya Yakobo hata milele, na ufalme wake utakuwa hauna mwisho.
2. Mfalme atakayetengenezewa Sanamu yake na chapa yake, Wale wafalme wengine 10 pamoja na yule mfanya miujiza nabii wa uongo watafanya kazi katika timeline moja muda wa miezi 42,
Revelation 13:5 Naye akapewa kinywa cha kunena maneno makuu, ya makufuru. Akapewa uwezo wa kufanya kazi yake miezi arobaini na miwili.
Ufunuo 17: 12 Na zile pembe kumi ulizoziona ni wafalme kumi, ambao hawajapokea ufalme bado, lakini wapokea mamlaka k**a wafalme muda wa saa moja pamoja na yule mnyama.
13 Hawa wana shauri moja, nao wampa yule mnyama nguvu zao na mamlaka yao.
Revelation 19:20 ... yule nabii wa uongo... , yeye aliyezifanya hizo ishara mbele yake, ambazo kwa hizo aliwadanganya watu wale walioipokea ile chapa ya huyo mnyama, nao walioisujudia sanamu yake;
huu ndio wakati wa ile chapa na mateso makuu, ambayo yanafanyika mwishoni kabisa kabla Yesu hajasimamisha utawala wake wa miaka 1000
NB: Huu Muda wa miezi 42 ndio muda pia ambao kutakuwa na wale manabii wawili wa Mungu (mizeituni miwili), na mwisho wa hawa manabii wa Mungu ni kuuliwa na huyo mfalme hapo juu.
TUNAJUA NI NDANI YA MUDA HUO KWAKUWA HAWA WAWILI WALIUAWAWA NA HUYO MFALME MWENYE SANAMU NA CHAPA.
Ufunuo 11: 3 Nami nitawaruhusu mashahidi wangu wawili, nao watatoa unabii siku elfu na mia mbili na sitini, hali wamevikwa magunia.
4 Hao ndio ile mizeituni miwili na vile vinara viwili visimamavyo mbele za Bwana wa nchi.
5 Na mtu akitaka kuwadhuru, moto hutoka katika vinywa vyao na kuwala adui zao. Na mtu akitaka kuwadhuru, hivyo ndivyo impasavyo kuuawa.
6 Hao wana amri ya kuzifunga mbingu, ili mvua isinyeshe katika siku za unabii wao. Nao wana amri juu ya maji kuyageuza kuwa damu, na kuipiga nchi kwa kila pigo, kila watakapo.
7 Hata watakapoumaliza ushuhuda wao, yule mnyama atokaye katika kuzimu atafanya vita nao, naye atawashinda na kuwaua.
8 Na mizoga yao itakuwa katika njia ya mji ule mkuu, uitwao kwa jinsi ya roho Sodoma, na Misri, tena ni hapo Bwana wao aliposulibiwa.
3. Yesu mwenyewe ndiye atakomesha huo utawala wa chapa 666, NA HAO WAWILI YAANI MFAMLE NA NABII WAKE WAO UONGO WATAKUWA WA KWANZA KUTUPWA KWENYE ZIWA LA MOTO BILA KUFA KWA JINSI YA MWILI, WATATUPWA HAKIWA HAI K**A WALE WALIOJARIBU KUMPINGA MUSA WALIVYOZAMISHWA CHINI YA ARDHI WAKIWA HAI.
Ufunuo 19: 20 Yule mnyama akak**atwa, na yule nabii wa uongo pamoja naye, yeye aliyezifanya hizo ishara mbele yake, ambazo kwa hizo aliwadanganya watu wale walioipokea ile chapa ya huyo mnyama, nao walioisujudia sanamu yake; hao wawili wakatupwa *wangali hai* katika lile ziwa la moto liwakalo kwa kiberiti;
mfano sawa na wale waliompinga Musa (Numbers 16:30 Lakini Bwana akiumba kitu kipya, na hiyo nchi ikifunua kinywa chake na kuwameza, pamoja na wote walio nao, *nao washukia shimoni wali hai;* ndipo mtatambua ya kwamba watu hawa wamemdharau Bwana)
21 na wale waliosalia waliuawa kwa upanga wake yeye aliyeketi juu ya yule farasi, upanga utokao katika kinywa chake. Na ndege wote wakashiba kwa nyama zao.
KUMBUKA HAPO πYEYE SHETANI HAINGIZWI ZIWA LA MOTO BADO
4. UFUFUO WA KWANZA UNAFANYIKA NA KUANZA KWA UTAWALA WA MIAKA 1000
Ufunuo 20:6 Huo ndio ufufuo wa kwanza. Heri, na mtakatifu, ni yeye aliye na sehemu katika ufufuo wa kwanza; juu ya hao mauti ya pili haina nguvu; bali watakuwa makuhani wa Mungu na wa Kristo, nao watatawala pamoja naye hiyo miaka elfu.
NB: Utawala wa miaka 1000 utafanyika kwenye dunia hii hii ya sasa kabla ya uumbaji wa nchi mpya.
5. hiyo No 4 ndio inaambaatana na Kumfunga shetani shimoni kwa miaka 1000 kwanza, ili Yesu na watu wake walioshiriki ufufuo wa kwanza watawale dunia .
HIKI KIPENGELE NI CHA MUHIMU ILI KUTIMIZA UNABII ALIOPEWA DAUDI KUWA MZAO WAKE ATAKAA KWENYE KITI CHAKE CHA UFALME (UFALME WA DAUDI AMBAYE ALITAWAKA K**A MWANADAMU 100% AKIWA ANAONEKANA WAZI KWA WANDAMU NA SIO KWAMBA ALIKUWA ULIMWENGU MWINGINE. SO NAYE YESU ATAFANYA HIVYOHIVYO NA KUITAWALA DUNIA NZIMA, NA KUTIMIZA AHADI YA MUNGU KWA IBRAHIMU KUWA UZAO WAKE UTATAWALA DUNIA YOTE PHYSICALLY K**A AKINA DAUDI WALIVYOFANYA.
na kutimiza ahadi kwa Isreal juu ya kuja kwa Yesu k**a mfalme wao waliyetabiriwa. AHADII HII HADI LEO ISREAL WANAISUBIRI, kupata Mfamle atakayewaokoa na adui zao (mataifa mengine )
Luka 1: 70 K**a alivyosema tangu mwanzo Kwa kinywa cha manabii wake watakatifu;
71 Tuokolewe na adui zetu Na mikononi mwao wote wanaotuchukia;
72 Ili kuwatendea rehema baba zetu, Na kulikumbuka agano lake takatifu;
73 Uapo aliomwapia Ibrahimu, baba yetu,
74 Ya kwamba atatujalia sisi, Tuokoke mikononi mwa adui zetu, Na kumwabudu pasipo hofu,
75 Kwa utakatifu na kwa haki Mbele zake siku zetu zote.
Matendo 1: 6 Basi walipokutanika, wakamwuliza, wakisema, Je! Bwana, wakati huu ndipo unapowarudishia Israeli ufalme?
7 Akawaambia, Si kazi yenu kujua nyakati wala majira, Baba aliyoyaweka katika mamlaka yake mwenyewe.
π HIYO NDIO MITUME WALIDHANI INATAKIWA KUTIMIA BAADA TU YA YESU KUFUFUKUA. (WALIKUWA HAWAJUI KUWA KUNA NYAKATI ZINAITWA "NYAKATI/MAJIRA ZA MATAIFA" ambazo ziliingizwa katikati ya wiki 70 za unabii wa isreal/ Mungu alifanya temporary suspension ya hesabu ya wiki mpaka "MAJIRA YA MATAIFA" UTAKAPOTIMIA)
Nyakati za mataifa ndio hizi zilizopo sasa, ambazo zimeingizwa katikati ya majuma 70 ya Isreal, Baada nyakati za mataifa kuisha ndipo hesabu ya Majuma ya Isreal ita-resume.
Luka 21: 24 Wataanguka kwa ukali wa upanga, nao watatekwa nyara na kuchukuliwa katika mataifa yote; na Yerusalemu utakanyagwa na Mataifa, hata *majira ya Mataifa* yatakapotimia.
Romans 11:25 Kwa maana, ndugu zangu, sipendi msiijue siri hii, ili msijione kuwa wenye akili; ya kwamba kwa sehemu ugumu umewapata Israeli, mpaka utimilifu wa Mataifa uwasili.
NA HUO MUDA WA MIAKA 1000 YA YESU DUNIANI K**A MFALME WA DUNIA NDIO WAKATI AMBAO ISAYA 65:20-25 ITATIMIA PIAπ
Isaya 65: 20 Hatakuwapo tena mtoto wa siku chache, wala mzee asiyetimia siku zake; kwa maana mtoto atakufa mwenye umri wa miaka mia[MAANA YAKE MAUTI ITAKUWEPO K**A KAWAIDA KWAKUWA ITAKUWA KWENYE HII DUNIA YA SASA]; bali mtenda dhambi mwenye umri wa miaka mia atalaaniwa.[MAANA YAKE DHAMBI ITAKUWA IPO]
21 Nao watajenga nyumba, na kukaa ndani yake; watapanda mizabibu, na kula matunda yake.
22 Hawatajenga, akakaa mtu mwingine ndani yake; hawatapanda, akala mtu mwingine; maana k**a siku za mti ndivyo zitakavyokuwa siku za watu wangu, na wateule wangu wataifurahia kazi ya mikono yao muda wa siku nyingi.
23 Hawatajitaabisha kwa kazi bure, wala hawatazaa kwa taabu; kwa sababu wao ni wazao wa hao waliobarikiwa na Bwana, na watoto wao pamoja nao.
24 Na itakuwa ya kwamba, kabla hawajaomba, nitajibu; na wakiwa katika kunena, nitasikia.
25 Mbwa-mwitu na mwana-kondoo watalisha pamoja, na simba atakula majani k**a ng'ombe; na mavumbi yatakuwa chakula cha nyoka. Hawatadhuru wala kuharibu katika mlima wangu mtakatifu wote, asema Bwana.
6. baada ya huo Muda kuisha ndipo shetani atafunguliwa (ili tena wale UZAO WA ADAMU WA KWANZA waliozaliwa na kuishi nyakati za Yesu Nao wapate kujaribiwa, WANADAMU HAO WAKAJARIBU KUFANYA UASI, NA KUJARIBU KUUHARIBU ULE MJI ULIOSHUKA KUTOKA MINGUNI (MAKAO MAKUU YA UTAWALA WA YESU KWENYE DUNIA AMBAYO ITAKUWA BADO NI HII HII)
UFUNUO 20: 7 Na hiyo miaka elfu itakapokwisha, Shetani atafunguliwa, atoke kifungoni mwake;
8 naye atatoka kuwadanganya mataifa walio katika pembe nne za nchi, Gogu na Magogu, kuwakusanya kwa vita, ambao hesabu yao ni k**a mchanga wa bahari.
9 Wakapanda juu ya upana wa nchi, wakaizingira kambi ya watakatifu, na mji huo uliopendwa. Moto ukashuka kutoka mbinguni, ukawala.
7. THEN NDIPO SHETANI NAYE ANAUNGANISHWA KWENYE ZIWA LA MOTO, ANAKUWA NI KIUMBE WA TATU KIUNGIA HUMO
Ufunuo 20: 10 Na yule Ibilisi, mwenye kuwadanganya, akatupwa katika ziwa la moto na kiberiti, alimo yule mnyama na yule nabii wa uongo. Nao watateswa mchana na usiku hata milele na milele.
8. BAADA YA MAMBO HAYO NDIPO UFUFUO WA PILI UNATOKEA, KWA AJILI YA HUKUMU YA MILELE KWA KILA MWANADAMU NA KILA MALAIKA.
Daniel 12:2 Tena, wengi wa hao walalao katika mavumbi ya nchi wataamka, wengine wapate uzima wa milele, wengine aibu na kudharauliwa milele.
UFUNUO 20: 11 Kisha nikaona kiti cha enzi, kikubwa, cheupe, na yeye aketiye juu yake; ambaye nchi na mbingu zikakimbia uso wake, na mahali pao hapakuonekana.
12 Nikawaona wafu, wakubwa kwa wadogo, wamesimama mbele ya hicho kiti cha enzi; na vitabu vikafunguliwa; na kitabu kingine kikafunguliwa, ambacho ni cha uzima; na hao wafu wakahukumiwa katika mambo hayo yaliyoandikwa katika vile vitabu, sawasawa na matendo yao.
13 Bahari ikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake; na Mauti na Kuzimu zikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake. Wakahukumiwa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake.
14 Mauti na Kuzimu zikatupwa katika lile ziwa la moto. Hii ndiyo mauti ya pili, yaani, hilo ziwa la moto.
15 Na iwapo mtu ye yote hakuonekana ameandikwa katika kitabu cha uzima, alitupwa katika lile ziwa la moto.
1kor 6: 3 Hamjui ya kuwa [watu wa Yesu] mtawahukumu malaika, ?
9. BAADA YA No 8 ndipo AHADI YA MBINGU MPYA NA NCHI MPYA ITATIMIZWA NA MAANDIKO HAYA KUTIMIA
EBRANIA 1: 10 ... Wewe,Bwana,hapo mwanzo uliitia misingi ya nchi, Na mbingu ni kazi za mikono yako; 11 Hizo zitaharibika, bali wewe unadumu; Nazo zote zitachakaa k**a nguo, 12 Na k**a mavazi utazizinga, nazo zitabadilika;
2Peter 3:13 Lakini, k**a ilivyo ahadi yake, mnatazamia mbingu mpya na nchi mpya, ambayo haki yakaa ndani yake.
ufunuo 21:1 Kisha nikaona mbingu mpya na nchi mpya; kwa maana mbingu za kwanza na nchi ya kwanza zimekwisha kupita, wala hapana bahari tena.
____________
Ibrahim Nzunda
0784811512